Mithali 10:21-30
10:21 Isa 5:13; Yer 5:4Midomo ya mwenye haki hulisha wengi,
lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
10:22 Mwa 12:2; 13:2; Za 37:22; Kum 8:17-18Baraka ya Bwana hutajirisha,
wala haichanganyi huzuni.
10:23 Mit 2:14Mpumbavu hufurahia tabia mbaya,
lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
10:24 Isa 66:4; Mt 5:6; Ay 15:21Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata;
kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
10:25 Za 20:8; Mt 7:24-27Tufani inapopita, waovu hutoweka,
lakini wenye haki husimama imara milele.
10:26 Isa 65:5; Mit 13:17; 25:13; 26:6Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho,
ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
10:27 Kum 11:9; Mit 22:4; Mhu 7:17; Ay 15:32Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha,
lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
10:28 Es 7:10; Ay 8:13; Za 16:9Tarajio la mwenye haki ni furaha,
bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
10:29 Za 10:12; Mit 21:15; Hos 14:9Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki,
lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
10:30 Za 37:28-29; Mit 2:20-22Kamwe wenye haki hawataondolewa,
bali waovu hawatasalia katika nchi.