Mwanzo 26 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 26:1-35

Isaki Na Abimeleki

126:1 Mwa 12:10; 20:1Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari. 226:2 Mwa 12:1, 7; 46:3Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia. 326:3 Kut 3:12; Mwa 12:2, 7Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako. 426:4 Mwa 26:24; 48:4; 12:2Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa, 526:5 Mwa 18:19; Za 119:80, 112; Eze 18:21kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.” 626:6 Mwa 20:1Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.

726:7 Mwa 12:13Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”

8Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake. 9Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’ ”

Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”

1026:10 Mwa 12:8Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”

1126:11 1Sam 24:6; 26:9; Za 105:15Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”

1226:12 Mt 13:8; Mwa 26:3Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki. 1326:13 Mwa 13:2; Kum 8:18Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana. 1426:14 Mwa 12:16; 24:36Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu. 1526:15 Mwa 21:30; 21:25Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.

16Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”

17Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko. 18Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.

19Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi. 20Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki,26:20 Eseki maana yake ni Ugomvi. kwa sababu waligombana naye. 21Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.26:21 Sitna maana yake Upinzani. 2226:22 Kut 18:19; Mwa 17:6Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi,26:22 Rehobothi maana yake ni Mungu ametufanyia nafasi. akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”

23Kutoka pale akaenda Beer-Sheba. 2426:24 Mwa 24:12; 17:7Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”

25Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.

2626:26 Mwa 21:22Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake. 27Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”

2826:28 Mwa 21:22Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe 2926:29 Mwa 31:29, 52; 24:31kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’ ”

3026:30 Mwa 31:54; Kut 18:12Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa. 3126:31 Mwa 21:23, 27Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.

3226:32 Mwa 21:30Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!” 3326:33 Mwa 21:14Naye akakiita Shiba,26:33 Shiba kwa Kiebrania maana yake ni Saba. mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.26:33 Beer-Sheba maana yake ni Kisima cha wale saba, yaani wale kondoo saba ambao Abrahamu aliwatoa kama ushahidi kati yake na Abimeleki.

3426:34 Mwa 36:2Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti. 3526:35 Mwa 27:46; Ay 7:16Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.

King James Version

Genesis 26:1-35

1And there was a famine in the land, beside the first famine that was in the days of Abraham. And Isaac went unto Abimelech king of the Philistines unto Gerar. 2And the LORD appeared unto him, and said, Go not down into Egypt; dwell in the land which I shall tell thee of: 3Sojourn in this land, and I will be with thee, and will bless thee; for unto thee, and unto thy seed, I will give all these countries, and I will perform the oath which I sware unto Abraham thy father; 4And I will make thy seed to multiply as the stars of heaven, and will give unto thy seed all these countries; and in thy seed shall all the nations of the earth be blessed; 5Because that Abraham obeyed my voice, and kept my charge, my commandments, my statutes, and my laws.

6¶ And Isaac dwelt in Gerar: 7And the men of the place asked him of his wife; and he said, She is my sister: for he feared to say, She is my wife; lest, said he, the men of the place should kill me for Rebekah; because she was fair to look upon. 8And it came to pass, when he had been there a long time, that Abimelech king of the Philistines looked out at a window, and saw, and, behold, Isaac was sporting with Rebekah his wife. 9And Abimelech called Isaac, and said, Behold, of a surety she is thy wife: and how saidst thou, She is my sister? And Isaac said unto him, Because I said, Lest I die for her. 10And Abimelech said, What is this thou hast done unto us? one of the people might lightly have lien with thy wife, and thou shouldest have brought guiltiness upon us. 11And Abimelech charged all his people, saying, He that toucheth this man or his wife shall surely be put to death.

12Then Isaac sowed in that land, and received in the same year an hundredfold: and the LORD blessed him.26.12 received: Heb. found 13And the man waxed great, and went forward, and grew until he became very great: 26.13 went…: Heb. went going 14For he had possession of flocks, and possession of herds, and great store of servants: and the Philistines envied him.26.14 servants: or, husbandry 15For all the wells which his father’s servants had digged in the days of Abraham his father, the Philistines had stopped them, and filled them with earth. 16And Abimelech said unto Isaac, Go from us; for thou art much mightier than we.

17¶ And Isaac departed thence, and pitched his tent in the valley of Gerar, and dwelt there. 18And Isaac digged again the wells of water, which they had digged in the days of Abraham his father; for the Philistines had stopped them after the death of Abraham: and he called their names after the names by which his father had called them. 19And Isaac’s servants digged in the valley, and found there a well of springing water.26.19 springing: Heb. living 20And the herdmen of Gerar did strive with Isaac’s herdmen, saying, The water is ours: and he called the name of the well Esek; because they strove with him.26.20 Esek: that is, Contention 21And they digged another well, and strove for that also: and he called the name of it Sitnah.26.21 Sitnah: that is, Hatred 22And he removed from thence, and digged another well; and for that they strove not: and he called the name of it Rehoboth; and he said, For now the LORD hath made room for us, and we shall be fruitful in the land.26.22 Rehoboth: that is Room 23And he went up from thence to Beer-sheba. 24And the LORD appeared unto him the same night, and said, I am the God of Abraham thy father: fear not, for I am with thee, and will bless thee, and multiply thy seed for my servant Abraham’s sake. 25And he builded an altar there, and called upon the name of the LORD, and pitched his tent there: and there Isaac’s servants digged a well.

26¶ Then Abimelech went to him from Gerar, and Ahuzzath one of his friends, and Phichol the chief captain of his army. 27And Isaac said unto them, Wherefore come ye to me, seeing ye hate me, and have sent me away from you? 28And they said, We saw certainly that the LORD was with thee: and we said, Let there be now an oath betwixt us, even betwixt us and thee, and let us make a covenant with thee;26.28 We saw…: Heb. Seeing we saw 29That thou wilt do us no hurt, as we have not touched thee, and as we have done unto thee nothing but good, and have sent thee away in peace: thou art now the blessed of the LORD.26.29 That…: Heb. If thou shalt 30And he made them a feast, and they did eat and drink. 31And they rose up betimes in the morning, and sware one to another: and Isaac sent them away, and they departed from him in peace. 32And it came to pass the same day, that Isaac’s servants came, and told him concerning the well which they had digged, and said unto him, We have found water. 33And he called it Shebah: therefore the name of the city is Beer-sheba unto this day.26.33 Shebah: That is, an oath26.33 Beer-sheba: that is, the well of the oath

34¶ And Esau was forty years old when he took to wife Judith the daughter of Beeri the Hittite, and Bashemath the daughter of Elon the Hittite: 35Which were a grief of mind unto Isaac and to Rebekah.26.35 a grief…: Heb. bitterness of spirit