Yeremia 33 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 33:1-26

Ahadi Ya Kurudishwa

133:1 Yer 32:2; 37:21; 38:28; Za 88:8; Yer 13:3Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema: 233:2 Yer 10:16; Za 136:6; Kut 3:15; 15:3“Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake: 333:3 Mwa 18:17; Yer 29:12; Isa 55:6; Ay 28:11‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’ 433:4 2Fal 25:1; Eze 4:2; 26:8; Hab 1:10; Yer 32:24Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga 533:5 Yer 21:4-7; Kum 31:17; Isa 8:17katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.

633:6 Kum 32:39; Isa 30:26; 9:6“ ‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama. 733:7 Yer 32:44; Eze 39:25; Amo 9:14; Isa 1:26; Yer 24:6; 30:3Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali. 833:8 Law 16:30; Ebr 9:13-14; 2Sam 24:14; Mik 7:18; Yer 31:34Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu. 933:9 Isa 60:18; Yer 13:11; Isa 64:2; Yer 3:17; 1Yn 1:7-9; Isa 55:13Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’

1033:10 Yer 32:43; 9:11“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine 1133:11 Za 51:8; 24:8; Law 7:12; 2Nya 5:13; Za 25:8; 100:4-5; 14:7sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema,

“ ‘ “Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote,

kwa maana Bwana ni mwema;

upendo wake wadumu milele.”

Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.

1233:12 Yer 32:43; Isa 65:10; Eze 34:11-15“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo. 1333:13 Yer 32:43; Isa 65:10; Eze 34:11-15Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.

1433:14 Kum 28:1-14; Yos 23:15; Yer 29:10“ ‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.

1533:15 Isa 4:2; Za 72:2; Isa 11:1; 2Sam 7:12“ ‘Katika siku hizo na wakati huo

nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi,

naye atafanya lile lililo haki na sawa

katika nchi.

1633:16 Isa 45:17; 1Kor 1:30; Zek 8:3, 16; Sef 3:13; Eze 48:35; Yer 3:17; Isa 59:14; Yer 32:37Katika siku hizo, Yuda ataokolewa

na Yerusalemu ataishi salama.

Hili ndilo jina atakaloitwa:

Bwana Haki Yetu.’

1733:17 2Sam 7:13; 2Nya 7:18; Za 89:29-37Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli, 1833:18 Kum 18:1; Ebr 13:15; Hes 25:11-13; Ebr 7:17-22wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’ ”

19Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2033:20 Za 89:36; Mwa 8:22; Isa 54:9; Mwa 1:14“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake, 2133:21 Za 89:34; 2Sam 7:13-18; 2Nya 7:18basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi. 2233:22 Mwa 15:5; Hos 1:10; Mwa 13:16; Yer 30:19; Mwa 12:2Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’ ”

23Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2433:24 Eze 37:22; Neh 4:4; Yer 30:17; Eze 36:20“Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa. 2533:25 Mwa 1:18; Yer 31:35-36; Za 74:16-17; 148:6Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi, 2633:26 Law 26:44; Yer 31:37; Isa 14:1; Zek 10:6; Za 14:7; Yer 30:18basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’ ”

New International Reader’s Version

Jeremiah 33:1-26

The Lord Promises to Heal His People

1Jeremiah was still being held as a prisoner. He was kept in the courtyard of the guard. Then another message from the Lord came to him. The Lord said, 2“I made the earth. I formed it. And I set it in place. The Lord is my name. 3Call out to me. I will answer you. I will tell you great things you do not know. And unless I do, you wouldn’t be able to find out about them.” 4The Lord is the God of Israel. He speaks about the houses in Jerusalem. He talks about the royal palaces of Judah. The people had torn down many of them. They had used their stones to strengthen the city walls against attack. 5That was during their fight with the armies of Babylon. The Lord says, “The houses will be filled with dead bodies. They will be the bodies of the people I will kill. I will kill them when I am very angry with them. I will hide my face from this city. That’s because its people have committed so many sins.

6“But now I will bring health and healing to Jerusalem. I will heal my people. I will let them enjoy great peace and security. 7I will bring Judah and Israel back from the places where they have been taken. I will build up the nation again. It will be just as it was before. 8I will wash from its people all the sins they have committed against me. And I will forgive all the sins they committed when they turned away from me. 9Then this city will bring me fame, joy, praise and honor. All the nations on earth will hear about the good things I do for this city. They will see the great success and peace I give it. Then they will be filled with wonder. And they will tremble with fear.”

10The Lord says, “You say about this place, ‘It’s a dry and empty desert. It doesn’t have any people or animals in it.’ The towns of Judah and the streets of Jerusalem are now deserted. So they do not have any people or animals living in them. But happy sounds will be heard there once more. 11They will be the sounds of joy and gladness. The voices of brides and grooms will fill the streets. And the voices of those who bring thank offerings to my house will be heard there. They will say,

“ ‘Give thanks to the Lord who rules over all,

because he is good.

His faithful love continues forever.’

That’s because I will bless this land with great success again. It will be as it was before,” says the Lord.

12The Lord who rules over all says, “This place is a desert. It does not have any people or animals in it. But there will again be grasslands near all its towns. Shepherds will rest their flocks there. 13Flocks will again pass under the hands of shepherds as they count their sheep,” says the Lord. “That will be done in the towns of the central hill country. It will be done in the western hills and the Negev Desert. It will be done in the territory of Benjamin. And it will be done in the villages around Jerusalem and in the towns of Judah.

14“The days are coming,” announces the Lord. “At that time I will fulfill my good promise to my people. I made it to the people of Israel and Judah.

15“Here is what I will do in those days and at that time.

I will make a godly Branch grow from David’s royal line.

He will do what is fair and right in the land.

16In those days Judah will be saved.

Jerusalem will live in safety.

And it will be called

The Lord Who Makes Us Right With Himself.”

17The Lord says, “David will always have a son to sit on the throne of Israel. 18The priests, who are Levites, will always have a man to serve me. He will sacrifice burnt offerings. He will burn grain offerings. And he will offer sacrifices.”

19A message from the Lord came to Jeremiah. 20The Lord said, “Could you ever break my covenant with the day? Could you ever break my covenant with the night? Could you ever stop day and night from coming at their appointed times? 21Only then could my covenant with my servant David be broken. Only then could my covenant with the Levites who serve me as priests be broken. Only then would David no longer have someone from his family line to rule on his throne. 22Here is what I will do for my servant David. And here is what I will do for the Levites who serve me. I will make their children after them as many as the stars in the sky. And I will make them as many as the grains of sand on the seashore. It will be impossible to count them.”

23A message from the Lord came to Jeremiah. The Lord said, 24“Haven’t you noticed what these people are saying? They say, ‘The Lord once chose the two kingdoms of Israel and Judah. But now he has turned his back on them.’ So they hate my people. They do not think of them as a nation anymore. 25I say, ‘What if I had not made my covenant with day and night? What if I had not established the laws of heaven and earth? 26Only then would I turn my back on the children of Jacob and my servant David. Only then would I not choose one of David’s sons to rule over the children of Abraham, Isaac and Jacob. But I will bless my people with great success again. I will love them with tender love.’ ”