Mithali 12:18-27
12:18 Za 57:4; Mit 25:18; 15:4Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,
bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
12:19 Zek 1:5, 6Midomo isemayo kweli hudumu milele,
bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
12:20 Rum 14:19Upo udanganyifu katika mioyo
ya wale ambao hupanga mabaya,
bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
12:21 Ay 4:7; Za 91:10; Rum 8:28Hakuna dhara linalompata mwenye haki,
bali waovu wana taabu nyingi.
12:22 1Fal 13:18; Ufu 22:15; Mit 11:20Bwana anachukia sana midomo idanganyayo,
bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
12:23 Mit 10:14; Za 38:5; 59:7; Mit 18:2Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,
bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
12:24 Mit 10:4; 1Fal 11:28Mikono yenye bidii itatawala,
bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
12:25 Mit 15:13; Isa 50:4Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,
bali neno la huruma humfurahisha.
12:26 Za 95:10Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,
bali njia ya waovu huwapotosha.
Mtu mvivu haoki mawindo yake,
bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.