Ufunuo 21 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 21:1-27

Mbingu Mpya Na Nchi Mpya

121:1 Isa 65:17; 2Pet 3:13Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena. 221:2 Ebr 11:10; 12:22Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe. 321:3 2Kor 6:16; Zek 2:10; Isa 8:8Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 421:4 Ufu 7:17; 1Kor 15:26; Isa 35:10; 65:19Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”

521:5 Ufu 4:9; 20:11; 19:9Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”

621:6 Ufu 16:17; 1:8; 22:13; Yn 4:10Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote. 721:7 Ufu 2:7; 2Sam 7:14Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. 821:8 Za 5:6; Ufu 2:11Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”

921:9 Ufu 15:1, 6, 7; 19:7Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.” 1021:10 Ufu 17:3; 1:10; Eze 40:2; Ufu 21:2Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu. 1121:11 Ufu 15:8; 4:6; Isa 60:1, 2; Eze 43:2; Ufu 21:23; 21:18, 19Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo. 1221:12 Eze 48:30-34Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli. 1321:13 Eze 48:31, 34Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi. 1421:14 Efe 2:20; Ebr 11:10; Mdo 1:2621:14 Ufu 11:1; Eze 40:3; Ufu 21:12Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake. 1621:16 Eze 45:16; 48:16; 17Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200;21:16 Kilomita 2,200 hapa ni sawa na maili 1,200. urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa. 1721:17 Ufu 13:18Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 14421:17 Dhiraa 144 ni karibu mita 65. kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia. 1821:18 Ufu 21:11, 21Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo. 1921:19 Kut 28:17-20Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi, 2021:20 Ufu 4:3wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto. 2121:21 Ufu 21:12; Isa 54:12; Ufu 21:18Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.

2221:22 Yn 4:21-23; Ufu 1:8; 5:6Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake. 2321:23 Isa 24:23; 22:5Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. 2421:24 Isa 60:3, 5Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake. 2521:25 Isa 60:11; Zek 14:7; Ufu 22:5Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo. 2621:26 Ufu 21:24Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo. 2721:27 Yoe 3:17; Ufu 22:14, 15Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.

La Bible du Semeur

Apocalypse 21:1-27

Septième vision : le nouveau ciel et la nouvelle terre

1Puis je vis un ciel nouveau et une terre nouvelle21.1 Voir Es 65.17 ; 66.22., car le premier ciel et la première terre avaient disparu, et la mer n’existait plus.

2Je vis la ville sainte, la nouvelle Jérusalem, descendre du ciel, d’auprès de Dieu, belle comme une mariée qui s’est parée pour son époux. 3Et j’entendis une forte voix, venant du trône, qui disait :

Voici la Tente de Dieu avec les hommes. Il habitera avec eux ; ils seront ses peuples et lui, Dieu avec eux21.3 Voir Ex 6.7 ; Lv 26.12., sera leur Dieu. 4Il essuiera toute larme de leurs yeux. La mort ne sera plus et il n’y aura plus ni deuil, ni plainte, ni souffrance. Car ce qui était autrefois a définitivement disparu21.4 Ex 6.7 ; 25.8 ; 29.45 ; Lv 26.12 ; Ez 37.27..

5Alors celui qui siège sur le trône déclara : Voici : je renouvelle toutes choses.

Il ajouta : Ecris que ces paroles sont vraies et entièrement dignes de confiance.

6Puis il me dit : C’en est fait ! Je suis l’Alpha et l’Oméga21.6 Voir note 1.8., le commencement et la fin. A celui qui a soif, je donnerai, moi, à boire gratuitement à la source d’où coule l’eau de la vie.

7Tel sera l’héritage du vainqueur. Je serai son Dieu et il sera mon fils. 8Quant aux lâches, aux infidèles, aux dépravés, meurtriers et débauchés, aux magiciens, aux idolâtres et à tous les menteurs, leur part sera l’étang ardent de feu et de soufre, c’est-à-dire la seconde mort.

La nouvelle Jérusalem, Épouse de l’Agneau 21.9 La description de la nouvelle Jérusalem rappelle la vision de la Jérusalem restaurée d’Ez 40 à 48 et d’Es 60.

9Alors l’un des sept anges qui tenaient les sept coupes pleines des sept derniers fléaux vint me parler : Viens, me dit-il, je te montrerai la Mariée, l’Epouse de l’Agneau.

10Il me transporta en esprit sur une grande et haute montagne, d’où il me fit voir la ville sainte, Jérusalem, qui descendait du ciel, d’auprès de Dieu. 11Elle rayonnait de la gloire divine. Son éclat rappelait celui d’une pierre très précieuse, celui d’un jaspe d’une transparence cristalline. 12Elle était entourée d’une grande et haute muraille, percée de douze portes gardées par douze anges, et sur ces portes étaient gravés les noms des douze tribus d’Israël. 13Les portes étaient orientées trois vers l’est, trois vers le nord, trois vers le sud et trois vers l’ouest. 14La muraille reposait sur douze fondements qui portaient les noms des douze apôtres de l’Agneau.

15Mon interlocuteur tenait, en guise de mesure, un roseau d’or pour mesurer la ville, ses portes et sa muraille. 16La ville était bâtie en carré, sa longueur égalait sa largeur. L’ange mesura donc la ville avec son roseau et trouva douze mille stades, sa longueur, sa largeur et sa hauteur étant d’égale dimension21.16 Les mesures de ce chapitre ne sont pas converties en mètres ou en kilomètres pour conserver le symbolisme des nombres bibliques.. 17Il mesura aussi la muraille et trouva cent quarante-quatre coudées, d’après la mesure humaine employée par l’ange.

18La muraille était construite en jaspe, la ville elle-même était d’or pur, transparent comme du cristal pur. 19Les fondements de la muraille de la ville étaient ornés de toutes sortes de pierres précieuses, le premier de jaspe, le second de saphir, le troisième de chalcédoine, le quatrième d’émeraude, 20le cinquième de sardoine, le sixième de cornaline, le septième de chrysolithe, le huitième de béryl, le neuvième de topaze, le dixième de chrysoprase, le onzième de turquoise, le douzième d’améthyste. 21Les douze portes étaient douze perles ; chaque porte était faite d’une seule perle. L’avenue principale de la ville était d’or pur, transparent comme du cristal.

22Je ne vis aucun temple dans la ville : son temple, c’est le Seigneur, le Dieu tout-puissant, ainsi que l’Agneau. 23La ville n’a besoin ni du soleil, ni de la lune pour l’éclairer, car la gloire de Dieu l’illumine et l’Agneau lui tient lieu de lampe. 24Les peuples marcheront à sa lumière et les rois de la terre viendront lui apporter leur gloire. 25Tout au long du jour, les portes de la ville resteront ouvertes, car il n’y aura plus de nuit. 26On y apportera tout ce qui fait la gloire et l’honneur des peuples. 27Rien d’impur ne pourra y pénétrer. Nul homme qui se livre à des pratiques abominables et au mensonge n’y entrera. Seuls y auront accès ceux qui sont inscrits dans le livre de vie de l’Agneau.