Mithali 13:10-19
13:10 Amu 19:30; Mit 9:9Kiburi huzalisha magomvi tu,
bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri.
13:11 Mit 10:2; 9:9; 20:21Fedha isiyo ya halali hupungua,
bali yeye akusanyaye fedha kidogo kidogo huongezeka.
13:12 Mit 10:11Kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua,
bali tumaini lililotimizwa ni mti wa uzima.
13:13 Hes 15:31; Kut 9:20; Mit 16:20; 2Nya 36:16Yeye anayedharau mafundisho anajiletea maangamizi,
bali yeye anayeheshimu agizo hupewa tuzo.
13:14 Mit 10:11; 14:27Mafundisho ya mwenye busara ni chemchemi ya uzima,
ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.
Ufahamu mzuri hupata upendeleo,
bali njia ya asiye mwaminifu ni ngumu.
13:16 Es 5:11; Mit 12:23Kila mwenye busara hutenda kwa maarifa,
bali mpumbavu hudhihirisha upumbavu wake.
13:17 Mit 10:26; 25:13Mjumbe mwovu huanguka kwenye taabu,
bali mjumbe mwaminifu huleta uponyaji.
13:18 Mit 15:31-32; Za 141:5Yeye anayedharau maonyo hupata umaskini na aibu,
bali yeye anayekubali maonyo huheshimiwa.
13:19 Mit 10:11Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi,
bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya.