Mithali 11:9-18 NEN

Mithali 11:9-18

11:9 Mit 12:6; Yer 45:5; Ay 8:13Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

11:10 2Fal 11:20; Mit 28:12; Es 8:15Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

11:11 Mit 14:34; 29:8Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

11:12 Mit 14:21; Ay 6:24Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

11:13 Law 19:16; 1Tim 5:13; Mit 20:19; 10:14Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

11:14 Mit 20:18; 24:6; 2Sam 15:34; 1Fal 12:1; Mit 20:18; 2Sam 15:34; Mit 15:22; 24:6; 1Fal 12:1Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

11:15 Mit 6:1; 17:18; 22:26-27Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

11:16 Mit 31:31Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

11:17 Mt 25:34Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

11:18 Hos 10:12; Kut 1:20; Ay 4:8Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

Read More of Mithali 11