Mithali 14:4-14 NEN

Mithali 14:4-14

14:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

14:5 Kut 20:16; Za 12:2; Mit 6:19Shahidi mwaminifu hadanganyi,

bali shahidi wa uongo humimina uongo.

14:6 Mit 9:9; 17:24Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati,

bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.

Kaa mbali na mtu mpumbavu,

kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.

14:8 Lk 12:20; 1Kor 3:19; Mit 15:28; 21:29Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake,

bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

14:9 Mit 1:22; 10:23Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi,

bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.

Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe,

wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.

14:11 Za 72:7; Ay 8:15; Mit 3:33Nyumba ya mwovu itaangamizwa,

bali hema la mnyofu litastawi.

14:12 Rum 6:21; Mit 12:15; 16:25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,

bali mwisho wake huelekeza mautini.

14:13 Mhu 2:2; 7:3-6Hata katika kicheko moyo waweza kuuma,

nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.

14:14 2Nya 15:7; Mit 12:14Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao,

naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.

Read More of Mithali 14