Kutoka 19:1-25, Kutoka 20:1-26 NEN

Kutoka 19:1-25

Waisraeli Kwenye Mlima Sinai

19:1 Kut 6:6; Hes 3:14; 33:15Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai. 19:2 Kut 17:1; 36:1; Kum 5:2-4Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.

19:3 Kut 20:21; 3:4; 25:22; Mdo 7:38Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli: 19:4 Kum 29:2; Yos 24:7; Kum 32:11; Za 103:5; Isa 40:31; Yer 4:13; 48:40; Ufu 12:14; Kum 33:12; Isa 31:5; Eze 16:6‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu. 19:5 Kut 15:26; Kum 6:3; Za 78:10; Yer 7:23; Mwa 17:9; Kut 3:1; 8:22; 34:9; Kum 1:8; Tit 2:14; Kut 9:29; 1Kor 10:26Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu, 19:6 Isa 61:6; 66; 21; 1Pet 2:5; Mwa 18:19; Law 11:45; Kum 4:27; 7:6; 26:19; 28:9; 29:13; 33:3; Isa 4:3; 62:12; Yer 2:3; Amo 3:2ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”

19:7 Kut 18:12; Law 4:15; 9:1; Hes 16:25; Kut 4:30; Isa 8:10Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme. 19:8 Kut 24:3-7; Kum 5:27; 26:17Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.

19:9 Kut 20:21; 24:15-16; 33:9; 34:5; Kum 4:11; 2Sam 22:10-12; 2Nya 6:1; Kut 4:5; Za 18:11; 97:2; 99:7; Mt 17:5; Kum 4:12, 36; Yn 12:29-30Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.

19:10 Law 11:44; Hes 11:18; Isa 16:5; Yoe 2:16; Ebr 10:22; Mwa 35:2; Ufu 22:14Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao 19:11 Mwa 11:5; Kut 3:1; 24:16; 31:18; 34:2-4, 29-32; Law 7:38; 26:46; 27:34; Hes 3:1; Dan 10:5; Neh 9:13; Gal 4:24-25na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote. Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa. 19:13 Ebr 12:20; Yos 6:4; 1Nya 15:28; Za 81:3; 98:6; Kut 34:3Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”

19:14 Mwa 35:2Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao. 19:15 1Sam 21:4; 1Kor 7:5Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”

19:16 1Sam 2:10; Isa 29:6; Ebr 12:18-19; Ufu 4:1; Mwa 3:10; 1Sam 13:7; 14:15; 28:5; Za 99:1; Ebr 12:21Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka. 19:17 Kum 4:11Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima. 19:18 Kut 20:18; Za 104:32; Isa 6:4; Ufu 15:8; Kut 3:2; 24:17; Law 9:24; Kum 4:11, 24, 33; 5:4; 9:3; 1Fal 18:24, 38; 1Nya 21:26; 2Nya 7:1; Za 18:8; Ebr 12:18; Mwa 19:28; Ufu 9:2; Amu 5:5; 2Sam 22:8; Za 68:8; Isa 2:19; 5:25; 41:15; 64:1; Yer 4:24; 10:10; Mik 1:4; Nah 1:5; Hab 3:6-10; Hag 2:6Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi, 19:19 Kum 4:33; Neh 9:13; Za 81:7nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.

Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu, 19:21 Kut 24:10-11; Hes 4:20; 1Sam 6:19naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa. 19:22 Law 10:3; 1Sam 16:5; 2Nya 29:5; Yoe 2:16; 2Sam 6:7Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”

Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’ ”

19:24 Kut 24:1, 9Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”

Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.

Read More of Kutoka 19

Kutoka 20:1-26

Amri Kumi

(Kumbukumbu 5:1-21)

20:1 Kum 10:4; Neh 9:13; Za 119:9; 147:19; Mal 4:4Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:

20:2 Mwa 17:7; Kut 16:12; Law 19:2; 20:7; Isa 43:3; Eze 20:19; Mwa 15:7; Kut 6:6; 13:3; Eze 20:6“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.

20:3 Kut 34:14; Kum 6:14; 13; 10; 2Fal 17:35; Za 44:20; 81:9; Yer 1:16; 7:6-9; 11:13; 19:4; 25:6Usiwe na miungu mingine ila mimi.

