Mithali 29:10-18
29:10 Mwa 4:5-8; 1Yn 3:12Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu
na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
29:11 Ay 15:13; Mit 12:16Mpumbavu huonyesha hasira yake yote,
bali mwenye hekima hujizuia.
29:12 2Fal 21:9; Ay 34:30Kama mtawala akisikiliza uongo,
maafisa wake wote huwa waovu.
29:13 Mit 22:2; Mt 5:45Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili:
Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
29:14 Mit 29:4; Za 72:1-5; Mit 16:12Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki,
kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
29:15 Mit 29:17; 13:24Fimbo ya maonyo hutia hekima,
bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo
humwaibisha mama yake.
29:16 Za 37:36; 58:10; 91:8Wakati waovu wanapostawi,
pia dhambi vivyo hivyo,
lakini wenye haki wataliona anguko lao.
29:17 Mit 13:24; 29:15Mrudi mwanao, naye atakupa amani,
atakufurahisha nafsi yako.
29:18 Za 19:11; Yn 13:17; Amo 8:11-12; 1Sam 3:1Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia,
bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.