Ufunuo 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 1:1-20

Utangulizi Na Salamu

11:1 Ufu 22:16; Dan 2:28, 29; Yn 12:49; 17:8, 19; Ufu 22:6Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake, 21:2 1Kor 1:6; Ufu 6:9; Ebr 4:12; Ufu 12:17; 19:10ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo. 31:3 Lk 11:28; Ufu 22:7; Rum 13:11Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.

Salamu Kwa Makanisa Saba

41:4 Isa 11:2; Rum 1:7; Ufu 4:8; 11:17; 3:1; 4:5; 5:6Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia:

Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi, 51:5 Isa 55:4; Kol 1:18; Ufu 17:14na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia.

Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake, 61:6 1Pet 2:5; Rum 11:36akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen.

71:7 Dan 7:13; Zek 12:10Tazama! Anakuja na mawingu,

na kila jicho litamwona,

hata wale waliomchoma;

na makabila yote duniani

yataomboleza kwa sababu yake.

Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.

81:8 Ufu 22:6; 4:8; 21:6; 22:13; 15:3; Kut 3:14; Isa 41:4; Ufu 21:6“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”

Maono Ya Kristo

91:9 Mdo 14:22; 2Tim 2:12Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu. 101:10 Ufu 17:3; 3:1Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu 111:11 Ufu 2:8; 22:13; Mdo 18:19; Kol 2:1; Mdo 16:14ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

121:12 Zek 1:2; Ufu 3:1Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu, 131:13 Eze 1:26; Ufu 14:14; Dan 10:5; Ufu 15:6na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake. 141:14 Dan 7:9; Ufu 19:12Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto. 151:15 Eze 1:7; 43:2; Ufu 2:18; 19:6Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi. 161:16 Ufu 3:1; Isa 1:20; Ebr 4:12Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.

171:17 Eze 1:28; Dan 8:17, 18; Isa 48:12; Ufu 22:13Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho. 181:18 Rum 6:9; Kum 32:40; Ufu 9:1Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu.1:18 Kuzimu linalotokana na neno Hades la Kiyunani au Sheol kwa Kiebrania; maana yake ni mahali pa mateso kwa watu waliopotea.

191:19 Ufu 1:11; Hab 2:2“Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya. 201:20 Zek 4:2; Mt 5:14, 15Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.

King James Version

Revelation 1:1-20

1The Revelation of Jesus Christ, which God gave unto him, to shew unto his servants things which must shortly come to pass; and he sent and signified it by his angel unto his servant John: 2Who bare record of the word of God, and of the testimony of Jesus Christ, and of all things that he saw. 3Blessed is he that readeth, and they that hear the words of this prophecy, and keep those things which are written therein: for the time is at hand. 4John to the seven churches which are in Asia: Grace be unto you, and peace, from him which is, and which was, and which is to come; and from the seven Spirits which are before his throne; 5And from Jesus Christ, who is the faithful witness, and the first begotten of the dead, and the prince of the kings of the earth. Unto him that loved us, and washed us from our sins in his own blood, 6And hath made us kings and priests unto God and his Father; to him be glory and dominion for ever and ever. Amen. 7Behold, he cometh with clouds; and every eye shall see him, and they also which pierced him: and all kindreds of the earth shall wail because of him. Even so, Amen. 8I am Alpha and Omega, the beginning and the ending, saith the Lord, which is, and which was, and which is to come, the Almighty.

9I John, who also am your brother, and companion in tribulation, and in the kingdom and patience of Jesus Christ, was in the isle that is called Patmos, for the word of God, and for the testimony of Jesus Christ. 10I was in the Spirit on the Lord’s day, and heard behind me a great voice, as of a trumpet, 11Saying, I am Alpha and Omega, the first and the last: and, What thou seest, write in a book, and send it unto the seven churches which are in Asia; unto Ephesus, and unto Smyrna, and unto Pergamos, and unto Thyatira, and unto Sardis, and unto Philadelphia, and unto Laodicea. 12And I turned to see the voice that spake with me. And being turned, I saw seven golden candlesticks; 13And in the midst of the seven candlesticks one like unto the Son of man, clothed with a garment down to the foot, and girt about the paps with a golden girdle. 14His head and his hairs were white like wool, as white as snow; and his eyes were as a flame of fire; 15And his feet like unto fine brass, as if they burned in a furnace; and his voice as the sound of many waters. 16And he had in his right hand seven stars: and out of his mouth went a sharp twoedged sword: and his countenance was as the sun shineth in his strength. 17And when I saw him, I fell at his feet as dead. And he laid his right hand upon me, saying unto me, Fear not; I am the first and the last: 18I am he that liveth, and was dead; and, behold, I am alive for evermore, Amen; and have the keys of hell and of death.

19Write the things which thou hast seen, and the things which are, and the things which shall be hereafter; 20The mystery of the seven stars which thou sawest in my right hand, and the seven golden candlesticks. The seven stars are the angels of the seven churches: and the seven candlesticks which thou sawest are the seven churches.