Mwanzo 25 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 25:1-34

Kifo Cha Abrahamu

1Abrahamu alioa mke mwingine, ambaye jina lake aliitwa Ketura. 225:2 Yer 25:25; Mwa 36:35; 37:28, 36; Kut 2:15; Hes 22:4; 25:6; Amu 6:1-3; 8:22-24; 9:17; Za 83:9; Isa 9:4; 10:26; Hab 3:7; Ay 2:11Huyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. 3Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi. 425:4 Isa 60:6Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Hawa wote walikuwa uzao wa Ketura.

525:5 Mwa 24:36Abrahamu akamwachia Isaki kila kitu alichokuwa nacho. 625:6 Mwa 22:24; 21:10; Amu 6:3, 33; 1Fal 4:30; Eze 25:4Lakini Abrahamu alipokuwa bado hai, akawapa watoto wa masuria wake zawadi, kisha akawaondoa waende kuishi pande za mashariki mbali na mwanawe Isaki.

725:7 Mwa 12:4; 35:28; 47:9, 28; 50:22; Ay 42:16Kwa jumla, Abrahamu aliishi miaka 175. 825:8 Mwa 35:29; 49:29; Hes 20:24; 31:2; Kum 31:14; 32:50; 34:5Ndipo Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa akiwa mwenye umri mzuri, mzee aliyeshiba siku, naye akakusanywa pamoja na watu wake. 925:9 Mwa 35:29; 47:30; 49:31; 23:9; 13:18; 50:13Watoto wake Isaki na Ishmaeli wakamzika katika pango la Makpela karibu na Mamre, katika shamba lililokuwa la Efroni mwana wa Sohari Mhiti, 1025:10 Mwa 10:15Shamba ambalo Abrahamu alilinunua kwa Wahiti. Hapo ndipo Abrahamu alipozikwa pamoja na mkewe Sara. 1125:11 Mwa 12:2; 16:14Baada ya kifo cha Abrahamu, Mungu akambariki mwanawe Isaki, ambaye baadaye aliishi karibu na Beer-Lahai-Roi.

Wana Wa Ishmaeli

1225:12 Mwa 2:4; 17:20; 21:18Hivi ndivyo vizazi vya Ishmaeli mtoto wa Abrahamu, ambaye mjakazi wake Sara, Hagari Mmisri, alimzalia Abrahamu.

1325:13 Mwa 28:9; 36:3; Za 120:5; Isa 21:16; 42:11; 60:7; Yer 2:10; 49:28; Eze 27:21Haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, yaliyoorodheshwa kulingana na jinsi walivyozaliwa: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli ni Nebayothi, akafuatia Kedari, Adbeeli, Mibsamu, 1425:14 Yos 15:25; Oba 1:1; Isa 21:11Mishma, Duma, Masa, 1525:15 Ay 6:19; Isa 21:14; Yer 25:23; 1Nya 5:19Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema. 1625:16 Mwa 17:20; 13:16; Za 83:9Hawa walikuwa wana wa Ishmaeli na haya ni majina ya viongozi wa makabila kumi na mawili kulingana na makao yao na kambi zao. 17Kwa jumla Ishmaeli aliishi miaka 137. Akapumua pumzi ya mwisho, akafa, naye akakusanywa pamoja na watu wake. 1825:18 Mwa 17:20; 21:18; 16:7, 12Wazao wa Ishmaeli waliishi kuanzia nchi ya Havila hadi Shuri, karibu na mpaka wa Misri, unapoelekea Ashuru. Hao waliishi kwa uhasama na ndugu zao wote.

Yakobo Na Esau

19Hivi ndivyo vizazi vya Isaki mwana wa Abrahamu.

Abrahamu akamzaa Isaki, 2025:20 Mwa 26:34; 48:7; 35:28; 24:67; 22:22; 28:2-6; 30:20; 31:18; 33:18; 46:15; 24:29; Kum 26:5Isaki alikuwa na umri wa miaka arobaini alipomwoa Rebeka binti Bethueli Mwaramu kutoka Padan-Aramu, nduguye Labani Mwaramu.

2125:21 Mwa 30:17, 22; 11:30; Ezr 8:23; 1Sam 1:17, 23; 1Nya 5:20; 2Nya 33:13; Za 127:3Isaki akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, kwa sababu alikuwa tasa. Bwana akajibu maombi yake na Rebeka mkewe akapata mimba. 2225:22 Kut 18:15; 28:30; 33:7; Law 24:12; Hes 9:6-8; 27:5; Kum 17:9; 2Fal 3:11; 22:13; Isa 30:2; Yer 21:2; 37:7; Eze 14:7; 2Watoto wakashindana tumboni mwake, akasema, “Kwa nini haya yanatokea kwangu?” Kwa hiyo akaenda kumuuliza Bwana.

23Bwana akamjibu,

“Mataifa mawili yamo tumboni mwako,

na mataifa hayo mawili

kutoka ndani yako watatenganishwa.

Mmoja atakuwa na nguvu zaidi kuliko mwingine,

na yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.”

