Waefeso 4:17-32, Waefeso 5:1-7 NEN

Waefeso 4:17-32

Maisha Ya Zamani Na Maisha Mapya

4:17 Rum 1:21Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao. 4:18 Rum 1:21; Efe 2:12; 2Kor 3:14Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao. 4:19 1Tim 4:2; Rum 1:24; Kol 3:5Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.

Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo. 4:21 Efe 1:13Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu. 4:22 1Pet 2:1; Rum 6:6Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu, 4:23 Kol 3:10ili mfanywe upya roho na nia zenu, 4:24 Rum 6:4; Efe 2:10mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.

Kanuni Za Maisha Mapya

4:25 Law 19:11; Rum 12:15Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja. 4:26 Za 4:4; Yak 1:19, 20; Mt 5:22Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika, 4:27 Yak 4:7; 1Pet 5:9wala msimpe ibilisi nafasi. 4:28 Mdo 20:35; 1The 4:11; Lk 3:11Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.

4:29 Kol 3:8; Mt 12:36; Efe 5:4; Kol 3:8; 4:6; 1The 5:11Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao. 4:30 1The 5:19; Rum 8:23Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi. 4:31 Kol 3:8; Tit 3:2; Yak 4:11; 1Pet 2:1; Tit 3:3Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu. 4:32 Mt 6:14, 15Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Read More of Waefeso 4

Waefeso 5:1-7

Kuenenda Nuruni

5:1 Lk 6:36; Mt 5:45; 8; Lk 6:26; Efe 4:32Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao, 5:2 Gal 1:4; 2Kor 6:15; Ebr 7:27mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.

5:3 Kol 3:5; 1Kor 6:18; Efe 4:29Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu. 5:4 Mt 12:35; Efe 4:29; Rum 1:28; Kol 3:8Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu. 5:5 Kol 3:5; 1Kor 6:9Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu. 5:6 Rum 1:18; Kol 2:4, 8; Yer 29:8; Mt 24:4; Kol 2:4, 8, 18; 2The 2:3; Rum 1:1Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii. Kwa hiyo, msishirikiane nao.

Read More of Waefeso 5