Yeremia 32 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 32:1-44

Yeremia Anunua Shamba

132:1 2Fal 25:1; Yer 25:1; 39:1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza. 232:2 Neh 3:25; Yer 37:21; Mt 5:12; Za 88:8Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.

332:3 Yer 26:8-9; 21; 4; 34:2-4Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka. 432:4 Yer 21:7; 52:9; 44:30; 34:21; 38:18, 23; 39:5-7Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe. 532:5 Yer 39:7; Eze 12:13; Mao 1:14; Mit 21:30; Yer 21:4; 2Fal 25:7Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’ ”

6Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema: 732:7 Law 25:24-32; Rut 4:3-4; Mt 27:10; Yos 21:18Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’

8“Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’

“Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana. 932:9 Mwa 23:16; Yer 37:12Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba32:9 Shekeli 17 za fedha ni sawa na gramu 200. za fedha. 1032:10 Rut 4:9; Isa 8:2; Mwa 23:20Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani. 11Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri, 1232:12 Yer 36:4; 43:3-6; 51:59nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.

13“Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao: 1432:14 Isa 8:16‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu. 1532:15 Eze 28:26; Amo 9:14-15; Yer 30:18; Isa 44:26Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’

16“Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:

1732:17 Kum 9:29; Kut 20:5; Za 102:25; 2Fal 3:18; Mwa 32:9-12; Mt 19:26; 2Fal 19:15“Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza. 1832:18 Kum 5:9-10; Eze 20:5; Kut 20:6; Za 109:14; Yer 10:16; Za 79:12Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, 1932:19 Isa 28:29; Ay 34:11, 21; Mit 5:21; Dan 2:20; Mt 16:27; Ay 12:13; 14:16makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake. 2032:20 Kut 9:16; Isa 63:12; Kut 3:20; Ay 9:10; Isa 55:13; Yer 13:11Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo. 2132:21 1Nya 17:21; Kut 6:6; Kum 26:8; 2Sam 7:23; Dan 9:15; Yer 6:12; Kum 5:15Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu. 2232:22 Kut 3:8; Eze 20:6Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali. 2332:23 Za 78:54-55; Neh 9:26; Dan 9:10-14; Kum 28:64; Za 44:2; Kut 16:28; Yer 11:8Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.

2432:24 Yer 14:12; Yos 23:15; Kum 4:25-26; 2Sam 20:15; Yer 6:6; Kum 28:2“Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa. 25Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’ ”

26Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2732:27 Hes 16:22; Mwa 18:14; 2Fal 3:18“Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza? 2832:28 2Nya 36:17; Yer 21:10Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka. 2932:29 Yer 19:13; 52:13; 44:18; 7:9Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.

3032:30 Za 25:7; Yer 22:21; 8:19; 25:7“Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana. 3132:31 2Fal 23:27; 24:3; Sef 3:1; Mt 23:37; 2Fal 21:4-5; 1Fal 11:7-8Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu. 3232:32 Isa 1:4-6; Dan 9:8; 1Fal 14:9; Yer 2:26; 44:9Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu. 3332:33 1Fal 14:9; Za 14:3; Kum 4:5; Isa 28:9; Yer 7:13, 28; 2:27; Eze 8:16; Zek 7:11Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu. 3432:34 Yer 7:30; Eze 8:3-16Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi. 3532:35 Law 18:21; Yer 7:31; 2Fal 23:10; Yer 19:5; 25:7Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.

36“Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo: 3732:37 Isa 11:12; Yer 23:3-6; Law 25:18; Kum 30:3; Eze 34:28; 39:26; Yer 21:5Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama. 3832:38 Yer 24:7; 2Kor 6:16Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. 3932:39 Eze 11:19; Yn 17:21; 2Nya 30:12; Mdo 4:32; Kum 6:24; 10:16; Za 86:11Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao. 4032:40 Mwa 9:16; Isa 55:3; Yer 24; 7; Isa 42:6; Kum 4:10Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami. 4132:41 Kum 28:3-12; Yer 24:6; Kum 30; 9; Amo 9:15; Yer 31:28; Isa 62:4; Mik 7:18Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.

4232:42 Yer 29:10; 31:28; Mao 3:38“Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi. 43Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’ 4432:44 Yer 17:26; Ezr 9:9; Yer 33:7, 11, 26; Rut 4:9; Isa 8:2; Za 14:7Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao,32:44 Au: nitawarudisha tena kutoka utumwani. asema Bwana.”

New International Reader’s Version

Jeremiah 32:1-44

Jeremiah Buys a Field

1A message from the Lord came to Jeremiah. It came in the 10th year that Zedekiah was king of Judah. It was in the 18th year of the rule of Nebuchadnezzar. 2The armies of the king of Babylon were getting ready to attack Jerusalem. Jeremiah the prophet was being held as a prisoner. He was kept in the courtyard of the guard. It was part of Judah’s royal palace.

3Zedekiah, the king of Judah, had made Jeremiah a prisoner there. Zedekiah had said to him, “Why do you prophesy as you do? You say, ‘The Lord says, “I am about to hand over this city to the king of Babylon. He will capture it. 4Zedekiah, the king of Judah, will not escape from the powerful hands of the armies of Babylon. He will certainly be handed over to the king of Babylon. Zedekiah will speak with him face to face. He will see him with his own eyes. 5Nebuchadnezzar will take Zedekiah to Babylon. Zedekiah will remain there until I deal with him,” announces the Lord. “Suppose you fight against the armies of Babylon. If you do, you will not succeed.” ’ ”

6Jeremiah said, “A message from the Lord came to me. The Lord said, 7‘Hanamel is going to come to you. He is the son of your uncle Shallum. Hanamel will say, “Buy my field at Anathoth. You are my closest relative. So it’s your right and duty to buy it.” ’

8“Then my cousin Hanamel came to me. I was in the courtyard of the guard. It happened just as the Lord had said it would. Hanamel said, ‘Buy my field at Anathoth. It is in the territory of Benjamin. It is your right to buy it and own it. So buy it for yourself.’

