Ayubu 15:1-35, Ayubu 16:1-22, Ayubu 17:1-16, Ayubu 18:1-21 NEN

Ayubu 15:1-35

Elifazi Anaongea: Ayubu Anadhoofisha Imani

15:1 Ay 4:1Kisha Elifazi Mtemani akajibu:

15:2 Mwa 41:6; Ay 6:26“Je, mtu mwenye hekima hujibu kwa mawazo matupu,

au kujaza tumbo lake kwa upepo wenye joto wa mashariki?

15:3 Neh 4:2-3; Ay 6:26Je, aweza kubishana juu ya maneno yasiyofaa,

kwa hotuba zisizo na maana?

15:4 Ay 25:6Lakini unadhoofisha hata uchaji wa Mungu

na kuzuia ibada mbele za Mungu.

15:5 Ay 11:6; 22:5; 5:13; Mt 16:23Dhambi yako inasukuma kinywa chako,

nawe umechagua ulimi wa hila.

15:6 Za 10:2; Mt 12:37; Lk 19:22; Ay 7:15; 18:7Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si changu;

midomo yako mwenyewe inashuhudia dhidi yako.

15:7 Ay 38:21; 1Sam 2:8; Mit 8:25; Za 90:2“Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa?

Ulizaliwa kabla ya vilima?

15:8 Yer 23:18; 1Kor 2:11Je, wewe husikiliza mashauri ya siri ya Mungu?

Je, wewe unaizuia hekima iwe yako mwenyewe?

15:9 Ay 12:3Wewe unajua kitu gani tusichokijua sisi?

Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?

15:10 Ay 12:12; 32:6-7; 8:8-10Wale wenye mvi na wazee wako upande wetu,

watu ambao ni wazee hata kuliko baba yako.

15:11 Mwa 37:35; 2Kor 1:3-4; Kum 8:3; Yer 15:16Je, faraja za Mungu hazikutoshi,

au maneno yaliyosemwa kwako kwa upole si kitu?

15:12 Ay 11:13; 36:13Kwa nini moyo wako unakudanganya,

na kwa nini macho yako yanangʼaa,

15:13 Mit 29:11; Dan 11:30; Za 94:4; Ay 11:8; 22:5; 30:2ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu,

na kumwaga maneno kama hayo kutoka kinywani mwako?

15:14 Ay 14:1; 4:17; 2Nya 6:36; Mhu 7:18, 20“Mwanadamu ni kitu gani, hata aweze kuwa safi,

au yeye aliyezaliwa na mwanamke, hata aweze kuwa mwadilifu?

15:15 Ay 5:1; 4:18Kama Mungu hawaamini watakatifu wake,

kama hata mbingu zenyewe si safi machoni pake,

15:16 Law 5:2; Ay 12:4; 20:12; Mit 19:28; Za 14:1sembuse mwanadamu ambaye ni mwovu na mpotovu,

ambaye hunywa uovu kama anywavyo maji!

15:17 Ay 4:8“Nisikilize mimi nami nitakueleza,

acha nikuambie yale niliyoyaona,

15:18 Kum 32:7; Ay 8:8; Mwa 18:19ambayo watu wenye hekima wameyanena,

bila kuficha lolote walilopokea toka kwa baba zao

15:19 Mwa 12:1; Ay 22:8(wakati ambao wao peke yao ndio walipewa nchi,

hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao):

15:20 Oba 1:15; Sef 1:17Mtu mwovu siku zake zote hupata mateso,

miaka yote aliwekewa mkorofi.

15:21 1Sam 3:11; Yer 6:25; Isa 13:3; 1The 5:3Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake;

katika kufanikiwa kwake, wanyangʼanyi humshambulia.

15:22 Hos 9:13; Amo 5:19Hukata tamaa kuokoka gizani;

amewekwa kwa ajili ya upanga.

15:23 Za 59:15; 109:10; Ay 18:12Hutangatanga, akitafuta chakula;

anajua kwamba siku ya giza iko karibu.

15:24 Isa 8:22; 9:1; Ay 15:20; 18:14Taabu na maumivu makuu vinamtia hofu;

humshinda kama mfalme aliye tayari kwa vita,

15:25 Za 2:2-3; Mit 21:30kwa sababu amemkunjia Mungu ngumi yake

na kujigamba dhidi ya Mwenyezi,

15:26 Yer 44:16kwa kiburi akishambulia dhidi ya Mungu

akiwa na ngao nene, iliyo imara.

15:27 Amu 3:17; Za 17:10“Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene

na kiuno chake kimevimba kwa kunenepa,

15:28 Isa 5:9; Ay 3:14ataishi katika miji ya magofu,

na katika nyumba ambazo haziishi mwanadamu yeyote,

nyumba zinazokuwa vifusi.

