Ayubu 33:1-33, Ayubu 34:1-37 NEN

Ayubu 33:1-33

Elihu Anamkemea Ayubu

33:1 Ay 32:10; 6:28; 13:6“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu;

zingatia kila kitu nitakachosema.

Karibu nitafungua kinywa changu;

maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.

33:3 Ay 27:4; 36:4Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu;

midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.

33:4 Mwa 2:7; Ay 10:3; 27:3Roho wa Mungu ameniumba;

pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.

33:5 Ay 13:18Unijibu basi, kama unaweza;

jiandae kunikabili mimi.

33:6 Ay 9:32; 4:19Mimi ni kama wewe mbele za Mungu;

mimi pia nimetolewa kwenye udongo.

33:7 Ay 13:21; 2Kor 2:4Huna sababu ya kuniogopa,

wala mkono wangu haupaswi kukulemea.

“Lakini umesema nikiwa ninakusikia,

nami nilisikia maneno yenyewe:

33:9 Ay 10:7; 9:30; 16:17‘Mimi ni safi na sina dhambi;

mimi ni safi na sina hatia.

33:10 Ay 13:24Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu,

naye ananiona kama adui yake.

33:11 Ay 13:27; Mit 3:6; Isa 30:21Ananifunga miguu kwa pingu,

tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’

33:12 Mhu 7:20; Za 8:4; Isa 55:8-9“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa,

kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.

33:13 Ay 40:2; Isa 45:9Kwa nini unamlalamikia

kwamba yeye hamjibu mwanadamu?

33:14 Za 62:11; Mwa 30:2; Mt 27:19Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja,

au wakati mwingine kwa njia nyingine,

ingawa mwanadamu anaweza asielewe.

33:15 Mwa 30:2; Mt 27:19Mungu husema na mwanadamu katika ndoto,

katika maono ya usiku,

wakati usingizi mzito uwaangukiapo

wanadamu wasinziapo vitandani mwao,

33:16 Ay 36:10anaweza akasemea masikioni mwao,

na kuwatia hofu kwa maonyo,

33:17 Ay 36:10, 15; 6:4; Za 88:15-16ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya

na kumwepusha na kiburi,

33:18 Yn 2:6; Zek 9:11; Ay 15:22; Mt 26:52kuiokoa nafsi yake na shimo,

uhai wake usiangamizwe kwa upanga.

33:19 Kum 8:5; Za 6:2; Isa 38:13Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake,

kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,

33:20 Za 102; 4; 107:18; Ay 3:24kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula

nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.

33:21 Ay 2:5; 16:8Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda,

nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika,

sasa inatokeza nje.

33:22 Ay 38:17; Za 9:13; 88:3; 107:18; 116:3Nafsi yake inakaribia kaburi,

nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.

33:23 Ay 36:9-10; Mik 6:8; Gal 3:19; Ebr 8:6; 9:15; Ay 36:9-10; Mik 6:8“Kama bado kuna malaika upande wake

kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu,

wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,

33:24 Isa 38:17kumwonea huruma na kusema,

‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni;

nimepata ukombozi kwa ajili yake’:

33:25 2Fal 5:14ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto;

hurudishwa upya kama siku za ujana wake.

33:26 Mit 8:35; 2Fal 20:2-5; Lk 2:52; Ezr 3:13; Za 13:5Humwomba Mungu, akapata kibali kwake,

huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha;

Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.

33:27 Hes 22:34; 2Sam 12:13; Ezr 9:13; Yak 2:13; Lk 15:21Ndipo huja mbele za watu na kusema,

‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki,

lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.

33:28 Kut 15:13; Za 34:22; 107:20; Ay 17:16; 22:20Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni,

nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’

33:29 Yer 10:23; Flp 2:13“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu;

mara mbili hata mara tatu,

33:30 Za 49:19; Isa 53:11; Zek 9:11ili aigeuze nafsi yake toka shimoni,

ili nuru ya uzima imwangazie.

33:31 Yer 23:18; Ay 32:10“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi;

nyamaza, nami nitanena.

33:32 Ay 6:29; 35:2Kama unalo lolote la kusema, unijibu;

sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.

33:33 Mit 10:8, 10, 19; Za 34:11Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi;

nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

Read More of Ayubu 33

Ayubu 34:1-37

Elihu Anatangaza Haki Ya Mungu

Kisha Elihu akasema:

34:2 Ay 32:10“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima;

nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.