24Wakati wake wa kujifungua ulipotimia, walikuwepo mapacha wa kiume tumboni mwake. 25Wa kwanza kuzaliwa alikuwa mwekundu, mwili wake wote ulikuwa kama mtu aliyevaa vazi lenye nywele; wakamwita jina lake Esau.25:25 Esau maana yake Mwenye nywele nyingi. 26Baadaye, ndugu yake akatoka, mkono wake ukiwa umemshika Esau kisigino; akaitwa jina lake Yakobo.25:26 Yakobo maana yake Ashikaye kisigino, au Atwaaye mahali pa mwingine, au Mdanganyaji, au Mwenye hila, au Mlaghai, au Mjanja. Isaki alikuwa mwenye miaka sitini Rebeka alipowazaa.

27Watoto wakakua, naye Esau akakuwa mwindaji hodari, mtu wa mbugani, wakati Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa nyumbani. 28Isaki, ambaye alikuwa anapendelea zaidi nyama za porini, alimpenda Esau, bali Rebeka alimpenda Yakobo.

29Siku moja Yakobo alipika mchuzi wa dengu, Esau akarudi kutoka porini akiwa na njaa kali. 30Esau akamwambia Yakobo, “Haraka, nipe huo mchuzi mwekundu! Nina njaa kali sana!” (Hii ndiyo sababu pia aliitwa Edomu.)25:30 Edomu maana yake Mwekundu.

31Yakobo akamjibu, “Niuzie kwanza haki yako ya mzaliwa wa kwanza.”

32Esau akasema, “Tazama, mimi niko karibu ya kufa, itanifaa nini haki ya mzaliwa wa kwanza?”

33Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Hivyo Esau akamwapia, akamuuzia Yakobo haki yake ya kuzaliwa.

34Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake.

Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

King James Version

Genesis 25:1-34

1Then again Abraham took a wife, and her name was Keturah. 2And she bare him Zimran, and Jokshan, and Medan, and Midian, and Ishbak, and Shuah. 3And Jokshan begat Sheba, and Dedan. And the sons of Dedan were Asshurim, and Letushim, and Leummim. 4And the sons of Midian; Ephah, and Epher, and Hanoch, and Abidah, and Eldaah. All these were the children of Keturah.

5¶ And Abraham gave all that he had unto Isaac. 6But unto the sons of the concubines, which Abraham had, Abraham gave gifts, and sent them away from Isaac his son, while he yet lived, eastward, unto the east country. 7And these are the days of the years of Abraham’s life which he lived, an hundred threescore and fifteen years. 8Then Abraham gave up the ghost, and died in a good old age, an old man, and full of years; and was gathered to his people. 9And his sons Isaac and Ishmael buried him in the cave of Machpelah, in the field of Ephron the son of Zohar the Hittite, which is before Mamre; 10The field which Abraham purchased of the sons of Heth: there was Abraham buried, and Sarah his wife.

11¶ And it came to pass after the death of Abraham, that God blessed his son Isaac; and Isaac dwelt by the well Lahai-roi.

12¶ Now these are the generations of Ishmael, Abraham’s son, whom Hagar the Egyptian, Sarah’s handmaid, bare unto Abraham: 13And these are the names of the sons of Ishmael, by their names, according to their generations: the firstborn of Ishmael, Nebajoth; and Kedar, and Adbeel, and Mibsam, 14And Mishma, and Dumah, and Massa, 15Hadar, and Tema, Jetur, Naphish, and Kedemah:25.15 Hadar: or, Hadad 16These are the sons of Ishmael, and these are their names, by their towns, and by their castles; twelve princes according to their nations. 17And these are the years of the life of Ishmael, an hundred and thirty and seven years: and he gave up the ghost and died; and was gathered unto his people. 18And they dwelt from Havilah unto Shur, that is before Egypt, as thou goest toward Assyria: and he died in the presence of all his brethren.25.18 died: Heb. fell

19¶ And these are the generations of Isaac, Abraham’s son: Abraham begat Isaac: 20And Isaac was forty years old when he took Rebekah to wife, the daughter of Bethuel the Syrian of Padan-aram, the sister to Laban the Syrian. 21And Isaac intreated the LORD for his wife, because she was barren: and the LORD was intreated of him, and Rebekah his wife conceived. 22And the children struggled together within her; and she said, If it be so, why am I thus? And she went to enquire of the LORD. 23And the LORD said unto her, Two nations are in thy womb, and two manner of people shall be separated from thy bowels; and the one people shall be stronger than the other people; and the elder shall serve the younger.

24¶ And when her days to be delivered were fulfilled, behold, there were twins in her womb. 25And the first came out red, all over like an hairy garment; and they called his name Esau. 26And after that came his brother out, and his hand took hold on Esau’s heel; and his name was called Jacob: and Isaac was threescore years old when she bare them. 27And the boys grew: and Esau was a cunning hunter, a man of the field; and Jacob was a plain man, dwelling in tents. 28And Isaac loved Esau, because he did eat of his venison: but Rebekah loved Jacob.25.28 he…: Heb. venison was in his mouth

29¶ And Jacob sod pottage: and Esau came from the field, and he was faint: 30And Esau said to Jacob, Feed me, I pray thee, with that same red pottage; for I am faint: therefore was his name called Edom.25.30 with…: Heb. with that red, with that red pottage25.30 Edom: that is Red 31And Jacob said, Sell me this day thy birthright. 32And Esau said, Behold, I am at the point to die: and what profit shall this birthright do to me?25.32 at…: Heb. going to die 33And Jacob said, Swear to me this day; and he sware unto him: and he sold his birthright unto Jacob. 34Then Jacob gave Esau bread and pottage of lentiles; and he did eat and drink, and rose up, and went his way: thus Esau despised his birthright.