Mithali 15:1-10
15:1 Mit 25:15; 2Nya 10:7; 1Fal 12:7Jawabu la upole hugeuza ghadhabu,
bali neno liumizalo huchochea hasira.
15:2 Mit 12:23; Mhu 10:12; Za 59:7Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa,
bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
15:3 2Nya 16:9; Ay 34:21; Ebr 4:13; Mit 5:21; Yer 16:17Macho ya Bwana yako kila mahali,
yakiwaangalia waovu na wema.
15:4 Za 5:9; Mit 10:11; 12:18Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima,
bali ulimi udanganyao huponda roho.
Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake,
bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.
15:6 Mit 8:21; 10:16Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa,
bali mapato ya waovu huwaletea taabu.
15:7 Mit 15:2; 10:13Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa,
bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
15:8 Isa 61:8; Yer 6:20; Ay 35:13; Yn 9:31; Amo 5:22Bwana huchukia sana dhabihu za waovu,
bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.
15:9 Kum 7:13; 1Tim 6:11; Isa 51:1-7Bwana huchukia sana njia ya waovu,
bali huwapenda wale wafuatao haki.
15:10 Mit 15:13; 17:22Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia;
yeye achukiaye maonyo atakufa.