34:3 Ay 12:11Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno

kama vile ulimi uonjavyo chakula.

34:4 1The 5:21Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa,

nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.

34:5 Ay 33:9; 6:29; 27:2; 9; 17“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia,

lakini Mungu ameninyima haki yangu.

34:6 Yer 10:19; Ay 10:3Ingawa niko sawa,

ninaonekana mwongo;

nami ingawa sina kosa,

kidonda changu hakiponi.’

34:7 Ay 9:21; 15:16Ni mtu gani aliye kama Ayubu,

anywaye dharau kama maji?

34:8 Ay 22:15; Za 50:18Ashirikianaye na watenda mabaya

na kuchangamana na watu waovu.

34:9 Ay 9:29-31Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote

anapojitahidi kumpendeza Mungu.’

34:10 Mwa 18:25; Za 92:15; Rum 3:5“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu.

Kamwe Mungu hatendi uovu,

Mwenyezi hafanyi kosa.

34:11 Ay 21:31; 2Kor 5:10; Yer 17:10; Eze 33; 20; Mit 24:12Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda;

huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.

34:12 Za 9:16; Kol 3:25Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa,

kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.

34:13 Ay 36:23; Isa 40:14Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia?

Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?

34:14 Hes 16:22; Za 104:29; Mhu 12:7Kama lilikuwa kusudi la Mungu,

naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,

34:15 Za 90:10; Mwa 2:7wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja,

na mtu angerudi mavumbini.

34:16 Ay 32:10; 34:30“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili;

sikilizeni hili nisemalo.

34:17 Mwa 18:23; 2Sam 23:3-4; Mit 20:8; Rum 3:5-7; Ay 10:7Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala?

Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?

34:18 Kut 22:28; Isa 40:24Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’

nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’

34:19 Kum 10:17; Mdo 10:34; Law 19:15; Yak 2:5yeye asiyependelea wakuu,

wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini,

kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?

34:20 Kut 11:4; 12:29; Ay 12:19Wanakufa ghafula, usiku wa manane;

watu wanatikiswa nao hupita;

wenye nguvu huondolewa

bila mkono wa mwanadamu.

34:21 Mit 15:3; Ebr 4:13“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu;

anaona kila hatua yao.

34:22 Za 74:20; Ay 3:5; Amo 9:2-3Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa,

ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.

34:23 Ay 11:11; Ezr 9:13Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana,

ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.

34:24 Ay 12:19; Dan 2:21Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi

na kuwaweka wengine mahali pao.

34:25 Ay 11:11; Mit 5:21-23Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote,

huwaondoa usiku, nao wakaangamia.

34:26 Mwa 6:5; Ay 8:22; 28:24; Za 9:5; Yer 44:5Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao

mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,

34:27 Za 14:3; Isa 5:12; 1Sam 15:11kwa sababu wameacha kumfuata Mungu,

nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.

34:28 Kut 22:23; Yak 5:4; Mhu 5:8Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake,

hivyo akasikia kilio cha wahitaji.

34:29 Za 28:1; 83:1; 109:1; Rum 8:34; Za 13:1; 97:9; 83:18Lakini kama akinyamaza kimya,

ni nani awezaye kumhukumu?

Kama akiuficha uso wake,

ni nani awezaye kumwona?

Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,

34:30 Za 25:15; Mit 29:2-12; 1Fal 12:28-30ili kumzuia mtu mwovu kutawala,

au wale ambao huwategea watu mitego.

“Kama mwanadamu akimwambia Mungu,

‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.

34:32 Kut 33:13; Za 27:11; Lk 19:8; Ay 33:27Nifundishe nisichoweza kuona;

kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’

34:33 Mit 17:23; Yn 3:8Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako,

wakati wewe umekataa kutubu?

Yakupasa wewe uamue, wala si mimi;

sasa niambie lile ulijualo.

“Wanadamu wenye ufahamu husema,

wenye hekima wanaonisikia huniambia,

34:35 Ay 35:16; 38:2; 42:3; 26:3‘Ayubu huongea bila maarifa;

maneno yake hayana busara.’

34:36 Ay 6:29; 22:15Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho,

kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!

Kwenye dhambi yake huongeza uasi;

kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu,

na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

Read More of Ayubu 34