Mithali 1:20-33 NEN

Mithali 1:20-33

Onyo Dhidi Ya Kukataa Hekima

1:20 Ay 28:12; Mt 7:10-13; 9:1-3, 13-15Hekima huita kwa sauti kuu barabarani,

hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;

kwenye makutano ya barabara za mji

zenye makelele mengi hupaza sauti,

kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:

1:22 Mit 6:32; 7:7; 8:5; 9:4, 16; Za 50:17“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini?

Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha,

na wapumbavu kuchukia maarifa?

1:23 Yoe 2:28; Yn 7:37Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu,

ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu

na kuwafahamisha maneno yangu.

1:24 Isa 65:12; Zek 7:11Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita

na hakuna yeyote aliyekubali

niliponyoosha mkono wangu,

1:25 Lk 7:30kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote

na hamkukubali karipio langu,

1:26 Za 2:4; Kum 28:63; Mit 10:24mimi nami nitawacheka katika maafa yenu,

nitawadhihaki wakati janga litawapata:

1:27 Za 18:18; Mit 5:12-14wakati janga litawapata kama tufani,

wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,

wakati dhiki na taabu zitawalemea.

1:28 Isa 1:15; Mik 3:4; Eze 8:18; Hos 5:6“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;

watanitafuta lakini hawatanipata.

1:29 Ay 21:14; Isa 27:11; Mdo 7:51Kwa kuwa walichukia maarifa,

wala hawakuchagua kumcha Bwana,

1:30 Ay 21:14; Za 81:11kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,

na kukataa maonyo yangu,

1:31 2Nya 36:16; Yer 14:16watakula matunda ya njia zao,

na watashibishwa matunda ya hila zao.

1:32 Isa 66:4; Yer 2:19Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua,

nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.

1:33 Hes 24:21; Za 25:12; 112:8Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama,

atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

Read More of Mithali 1