Mithali 10:31-32, Mithali 11:1-8 NEN

Mithali 10:31-32

10:31 Mit 10:13; 15:2; 31:26; Za 52:4Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima,

bali ulimi wa upotovu utakatwa.

10:32 Mhu 10:12; Za 59:7Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa,

bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

Read More of Mithali 10

Mithali 11:1-8

11:1 Law 19:36; Ay 6:2; Mit 16:11; Eze 45:10Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

11:2 Dan 4:30; Mit 16:18; 18:12Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

11:3 Mit 13:6Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

11:4 Ay 20:20; Eze 7:19; Sef 1:18Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

11:5 1Fal 8:36; Mit 5:21-23; 13:6; 21:7Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

11:6 Es 7:9; 1Tim 4:8; Mhu 10:8Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

11:7 Ay 8:13; Mit 10:28Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

11:8 Mit 21:8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

Read More of Mithali 11