20:4 Kut 32:8; 34:17; Law 19:4; 26:1; Kum 4:15-23; 27:15; 2Sam 7:22; 1Fal 14:9; 2Fal 17:12; Isa 42:8; 44:9Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji. 20:5 Kut 23:13; Yos 23:7; Amu 6:10; 2Fal 17:35; Isa 44:15-19; 46:6; Kut 34:14; Kum 4:24; Yos 24:19; Mwa 9:25; Law 26:39; Kut 34:7; Hes 14:18; Yer 32:18Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 20:6 Kut 34:7; Hes 14:18; Kum 7:9; Yer 32:18; Lk 1:50; Rum 11:28lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.

20:7 Kut 22:28; Law 18:21; 19:12; 22:2; 24:11, 16; Kum 6:13; 10:20; Ay 2:5-9; Za 63:11; Isa 8:21; Eze 20:39; 39:7; Mt 5:33Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.

20:8 Kut 16:23; 31:13-16; 35:3; Law 19:3, 30; 26:2; Isa 56:2; Yer 17:21-27; Eze 22:8Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase. 20:9 Kut 23:12; 31:13-17; 34:21; 35:2-3; Law 23:3; Lk 13:14Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote, 20:10 Mwa 2:3; Kut 31:14; Law 23:38; Hes 28:9; Isa 56:2; Eze 20:12, 20lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 20:11 Mwa 1:3–2:1; 2:2; Kut 31:17; Eze 4:4Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.

20:12 Kum 5:16; Mt 15:4; 19:19; Mk 7:10; 10:19; Lk 18:20; Efe 6:2; Kum 6:2; Efe 6:3; Kum 11:9; 25:15; Yer 35:7Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.

20:13 Mwa 4:23; Mt 5:21; 19:18; Lk 18:20; Rum 13:8-9; Yak 2:11Usiue.

20:14 Law 18:20; 20:10; Hes 5:12, 13, 29; Mit 6:29-32; Mt 5:27; 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usizini.

20:15 Law 19:11-13; Eze 18:7; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9Usiibe.

20:16 Law 19:11; Yer 9:3-5; Kut 23:1, 7; Law 19:18; Za 50:20; 101:5; 119:29; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 3:14; 18:20Usimshuhudie jirani yako uongo.

20:17 Lk 12:15; Rum 7:7; 13:9; Efe 5:3; Ebr 13:5Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”

Watu Wanaogopa

(Kumbukumbu 5:22-33)

20:18 Kut 19:16-19; Kum 4:36; Isa 58:1; Yer 6:17; Eze 33:3; Ebr 12:1-19; Ufu 1:10; Kut 19:18; Mwa 3:10; Kut 14:31; 19:16Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali 20:19 Ay 37:4-5; 40:9; Za 29:3-4; Kum 5:23-27; 18:16; Gal 3:19na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”

20:20 Mwa 15:1; 22:1; Kum 4:10; 6:2; 10:12; Za 111:10; 128:1; Mit 1:7; Mhu 12:13; Isa 8:13; Ay 1:8; 2:3; 28:28; Mit 3:7; 8:13; 14:16; 16:6Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”

20:21 Kut 19:9; Kum 5:22; Za 81:8; 68:4; 97:2; Isa 19:1Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.

Sanamu Na Madhabahu

20:22 Kum 5:24-26; Neh 9:13Kisha Bwana akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimesema nanyi kutoka mbinguni: 20:23 Kut 22:20; 32:4, 8; 34:17; Kum 29:17-18; Neh 9:18Msijifanyizie miungu yoyote na kuilinganisha nami, msijitengenezee miungu ya fedha wala miungu ya dhahabu.

20:24 Kut 27:1; 40:29; Hes 16:38; Kum 27:5; Yos 8:30; 2Fal 16:14; 2Nya 4:1; Eze 43:13; Mwa 8:20; Kut 18:12; Kum 12:5; 16:6, 11; 26:2; 1Fal 9:3; 2Fal 21:4-7; 2Nya 6:6; 12:13; Ezr 6:12; Mwa 12:2; 22:17“ ‘Utanitengenezea madhabahu ya udongo, na juu yake utoe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani, kondoo zako, mbuzi na ngʼombe zako. Popote nitakapofanya Jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki. 20:25 Yos 8:31; 1Fal 6:7Ikiwa unanitengenezea madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia chombo cha kuchongea mtaitia unajisi. 20:26 Eze 43:17Msitumie ngazi kupandia kwenye madhabahu yangu, uchi wako usije ukadhihirika kwa chini.’

Read More of Kutoka 20