Luka 9:57-62, Luka 10:1-24 NEN

Luka 9:57-62

Gharama Ya Kumfuata Yesu

(Mathayo 8:19-22)

9:57 Mt 8:19Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”

9:58 Mt 8:20Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”

9:59 Mt 4:19Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.”

Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”

9:60 Mt 3:2Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”

9:61 1Fal 19:20Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”

Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”

Read More of Luka 9

Luka 10:1-24

Yesu Awatuma Wale Sabini Na Wawili

10:1 Lk 7:13; 9:1-2, 51-52; Mk 6:7; Mt 10:1Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye. 10:2 Mt 9:37-38; Yn 4:35Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno. 10:3 Mt 10:16Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu. 10:4 Lk 9:3-5; 2Fal 4:29Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.

10:5 Mt 4:12“Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’ Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia. 10:7 Mt 10:10; 1Kor 9:14Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.

10:8 1Kor 10:27“Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu, 10:9 Mt 3:2; 10:7waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’ Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme: 10:11 Mt 10:14; Mk 6:11‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’ 10:12 Mt 10:15; 11:24Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.

Onyo Kwa Miji Isiyotubu

(Mathayo 11:20-24)

10:13 Lk 6:24-26; Ufu 11:3“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu. Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi. 10:15 Mt 4:13; Mwa 11:4; Kum 1:28; Isa 14:13; Yer 51:53Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.”

10:16 Mt 10:40; Yn 13:20“Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”

10:17 Mk 16:17Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”

10:18 Mt 4:10; Isa 14:12; Ufu 9:1Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi. 10:19 Mk 16:18; Mdo 28:3-5Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru. 10:20 Dan 12:1; Flp 4:3Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”

Yesu Anashangilia

(Mathayo 11:25-27; 13:16-17)

10:21 1Kor 1:26-29Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.

10:22 Mt 28:18; Yn 1:18“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”

10:23 Mt 13:16, 17 Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona. 10:24 1Pet 1:10-12Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”

Read More of Luka 10