Mithali 15:31-33, Mithali 16:1-7 NEN

Mithali 15:31-33

15:31 Mit 9:7-9; 12:1Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima

atakuwa miongoni mwa wenye hekima.

15:32 Mit 1:7; 12:1; Mhu 7:5Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe,

bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.

15:33 Mit 29:23; Isa 66:2Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima,

nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.

Read More of Mithali 15

Mithali 16:1-7

16:1 Mt 10:19; Mit 19:21Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu,

bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.

16:2 1Sam 16:7; 2Nya 6:30; Lk 16:15; Dan 5:27Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe,

bali makusudi hupimwa na Bwana.

16:3 2Nya 20:20; Za 20:4Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo,

nayo mipango yako itafanikiwa.

16:4 Isa 43:7; Kut 9:16; 2Nya 34:24; Rum 9:22Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe;

hata waovu kwa siku ya maangamizi.

16:5 Za 40:4; Mit 6:16; 11:20-21Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo.

Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.

16:6 Kut 20:20; Mit 14:16; Dan 4:26Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa;

kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.

16:7 Kol 1:10; Mwa 39:21; Za 105:15; Yer 39:12; 40:1; 42:12; Dan 1:9Njia za mtu zinapompendeza Bwana,

huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani.

Read More of Mithali 16