“I knew that this was the Lord’s message. 9So I bought the field at Anathoth from my cousin Hanamel. I weighed out seven ounces of silver for him. 10I signed and sealed the deed of purchase. I had some people witness everything. And I weighed out the silver on the scales. 11There were two copies of the deed. One was sealed and the other wasn’t. The deed included the terms and conditions of the sale. 12I gave Baruch the copies of the deed. My cousin Hanamel saw me do this. The witnesses who had signed the deed were there too. So were all the Jews who were sitting in the courtyard of the guard. Baruch was the son of Neriah. Neriah was the son of Mahseiah.

13“I gave Baruch directions in front of all of them. I said, 14‘The Lord who rules over all is the God of Israel. He says, “Take this deed of purchase. Take the sealed and unsealed copies. Put them in a clay jar. Then they will last a long time.” 15The Lord who rules over all is the God of Israel. He says, “Houses, fields and vineyards will again be bought in this land.” ’

16“I gave the deed of purchase to Baruch, the son of Neriah. Then I prayed to the Lord. I said,

17“ ‘Lord and King, you have reached out your great and powerful arm. You have made the heavens and the earth. Nothing is too hard for you. 18You show your love to thousands of people. But you cause the sins of parents to affect even their children. Great and powerful God, your name is the Lord Who Rules Over All. 19Your purposes are great. Your acts are mighty. Your eyes see everything people do. You reward each one of them in keeping with their conduct. You do this based on what they have done. 20You performed signs and wonders in Egypt. And you have continued to do them to this day. You have done them in Israel and among all people. You are still known for doing them. 21You brought your people Israel out of Egypt. You did it with signs and wonders. You reached out your mighty hand and powerful arm. You did great and wonderful things. 22You gave Israel this land that you promised to their people of long ago. It is a land that has plenty of milk and honey. 23Israel came in and took it over. But they did not obey you. They didn’t follow your law. They didn’t do what you commanded them to do. So you brought all this trouble on them.

24“ ‘See how ramps are built up against Jerusalem’s walls to attack it. The city will be handed over to the armies of Babylon. They are attacking it. It will fall because of war, hunger and plague. What you said would happen is now happening, as you can see. 25Lord and King, the city will be handed over to the armies of Babylon. In spite of that, you tell me to buy a field. You say, “Pay for it with silver. And have the sale witnessed.” ’ ”

26Then a message from the Lord came to Jeremiah. The Lord said, 27“I am the Lord. I am the God of all people. Is anything too hard for me?” 28So the Lord says, “I am about to hand this city over to the armies of Babylon. I will give it to Nebuchadnezzar, the king of Babylon. He will capture it. 29The armies of Babylon are now attacking this city. They will come in and set it on fire. They will burn it down. They will burn down the houses where the people made me very angry. They burned incense on their roofs to the god named Baal. And they poured out drink offerings to other gods.

30“The people of Israel and Judah have done nothing but evil in my eyes. They have done it since the nation was young. In fact, they have done nothing but make me very angry. They have worshiped statues of gods their own hands have made,” announces the Lord. 31“This city has always stirred up my great anger. It has done it since the day it was built. Now I must remove it from my sight. 32The people of Israel and Judah have made me very angry. They have done many evil things. They, their kings and officials have sinned. So have their priests and prophets. And the people of Judah and Jerusalem have also sinned. 33They turned their backs to me. They would not face me. I taught them again and again. But they would not listen or pay attention when they were corrected. 34They set up the hateful statues of their gods. They did it in the house where I have put my Name. They made my house ‘unclean.’ 35The people built high places for Baal in the Valley of Ben Hinnom. That is where they sacrifice their children to Molek in the fire. That is something I did not command. It did not even enter my mind. They did something I hate. They made Judah sin.”

36Here is what you people of Judah are saying about this city. “By war, hunger and plague it will be handed over to the king of Babylon.” But here is what the Lord, the God of Israel, says. 37“You can be sure that I will gather my people again. I will send them away when my burning anger blazes out against them. But I will bring them back to this place. And I will let them live in safety. 38They will be my people. And I will be their God. 39I will give them a single purpose in life. Then, they will always have respect for me. Then all will go well for them. And it will also go well for their children after them. 40I will make a covenant with them that will last forever. I promise that I will never stop doing good to them. I will cause them to respect me. Then they will never turn away from me again. 41I will take pleasure in doing good things for them. I will certainly plant them in this land. I will do these things with all my heart and soul.”

42The Lord says, “I have brought all this horrible trouble on these people. But now I will give them all the good things I have promised them. 43Once more fields will be bought in this land. It is the land about which you now say, ‘It is a dry and empty desert. It doesn’t have any people or animals in it. It has been handed over to the armies of Babylon.’ 44Fields will be bought with silver. Deeds will be signed, sealed and witnessed. That will be done in the territory of Benjamin. It will be done in the villages around Jerusalem and in the towns of Judah. It will also be done in the towns of the central hill country. And it will be done in the towns of the western hills and the Negev Desert. I will bless their people with great success again,” announces the Lord.