Ufunuo 22 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 22:1-21

Mto Wa Maji Ya Uzima

122:1 Ufu 4:6; Eze 47:1; Zek 14:8Kisha yule malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima, maangavu kama kioo yakitiririka kutoka kwenye kile kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo, 222:2 Ufu 2:7; Eze 47:12kupitia katikati ya barabara kuu ya huo mji. Kwenye kila upande wa huo mto kulikuwa na mti wa uzima utoao matunda ya aina kumi na mbili, ukizaa matunda yake kila mwezi. Nayo majani ya mti huo ni kwa ajili ya uponyaji wa mataifa. 322:3 Zek 14:11; Ufu 7:15Katika mji huo hakutakuwa tena na laana, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo humo na watumishi wake watamtumikia, 422:4 Mt 5:8; Ufu 14:1nao watamwona uso wake na Jina lake litakuwa kwenye vipaji vya nyuso zao. 522:5 Ufu 21:23, 25; 20:4; Dan 7:27Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, kwa maana Bwana Mungu atakuwa nuru yao, nao watatawala milele na milele.

622:6 Ufu 1:1; 19:9; 21:5; Ebr 12:9Kisha yule malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kuaminika na kweli. Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumishi wake yale ambayo hayana budi kutukia upesi.”

Bwana Yesu Anakuja

722:7 Ufu 3:11; 1:3; Mt 16:27; Ufu 22:10, 18, 19“Tazama, naja upesi! Amebarikiwa yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.”

822:8 Ufu 1:1; 19:10Mimi, Yohana, ndiye niliyesikia na kuyaona mambo haya. Nami nilipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka chini nikasujudu miguuni pa yule malaika aliyekuwa akinionyesha mambo hayo. 922:9 Ufu 19:10; 22:10, 18, 19Lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi ni mtumishi pamoja nawe na ndugu zako manabii na wote wanaoyashika maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu!”

1022:10 Dan 8:26; Ufu 10:4; 1:3Kisha akaniambia, “Usiyafunge maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, kwa sababu wakati umekaribia. 1122:11 Eze 3:27; Dan 12:10Atendaye mabaya na aendelee kutenda mabaya, aliye mchafu na aendelee kuwa mchafu, yeye atendaye haki na aendelee kutenda haki, na yeye aliye mtakatifu na aendelee kuwa mtakatifu.”

1222:12 Isa 14:10; Mt 16:27; Isa 62:11“Tazama, naja upesi! Thawabu yangu i mkononi mwangu, nami nitampa kila mtu sawasawa na alivyotenda. 1322:13 Ufu 1:8, 17; 21:6Mimi ni Alfa na Omega, wa Kwanza na wa Mwisho, Mwanzo na Mwisho.

1422:14 Ufu 2:7; 21:12, 27“Wamebarikiwa wale wafuao mavazi yao, ili wapate haki ya kuuendea huo mti wa uzima na kuuingia huo mji kupitia kwenye malango yake. 1522:15 Kum 23:18; Kol 3:5, 6; Flp 3:2Huko nje wako mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu, na kila mtu apendaye udanganyifu na kuufanya.

1622:16 Ufu 1:1, 4; 5:5; 2Pet 1:19; Ufu 2:28“Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu kushuhudia mambo haya kwa ajili ya makanisa. Mimi ndimi Shina na Mzao wa Daudi, ile Nyota ya Asubuhi ingʼaayo.”

1722:17 Ufu 14:13Roho na bibi arusi wanasema, “Njoo!” Naye asikiaye na aseme, “Njoo!” Yeyote mwenye kiu na aje, na kila anayetaka na anywe maji ya uzima bure.

1822:18 Kum 12:32; Mit 30:6; Ufu 5:6; 16:21Namwonya kila mtu asikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki: Mtu yeyote akiongeza humo chochote, Mungu atamwongezea mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. 1922:19 Kum 4:2Kama mtu yeyote akipunguza humo chochote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.

2022:20 Ufu 1:2; 1Kor 16:22Yeye anayeshuhudia mambo haya asema, “Hakika, naja upesi!”

