Mithali 14:25-35 NEN

Mithali 14:25-35

14:25 Mit 12:17Shahidi wa kweli huokoa maisha,

bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.

14:26 Mit 19:23; Isa 33:6Yeye amchaye Bwana ana ngome salama,

na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.

14:27 Za 18:5; Mit 13:14Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

14:28 2Sam 19:7Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme,

bali pasipo watu mkuu huangamia.

14:29 Mhu 7:8-9; Mit 15:18; Yak 1:19Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi,

bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.

14:30 Ay 5:2; Mdo 7:9; Mit 12:4Moyo wenye amani huupa mwili uzima,

bali wivu huozesha mifupa.

14:31 Ay 31:15-16; Mit 17:5Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao,

bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

14:32 Za 34:21; Mit 6:15; Ay 13:15; 2Tim 4:18Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu,

bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.

14:33 Mit 2:6-10Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu

bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.

14:34 Mit 11:11Haki huinua taifa,

bali dhambi ni aibu kwa watu wote.

14:35 Es 8:2; Mt 25:14-30Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima,

bali ghadhabu yake humwangukia

mtumishi mwenye kuaibisha.

Read More of Mithali 14