Waefeso 4:1-16 NEN

Waefeso 4:1-16

Umoja Katika Mwili Wa Kristo

4:1 Efe 3:1; Kol 1:10; 1The 2:12Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa. 4:2 Kol 3:12, 13; Efe 1:4Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo. 4:3 Kol 3:14; Rum 15:5Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 4:4 1Kor 12:13Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja. 4:5 1Kor 8:6; 2Kor 11:4; Yud 3; Gal 3:27, 28; Ebr 6:6Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja, 4:6 Rum 11:36; 1Kor 12:6; Mal 2:10; 1Kor 8:6; 12:6; Rum 11:36Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.

4:7 1Kor 12:7, 11; Rum 12:3Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo. 4:8 Kol 2:15; Za 68:18Kwa hiyo husema:

“Alipopaa juu zaidi, 4:8 Juu zaidi hapa ina maana mbingu za mbingu.

aliteka mateka,

akawapa wanadamu vipawa.”

4:9 Yn 3:13; 6:33, 62(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?4:9 Pande za chini sana za dunia hapa maana yake Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu. 4:10 Mdo 1:9, 11; 1Tim 3:16; Ebr 4:14; 7:26; 9:24; Mdo 2:13; Mit 30:1-4; Efe 1:23Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.) 4:11 2Pet 3:2; Mdo 21:8Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu, 4:12 1Kor 12:27; 1Pet 2:5; 2Tim 3:17kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa 4:13 Kol 1:28mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.

4:14 1Kor 14:20; Yn 1:6; Efe 6:11Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu. 4:15 Efe 1:22Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo. 4:16 Kol 2:19Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.

Read More of Waefeso 4