Mithali 16:28-33, Mithali 17:1-4 NEN

Mithali 16:28-33

16:28 Mit 14:17; 17:9Mtu mpotovu huchochea ugomvi,

nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.

Mtu mkali humvuta jirani yake

na kumwongoza katika mapito yale mabaya.

16:30 Mit 6:13Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu;

naye akazaye midomo yake amenuia mabaya.

16:31 Mit 20:29Mvi ni taji ya utukufu;

hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

16:32 Mit 19:11Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa,

mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji.

16:33 Yos 7:14; Yn 1:7Kura hupigwa kwa siri,

lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.

Read More of Mithali 16

Mithali 17:1-4

17:1 Mit 15:16, 17; 16:8Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu

kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.

17:2 Mit 10:5; 19:26Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,

naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.

17:3 Mit 27:21; Yer 17:10; 1Pet 1:7; Za 26:2Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,

bali Bwana huujaribu moyo.

Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;

mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.

Read More of Mithali 17