Mithali 10:1-10 NEN

Mithali 10:1-10

Mithali Za Solomoni

10:1 1Fal 4:32; Mit 1:1; 15:20; 17:21; 19:13; 23:22; 27:11; 29:3Mithali za Solomoni:

Mwana mwenye hekima

huleta furaha kwa baba yake,

lakini mwana mpumbavu

huleta huzuni kwa mama yake.

10:2 Dan 4:27; Mit 13:11; 21:6; 12:28; Lk 12:29Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai,

lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.

10:3 Za 10:14; Mt 6:25-34Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa,

lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.

10:4 Mit 24:30-34; 13:4Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini

lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.

10:5 Mit 24:30-34Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi

ni mwana mwenye hekima,

lakini yeye alalaye wakati wa mavuno

ni mwana mwenye kuaibisha.

10:6 Es 7:8; Mit 13:3; Mhu 10:12Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki,

lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.

10:7 Mhu 8:10; Ay 18:17; Za 109:13Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka,

lakini jina la mwovu litaoza.

10:8 Ay 33:33; Mt 7:24-27Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo,

lakini mpumbavu apayukaye huangamia.

10:9 Za 23:4; 25:21; Isa 33:15; Mit 28:18Mtu mwadilifu hutembea salama,

lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.

10:10 Za 35:19Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni,

naye mpumbavu apayukaye huangamia.

Read More of Mithali 10