3 Yohana 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

3 Yohana 1:1-15

Salamu

11:1 Mdo 11:30; 2Yn 1Mzee:

Kwa Gayo rafiki yangu, nimpendaye katika kweli.

Gayo Anasifiwa Kwa Ajili Ya Ukarimu Wake

21:2 2Yn 4Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo. 31:3 Mdo 1:16; 2Yn 4Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza juu ya uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli. 41:4 1Kor 4:14; 1Yn 1:2Sina furaha kubwa kuliko hii, kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.

51:5 Rum 12:13Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako. 61:6 1Kor 16:11; 2Kor 1:16; Efe 4:1Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya kanisa. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu. 71:7 Yn 15:21; Mdo 20:33, 35Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini. 81:8 Ebr 13:2; 2Yn 10Kwa hiyo imetupasa sisi kuonyesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.

Deotrefe

9Nililiandikia kanisa, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu. 101:10 3Yn 14; 2Yn 5; Yn 9:22, 34Hivyo kama nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke kanisani.

Demetrio

111:11 Za 34:14; 37:27; 1Yn 2:29; 3:6, 9, 10Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema atoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.

121:12 Yn 19:39; 21:24Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.

Salamu Za Mwisho

131:13 2Yn 12Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino. 141:14 2Yn 12; Rum 1:7; Efe 6:23; Yn 10:3Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana.

15Amani iwe kwako. Rafiki zetu walioko hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walioko huko, kila mmoja kwa jina lake.

King James Version

3 John 1:1-14

1The elder unto the wellbeloved Gaius, whom I love in the truth.

2Beloved, I wish above all things that thou mayest prosper and be in health, even as thy soul prospereth. 3For I rejoiced greatly, when the brethren came and testified of the truth that is in thee, even as thou walkest in the truth. 4I have no greater joy than to hear that my children walk in truth. 5Beloved, thou doest faithfully whatsoever thou doest to the brethren, and to strangers; 6Which have borne witness of thy charity before the church: whom if thou bring forward on their journey after a godly sort, thou shalt do well: 7Because that for his name’s sake they went forth, taking nothing of the Gentiles. 8We therefore ought to receive such, that we might be fellowhelpers to the truth.

9I wrote unto the church: but Diotrephes, who loveth to have the preeminence among them, receiveth us not. 10Wherefore, if I come, I will remember his deeds which he doeth, prating against us with malicious words: and not content therewith, neither doth he himself receive the brethren, and forbiddeth them that would, and casteth them out of the church.

11Beloved, follow not that which is evil, but that which is good. He that doeth good is of God: but he that doeth evil hath not seen God. 12Demetrius hath good report of all men, and of the truth itself: yea, and we also bear record; and ye know that our record is true.

13I had many things to write, but I will not with ink and pen write unto thee: 14But I trust I shall shortly see thee, and we shall speak face to face. Peace be to thee. Our friends salute thee. Greet the friends by name.