15:29 Ay 3:15; 7:8; Isa 5:8Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu,

wala mali zake hazitakuwa nyingi juu ya nchi.

15:30 Ay 4:9, 15; 16:7; 20:26; Kut 15:10Hatatoka gizani;

mwali wa moto utanyausha machipukizi yake,

nayo pumzi ya kinywa cha Mungu itamwondolea mbali.

15:31 Yer 7:4-8; Mt 6:19; Za 62:1015:31 Ay 31:5; Mit 1:16; 6:18; Isa 44:20; 59:7; Mik 2:11; Mk 13:5Asijidanganye mwenyewe kutumainia ubatili,

kwa kuwa hatapata malipo yoyote.

15:32 Mhu 7:17; Za 109:8; Mit 10:27; Ay 18:16Atakuwa amelipwa kikamilifu kabla ya wakati wake,

nayo matawi yake hayatastawi.

15:33 Hab 3:17Atafanana na mzabibu uliopukutishwa matunda yake kabla hayajaiva,

kama mzeituni unaodondosha maua yake.

15:34 Kut 23:8; Ay 8:22; Isa 33:14Kwa kuwa jamii ya wasiomcha Mungu watakuwa tasa,

nao moto utateketeza hema za wale wanaopenda rushwa.

15:35 Hos 10:13; Gal 6:7; Za 7:14Hutunga mimba ya madhara na kuzaa uovu;

matumbo yao huumba udanganyifu.”

Read More of Ayubu 15

Ayubu 16:1-22

Hotuba Ya Tano Ya Ayubu

Ayubu Anathibitisha Tena Hali Yake Ya Kutokuwa Na Hatia

Kisha Ayubu akajibu:

16:2 Ay 6:15; 13:4; Za 69:20“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya,

nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!

16:3 Ay 6:26; 11:2; 18:2Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho?

Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?

16:4 Mt 27:29; Yer 18:16; Mao 2:15Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi,

kama mngekuwa katika hali yangu;

ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu,

na kuwatikisia ninyi kichwa changu.

16:5 Ay 29:25; Mwa 37:35Lakini kinywa changu kingewatia moyo;

faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.

16:6 Ay 6:3; 7:21“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi;

nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.

16:7 Amu 8:5; Ay 7:3; 1:19Ee Mungu, hakika umenichakaza;

umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.

16:8 Mao 5:17; Ay 10:17; 17:7; 19:20; Za 22:17; 88:9; 6:7Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi;

nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.

16:9 Ay 12:14; 13:24; Mao 2:16; Mdo 7:54; Hos 6:1; Ay 30:21; 9:5; 18:4; 19:11Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake,

na kunisagia meno yake;

adui yangu hunikazia macho yake makali.

16:10 Za 22:13; Mao 3:30; Mdo 7:57; 23:2; Za 27:3; Mik 5:1Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki;

hunipiga shavuni mwangu kwa dharau,

na kuungana pamoja dhidi yangu.

16:11 Ay 9:24Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya,

na kunitupa katika makucha ya waovu.

16:12 Ay 9:17; 6:4; Mao 3:12Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja;

amenikamata shingo na kuniponda.

Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;

16:13 Mit 7:23; Mao 3:13wapiga upinde wake wananizunguka.

Bila huruma, huchoma figo zangu,

na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.

16:14 Ay 9:17; 10:3; Yoe 2:7Huniponda tena na tena;

hunishambulia kama shujaa wa vita.

16:15 Mwa 37:34; Ay 2:8“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu

nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.

16:16 Ay 16:20; 2:7; 17:7; 30:17, 30; Isa 52:14; Za 6:6Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia,

macho yangu yamepigwa na giza kuu.

16:17 Yer 18:11; Yon 3:8Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri,

na maombi yangu ni safi.

16:18 Mwa 4:10; Ay 27:9; Isa 26:21; Za 66:18-19; Ebr 11:4“Ee nchi, usiifunike damu yangu,

nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.

16:19 Mwa 31:50; Rum 1:9; 1The 2:5; Ay 22:12; 19:27; Za 113:5; Isa 33:5Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni;

wakili wangu yuko juu.

16:20 Mao 2:19; Rum 8:34; Yn 15:15; Ay 16:16Mwombezi wangu ni rafiki yangu

macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;

16:21 1Fal 8:45; Za 140:12kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu

kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.

16:22 Ay 10:21; Mhu 12:5“Ni miaka michache tu itapita

kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

Read More of Ayubu 16

Ayubu 17:1-16

17:1 Za 88:3-4; Mhu 12:1-7Moyo wangu umevunjika,

siku zangu zimefupishwa,

kaburi linaningojea.

