Yuda 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yuda 1:1-25

Salamu

11:1 Yn 14:22; Mdo 1:13; Rum 1:6, 7; Yn 17:12Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo:

Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:

21:2 Rum 1:7; 2Pet 1:2Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.

Dhambi Na Hukumu Ya Watu Wasiomcha Mungu

31:3 Tit 1:4; 1Tim 6:12Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo. 41:4 Gal 2:4; 2Pet 2:1; 1Yn 2:22Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.

Hukumu Kwa Walimu Wa Uongo

51:5 Kum 1:32; 1Kor 10:1-5Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini. 61:6 2Pet 2:4, 9; Mwa 6:1; Yn 8:44; Ufu 20:10Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. 71:7 Kum 29:23; Mt 25:41; Mwa 19:24; 2Pet 2:6, 10; Mt 10:15Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele.

81:8 2Pet 2:10; Kut 22:28Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka. 91:9 Dan 12:1; Ufu 12:7; Zek 3:2Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!” 101:10 2Pet 2:12Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.

111:11 Mwa 4:3-8; 2Pet 2:15; Hes 16:1-3; 31:35Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.

121:12 2Pet 2:13; 1Kor 11:20-22; Mit 25:14; 2Pet 2:17; Efe 4:14; Mt 15:13Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa. 131:13 Isa 57:20; Flp 3:19; 2Pet 2:17Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele.

141:14 Mwa 5:18; 21:24; Kum 33:2; Dan 7:10Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake, 151:15 2Pet 2:6-9; 1Tim 1:9ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.” 161:16 2Pet 2:18; 2:10Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.

Maonyo Na Mausia

171:17 2Pet 3:2; Efe 4:11; Ebr 2:3Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani. 181:18 1Tim 4:1; 2Pet 2:4Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.” 191:19 1Kor 2:14, 15Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.

201:20 Kol 2:7; Efe 6:18Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu. 211:21 Tit 2:13; 2Pet 3:12; Ebr 9:28; Mt 25:46Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele.

22Wahurumieni walio na mashaka; 231:23 Amo 4:11; Zek 3:2-5; Ufu 3:4wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.

Dua Ya Kutakia Heri

241:24 Rum 16:25; 2Kor 4:14; Kol 1:22Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi: 251:25 Yn 5:44kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen.

King James Version

Jude 1:1-25

1Jude, the servant of Jesus Christ, and brother of James, to them that are sanctified by God the Father, and preserved in Jesus Christ, and called: 2Mercy unto you, and peace, and love, be multiplied.

3Beloved, when I gave all diligence to write unto you of the common salvation, it was needful for me to write unto you, and exhort you that ye should earnestly contend for the faith which was once delivered unto the saints. 4For there are certain men crept in unawares, who were before of old ordained to this condemnation, ungodly men, turning the grace of our God into lasciviousness, and denying the only Lord God, and our Lord Jesus Christ. 5I will therefore put you in remembrance, though ye once knew this, how that the Lord, having saved the people out of the land of Egypt, afterward destroyed them that believed not. 6And the angels which kept not their first estate, but left their own habitation, he hath reserved in everlasting chains under darkness unto the judgment of the great day. 7Even as Sodom and Gomorrha, and the cities about them in like manner, giving themselves over to fornication, and going after strange flesh, are set forth for an example, suffering the vengeance of eternal fire. 8Likewise also these filthy dreamers defile the flesh, despise dominion, and speak evil of dignities. 9Yet Michael the archangel, when contending with the devil he disputed about the body of Moses, durst not bring against him a railing accusation, but said, The Lord rebuke thee. 10But these speak evil of those things which they know not: but what they know naturally, as brute beasts, in those things they corrupt themselves. 11Woe unto them! for they have gone in the way of Cain, and ran greedily after the error of Balaam for reward, and perished in the gainsaying of Core. 12These are spots in your feasts of charity, when they feast with you, feeding themselves without fear: clouds they are without water, carried about of winds; trees whose fruit withereth, without fruit, twice dead, plucked up by the roots; 13Raging waves of the sea, foaming out their own shame; wandering stars, to whom is reserved the blackness of darkness for ever. 14And Enoch also, the seventh from Adam, prophesied of these, saying, Behold, the Lord cometh with ten thousands of his saints, 15To execute judgment upon all, and to convince all that are ungodly among them of all their ungodly deeds which they have ungodly committed, and of all their hard speeches which ungodly sinners have spoken against him. 16These are murmurers, complainers, walking after their own lusts; and their mouth speaketh great swelling words, having men’s persons in admiration because of advantage.

17But, beloved, remember ye the words which were spoken before of the apostles of our Lord Jesus Christ; 18How that they told you there should be mockers in the last time, who should walk after their own ungodly lusts. 19These be they who separate themselves, sensual, having not the Spirit. 20But ye, beloved, building up yourselves on your most holy faith, praying in the Holy Ghost, 21Keep yourselves in the love of God, looking for the mercy of our Lord Jesus Christ unto eternal life. 22And of some have compassion, making a difference: 23And others save with fear, pulling them out of the fire; hating even the garment spotted by the flesh.

24Now unto him that is able to keep you from falling, and to present you faultless before the presence of his glory with exceeding joy, 25To the only wise God our Saviour, be glory and majesty, dominion and power, both now and ever. Amen.