Amen. Njoo, Bwana Yesu.

2122:21 Rum 16:20Neema ya Bwana Yesu iwe na watakatifu wote. Amen.

La Bible du Semeur

Apocalypse 22:1-21

1Finalement, l’ange me montra le fleuve d’eau de la vie, limpide comme du cristal, qui jaillissait du trône de Dieu et de l’Agneau.

2Au milieu de l’avenue de la ville, entre deux bras du fleuve, se trouve l’arbre de vie. Il produit douze récoltes, chaque mois il porte son fruit. Ses feuilles servent à guérir les peuples.

3Il n’y aura plus aucune malédiction. Le trône de Dieu et de l’Agneau sera dans la ville. Ses serviteurs lui rendront un culte : 4ils verront sa face et porteront son nom sur leurs fronts. 5Il n’y aura plus jamais de nuit. On n’aura donc plus besoin ni de la lumière d’une lampe, ni de celle du soleil, car le Seigneur Dieu répandra sur eux sa lumière. Et ils régneront éternellement.

Conclusion

6L’ange me dit : Ces paroles sont vraies et entièrement dignes de foi. Dieu le Seigneur qui a inspiré ses prophètes, a envoyé son ange, pour montrer à ses serviteurs ce qui doit arriver bientôt.

7– Voici, dit Jésus, je viens bientôt ! Heureux celui qui obéit aux paroles prophétiques de ce livre.

8Moi, Jean, j’ai entendu et vu tout cela. Après avoir entendu et vu ces choses, je me prosternai aux pieds de l’ange qui me les avait montrées, et j’allais l’adorer.

9– Non, me dit-il, ne fais pas cela ! Je suis ton compagnon de service et celui de tes frères, les prophètes, et de ceux qui obéissent aux paroles de ce livre. Adore Dieu !

10Et il ajouta : Ne tiens pas secrètes les paroles prophétiques de ce livre, car le temps de leur accomplissement est proche. 11Que celui qui commet le mal continue à mal agir. Que celui qui est impur continue à s’adonner à l’impureté ; mais que celui qui est juste continue à faire ce qui est juste, et que celui qui est saint continue à se purifier.

12– Oui, dit Jésus, je viens bientôt. J’apporte avec moi mes récompenses pour rendre à chacun selon ses actes. 13Je suis l’Alpha et l’Oméga, le premier et le dernier, le commencement et la fin. 14Heureux ceux qui lavent leurs vêtements. Ils auront le droit de manger du fruit de l’arbre de vie et de franchir les portes de la ville. 15Mais dehors les hommes ignobles, ceux qui pratiquent la magie, les débauchés, les meurtriers, ceux qui adorent des idoles et tous ceux qui aiment et pratiquent le mensonge.

16Moi, Jésus, j’ai envoyé mon ange pour rendre témoignage à ces vérités destinées aux Eglises. Je suis le rejeton de la racine de David, son descendant. C’est moi, l’étoile brillante du matin.

17Et l’Esprit et l’Epouse disent : Viens ! Que celui qui entend ces paroles dise : Viens ! Que celui qui a soif vienne. Que celui qui veut de l’eau de la vie la reçoive gratuitement.

18Moi, je le déclare solennellement à tous ceux qui entendent les paroles prophétiques de ce livre : si quelqu’un y ajoute quoi que ce soit, Dieu ajoutera à son sort les fléaux décrits dans ce livre. 19Si quelqu’un retranche quelque chose des paroles prophétiques de ce livre, Dieu lui ôtera tout droit à l’arbre de vie et à la ville sainte décrits dans ce livre.

20Le témoin qui affirme ces choses déclare : Oui, je viens bientôt !

Oh oui, qu’il en soit ainsi : Viens Seigneur Jésus22.20 Voir l’acclamation araméenne : Marana tha (Notre Seigneur, viens) utilisée dans les cultes de l’Eglise primitive (1 Co 16.22). !

21Que le Seigneur Jésus accorde sa grâce à tous.