17:2 1Sam 1:6-7; Ay 11:3Hakika wenye mizaha wamenizunguka;

macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.

Ayubu Anaomba Msaada

17:3 Za 35:27; 40:17; Mit 6:1; Isa 38:14“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai.

Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?

17:4 Ay 12:12Umezifunga akili zao zisipate ufahamu,

kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.

17:5 Kut 22:15; Ay 11:20Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira,

macho ya watoto wake yatashindwa kuona.

17:6 1Fal 9:7; Yer 15:4“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu,

mtu ambaye watu humtemea mate usoni.

17:7 Ay 16:8; 2:12; 16:16Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi;

umbile langu lote ni kama kivuli.

17:8 Kut 4:14; Ay 22:19Watu wanyofu wanatishwa na hili;

watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.

17:9 Mit 4:18; 2Sam 22:21; Ay 22:30Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao,

nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.

17:10 Ay 12:3“Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena!

Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.

17:11 Ay 17:15; Isa 38:10; Ay 7:6Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika,

vivyo hivyo shauku za moyo wangu.

17:12 Isa 50:11; Ay 5:17-26; 11:17Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana,

kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’

17:13 2Sam 14:14; Ay 3:13; Za 139:8; 88:18Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi,17:13 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

kama nikikitandika kitanda changu gizani,

17:14 Ay 13:28; 30:28, 30; 4:19; 7:5; Za 16:10; 49:9; 17:15; Ay 7:6; Za 31:23; Mao 3:18; Eze 37:11kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’

na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’

liko wapi basi tarajio langu?

Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?

17:16 Mwa 2:7; Yon 2:6; Ay 3:17Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti?17:16 Malango ya mauti hapa ina maana ya Kuzimu.

Je, tutashuka pamoja mavumbini?”

Read More of Ayubu 17

Ayubu 18:1-21

Bildadi Anasema: Mungu Huwaadhibu Waovu

18:1 Ay 8:1Bildadi Mshuhi akajibu:

18:2 Ay 8:2; 16:3“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya?

Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.

18:3 Za 73:22; Ay 12:7Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama,

na kuonekana wajinga machoni pako?

18:4 Ay 13:14; 16:9; 14:18Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande

katika hasira yako,

je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe?

Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?

18:5 Yer 25:10; Yn 8:12; Mit 13:9“Taa ya mwovu imezimwa,

nao mwali wa moto wake umezimika.

18:6 Ay 8:22; 5:14; 11:17; 12:25Mwanga hemani mwake umekuwa giza;

taa iliyo karibu naye imezimika.

18:7 Za 18:36; Mit 4:12; Ay 5:13; 15:6Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa;

shauri lake baya litamwangusha.

18:8 Mik 7:2; Hab 1:15Miguu yake imemsukumia kwenye wavu,

naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.

18:9 Ay 22:10; 30:12; Isa 24:18; Yer 48:44; Amo 5:14; Mit 7:22Tanzi litamkamata kwenye kisigino;

mtego utamshikilia kwa nguvu.

18:10 Mit 7:22; Isa 51:20; 1Sam 28:9; Za 140:5Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;

mtego uko kwenye njia yake.

18:11 Ay 15:21; 20:8; Za 31:13; Isa 22:18; Yer 6:25Vitisho vimemtia hofu kila upande,

na adui zake humwandama kila hatua.

18:12 Isa 9:20; 65:13; 8:21; Ay 21:17; 31:3; 15:25Janga linamwonea shauku;

maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.

18:13 Zek 14:12; Hes 12:12Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake;

mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.

18:14 Ay 8:22; 15:24; 18:11Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake,

na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

18:15 Mwa 19:24; Za 11:6; Ay 18:18; 20:26Moto utakaa katika hema lake;

moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.

18:16 Hos 5:12; Amo 2:9; Mwa 27:28Mizizi yake chini itakauka

na matawi yake juu yatanyauka.

18:17 Mit 2:22; 10:7; Isa 49:15; Kum 32:26; 9:14; Za 9:5; 69:28Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia,

wala hatakuwa na jina katika nchi.

18:18 Ay 5:14; 18:11; 11:20; 30:8Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani,

naye amefukuzwa mbali atoke duniani.

18:19 Za 37:28; 21:10; Isa 14:22; Ay 27:14-15Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake,

wala aliyenusurika mahali alipoishi.

18:20 Yer 46:21; Eze 7:7Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata;

watu wa mashariki watapatwa na hofu.

18:21 Ay 21:28; Yer 9:3; 1The 4:5Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu;

ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

Read More of Ayubu 18