Mithali 12 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 12:1-28

Mafundisho Ya Kifamilia Na Ya Kijamii

112:1 Mit 5:11-14; 9:7-9; 13:1, 18; 15:5, 10Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa,

bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.

212:2 Ay 33:26; Za 84:11; 2Sam 15:3; Mit 11:20Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana,

bali Bwana humhukumu mwenye hila.

312:3 Mit 10:25Mtu hathibitiki kutokana na uovu,

bali mwenye haki hataondolewa.

412:4 Mit 14:30; 31:23; 1Kor 11:7; Rum 3:11Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe,

bali aaibishaye ni kama uozo

katika mifupa ya mumewe.

5Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki,

bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.

612:6 Mit 11:9; 14:3Maneno ya waovu huotea kumwaga damu,

bali maneno ya waadilifu huwaokoa.

712:7 Mt 7:24; Za 37:34; Mit 14:11; 15:25Watu waovu huondolewa na kutoweka,

bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.

812:8 1Sam 13:13; Mal 2:8-9; Mt 27:4-5Mtu husifiwa kulingana na hekima yake,

bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.

9Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi,

kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.

1012:10 Kum 25:4; Hes 22:29Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake,

bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.

1112:11 Mwa 3:19; Efe 4:28Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.

1212:12 Za 1:3; Lk 8:15Waovu hutamani mateka ya watu wabaya,

bali shina la mwenye haki hustawi.

1312:13 Za 59:12; Mit 10:6; 21:23; 2Pet 2:9Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi,

bali mwenye haki huepuka taabu.

1412:14 Mit 15:23; 14:14; Isa 3:10-11Kutokana na tunda la midomo yake

mtu hujazwa na mambo mema,

hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.

1512:15 Mit 16:2, 25; Lk 18:11Njia ya mpumbavu huonekana sawa

machoni pake mwenyewe,

bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.

1612:16 1Sam 25:25; Ay 5:2; Mit 29:11Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja,

bali mtu wa busara hupuuza matukano.

1712:17 Za 12:2; Mit 14:5, 25Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika,

bali shahidi wa uongo husema uongo.

1812:18 Za 57:4; Mit 25:18; 15:4Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,

bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.

1912:19 Zek 1:5, 6Midomo isemayo kweli hudumu milele,

bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.

2012:20 Rum 14:19Upo udanganyifu katika mioyo

ya wale ambao hupanga mabaya,

bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.

2112:21 Ay 4:7; Za 91:10; Rum 8:28Hakuna dhara linalompata mwenye haki,

bali waovu wana taabu nyingi.

2212:22 1Fal 13:18; Ufu 22:15; Mit 11:20Bwana anachukia sana midomo idanganyayo,

bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.

2312:23 Mit 10:14; Za 38:5; 59:7; Mit 18:2Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,

bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.

2412:24 Mit 10:4; 1Fal 11:28Mikono yenye bidii itatawala,

bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.

2512:25 Mit 15:13; Isa 50:4Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,

bali neno la huruma humfurahisha.

2612:26 Za 95:10Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,

bali njia ya waovu huwapotosha.

27Mtu mvivu haoki mawindo yake,

bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.

2812:28 Kum 30:15; Rum 5:21; Mit 10:2Katika njia ya haki kuna uzima;

katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 12:1-28

1喜爱管教的喜爱知识,

厌恶责备的愚不可及。

2善良的人蒙耶和华赐恩,

诡诈的人被耶和华定罪。

3人不能靠恶行坚立自己,

义人的根基却不会动摇。

4贤德的妻子是丈夫的冠冕,

无耻的妻子如丈夫的骨瘤。

5义人的心思公平正直,

恶人的计谋阴险诡诈。

6恶人的言语暗藏杀机,

正直人的口拯救生命。

7恶人覆灭不复存在,

义人的家屹立不倒。

8人有智慧受称赞,

心术不正遭唾弃。

9地位卑微却有仆人,

胜过自高却饿肚子。

10义人顾惜自己的牲畜,

恶人的怜悯也是残忍。

11努力耕耘者丰衣足食;

追求虚荣者愚不可及。

12恶人贪恋坏人的赃物,

义人的根结出硕果。

13恶人被自己的恶言所困,

但义人可以脱离险境。

14口出良言,饱尝美福;

双手勤劳,终得回报。

15愚人自以为是,

智者肯听劝诫。

16愚人难压怒气,

明哲忍辱负重。

17忠实的证人讲真话,

作伪证者满口谎言。

18出言不慎犹如利剑伤人,

智者之言却能医治创伤。

19诚实的口永远长存,

撒谎的舌转瞬即逝。

20图谋恶事的心怀诡诈,

劝人和睦的喜乐洋溢。

21义人无往不利,

恶人灾祸连连。

22耶和华厌恶说谎的嘴,

祂喜爱行为诚实的人。

23明哲不露锋芒,

愚人心吐愚昧。

24殷勤的手必掌权,

懒惰者必做奴仆。

25忧虑的心使人消沉,

一句良言振奋人心。

26义人引人走正路,

恶人领人入歧途。

27懒汉不烤猎物,

勤快人得资财。

28公义的道上有生命,

公义的路上无死亡。