Wagalatia 2:1-10 NEN

Wagalatia 2:1-10

Paulo Akubaliwa Na Mitume

2:1 Mdo 15:2; 4:36; 2Kor 2:13Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami. 2:2 Mdo 15:4; 12; 1Kor 9:24; Flp 2:16Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure. 2:3 2Kor 2:13; Mdo 16:3; 1Kor 9:21Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa. 2:4 2Kor 11:26; Yud 24; Mdo 15:1; Gal 5:1, 13Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani, 2:5 Gal 2:14; 3:1; 4:16hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.

2:6 Gal 6:3; Mdo 10:34Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote. 2:7 1The 2:4; 1Tim 1:11; Mdo 9:15Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi. 2:8 Mdo 1:25; 1Kor 1:1; Mdo 9:15; 13:2; 22:21Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa. 2:9 1Tim 3:15; Mdo 4:36; Rum 12:3; Mdo 15:13; Gal 2:7, 11, 14; 1Tim 3:15; Ufu 3:12Basi, Yakobo, Kefa2:9 Yaani Petro, pia mstari 11, 14. na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi. 2:10 Mdo 24:17; 11:30; 12:25; Rum 15:25; 1Kor 16:1; 2Kor 8:9Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.

Read More of Wagalatia 2