2 Wakorintho 5:11-21, 2 Wakorintho 6:1-2 NEN

2 Wakorintho 5:11-21

Huduma Ya Upatanisho

5:11 Ay 23:15; Ebr 10:31; 12:29; Yud 23; 2Kor 4:2Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia. 5:12 2Kor 3:1; 1:14Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni. 5:13 2Kor 11:1, 16-17; 12:11Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu. 5:14 Rum 6:6-7; Gal 2:20; Kol 3:3Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa. 5:15 Rum 14:7-9; 4:25Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.

5:16 2Kor 10:4; 11:18Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo. 5:17 Rum 16:3; Yn 1:13; Rum 6:4; Gal 6:15; Isa 65:17; Ufu 21:4-5Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya. 5:18 Rum 11:36; 5:10Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho: Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho. 5:20 2Kor 6:1; Efe 6:20; Isa 27:5Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu. 5:21 Ebr 4:15; 7:26; 1Pet 2:22-24; 1Yn 3:5; Rum 1:17; 1Kor 1:30Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.

Read More of 2 Wakorintho 5

2 Wakorintho 6:1-2

6:1 1Kor 3:9; 2Kor 5:20; 1Kor 15; 2Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure. 6:2 Isa 49; 8; Za 69:13; Isa 55:6Kwa maana asema:

“Wakati wangu uliokubalika nilikusikia,

siku ya wokovu nilikusaidia.”

Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.

Read More of 2 Wakorintho 6