Mithali 13 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 13:1-25

Mema Ya Muda Mfupi Na Yale Ya Kudumu

113:1 1Sam 2:25; Mit 10:1; 12:1; 15:5Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye,

bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.

213:2 Mit 12:14Kutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema,

bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri.

313:3 Za 12:2; Yak 3:2; Mit 10:6; Ay 1:22Yeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake,

bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia.

413:4 Mit 21:25-26Mvivu hutamani sana na hapati kitu,

bali nafsi ya mwenye bidii

hutoshelezwa kikamilifu.

513:5 Kol 3:9; Rum 12:9Mwenye haki huchukia uongo,

bali waovu huleta aibu na fedheha.

613:6 Mit 11:3-5; Yer 44:5Haki humlinda mtu mwadilifu,

bali uovu humwangusha mwenye dhambi.

713:7 2Kor 6:10Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote;

mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi.

813:8 Mit 15:16Utajiri wa mtu waweza kukomboa maisha yake,

bali mtu maskini hasikii kitisho.

913:9 Ay 18:5; Mit 4:18-19Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana,

bali taa ya mwovu itazimwa.

1013:10 Amu 19:30; Mit 9:9Kiburi huzalisha magomvi tu,

bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri.

1113:11 Mit 10:2; 9:9; 20:21Fedha isiyo ya halali hupungua,

bali yeye akusanyaye fedha kidogo kidogo huongezeka.

1213:12 Mit 10:11Kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua,

bali tumaini lililotimizwa ni mti wa uzima.

1313:13 Hes 15:31; Kut 9:20; Mit 16:20; 2Nya 36:16Yeye anayedharau mafundisho anajiletea maangamizi,

bali yeye anayeheshimu agizo hupewa tuzo.

1413:14 Mit 10:11; 14:27Mafundisho ya mwenye busara ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

15Ufahamu mzuri hupata upendeleo,

bali njia ya asiye mwaminifu ni ngumu.

1613:16 Es 5:11; Mit 12:23Kila mwenye busara hutenda kwa maarifa,

bali mpumbavu hudhihirisha upumbavu wake.

1713:17 Mit 10:26; 25:13Mjumbe mwovu huanguka kwenye taabu,

bali mjumbe mwaminifu huleta uponyaji.

1813:18 Mit 15:31-32; Za 141:5Yeye anayedharau maonyo hupata umaskini na aibu,

bali yeye anayekubali maonyo huheshimiwa.

1913:19 Mit 10:11Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi,

bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya.

2013:20 2Nya 10:8Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima,

bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara.

2113:21 Za 32:10; Mit 19:17; 11:12Balaa humwandama mtenda dhambi,

bali mafanikio ni thawabu kwa mwenye haki.

2213:22 Es 8:2; Mhu 2:26Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi,

bali mali ya wenye dhambi imehifadhiwa

kwa ajili ya wenye haki.

2313:23 Mit 12:11Shamba la mtu maskini laweza kuzalisha chakula kingi,

bali dhuluma hukifutilia mbali.

2413:24 Mit 29:15-17; Efe 6:4Yeye aizuiaye fimbo yake hampendi mwanawe,

bali yeye ampendaye

huwa mwangalifu kumwadibisha.

2513:25 Za 34:10; Mit 10:3Mwenye haki hula mpaka akaridhisha moyo wake,

bali tumbo la mwovu hutaabika kwa njaa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 13:1-25

1智慧儿听从父训,

嘲讽者不听责备。

2口出良言尝善果,

奸徒贪行残暴事13:2 奸徒贪行残暴事”或译“奸徒必饱受虐待”。

3说话谨慎,可保性命;

口无遮拦,自取灭亡。

4懒惰人空有幻想,

勤快人心想事成。

5义人憎恶虚谎,

恶人行事可耻。

6公义守卫正直的人,

邪恶倾覆犯罪之徒。

7有人强充富有,

其实身无分文;

有人假装贫穷,

却是腰缠万贯。

8富人用财富赎命,

穷人却免受惊吓。

9义人的光灿烂,

恶人的灯熄灭。

10自高自大招惹纷争,

虚心受教才是睿智。

11不义之财必耗尽,

勤俭积蓄财富增。

12盼望无期,使人忧伤;

夙愿得偿,带来生机13:12 带来生机”希伯来文是“使人像棵生命树”。

13蔑视训言,自招灭亡;

敬畏诫命,必得赏赐。

14智者的训言是生命之泉,

可使人避开死亡的网罗。

15睿智使人蒙恩惠,

奸徒之路通灭亡。

16明哲知而后行,

愚人炫耀愚昧。

17奸恶的使者陷入灾祸,

忠诚的使者带来医治。

18不受管教的贫穷羞愧,

接受责备的受到尊崇。

19愿望实现使心甘甜,

远离恶事为愚人憎恶。

20与智者同行必得智慧,

与愚人结伴必受亏损。

21祸患追赶罪人,

义人必得善报。

22善人为子孙留下产业,

罪人给义人积聚财富。

23穷人的田地出产丰富,

因不公而被抢掠一空。

24不用杖管教儿女是憎恶他们,

疼爱儿女的随时管教他们。

25义人丰衣足食,

恶人食不果腹。