Mithali 14:15-24
14:15 Mit 14:8Mtu mjinga huamini kila kitu,
bali mwenye busara hufikiria hatua zake.
14:16 Kut 20:20; Mit 22:3Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya,
bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.
14:17 Mit 28:25; 29:22Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu,
naye mtu wa hila huchukiwa.
Mjinga hurithi upumbavu,
bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.
14:19 Mit 11:29Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema,
nao waovu kwenye malango ya wenye haki.
14:20 Mit 19:4, 7Maskini huepukwa hata na majirani zao,
bali matajiri wana marafiki wengi.
14:21 Mit 11:12; 19:17; Za 41:1Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi,
bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.
14:22 Mit 4:16-17Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki?
Bali wale wanaopanga kilicho chema
hupata upendo na uaminifu.
Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida,
bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.
14:24 Mit 14:8Utajiri wa wenye hekima ni taji yao,
bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.