Mhubiri 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 1:1-18

Kila Kitu Ni Ubatili Mtupu

11:1 Mhu 7:27; 12:10Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu:

21:2 Za 39:5-6; 62:9; Rum 8:20-21; Mhu 4:4-6; 12:8“Ubatili mtupu! Ubatili mtupu!”

Mhubiri anasema.

“Ubatili mtupu!

Kila kitu ni ubatili.”

31:3 Mhu 3:9; 5:15-16; 2:11-22Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote

anayotaabikia chini ya jua?

41:4 2Pet 3:10; Za 104:5; Ay 8:19Vizazi huja na vizazi hupita,

lakini dunia inadumu milele.

51:5 Za 19:5-6Jua huchomoza na jua huzama,

nalo huharakisha kurudi mawioni.

6Upepo huvuma kuelekea kusini

na kugeukia kaskazini,

hurudia mzunguko huo huo,

daima ukirudia njia yake.

71:7 Ay 36:28; 38:10Mito yote hutiririka baharini,

hata hivyo bahari kamwe haijai.

Mahali mito inapotoka,

huko hurudi tena.

81:8 Mhu 3:1; Mit 27:20Vitu vyote vinachosha,

zaidi kuliko mtu anavyoweza kusema.

Jicho kamwe halitosheki kutazama,

wala sikio halishibi kusikia.

91:9 Mwa 8:22; Mhu 3:15; 2:12Kile kilichokuwepo kitakuwepo tena,

kile kilichofanyika kitafanyika tena,

hakuna kilicho kipya chini ya jua.

10Kuna kitu chochote ambacho mtu anaweza kusema,

“Tazama! Kitu hiki ni kipya”?

Kilikuwepo tangu zamani za kale,

kilikuwepo kabla ya wakati wetu.

111:11 Mhu 8:10; 9:5, 15; 2:16; Za 88:12; Mwa 40:23Hakuna kumbukumbu ya watu wa zamani,

hata na wale ambao hawajaja bado

hawatakumbukwa

na wale watakaofuata baadaye.

Hekima Ni Ubatili

12Mimi, Mhubiri, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu. 131:13 Mwa 3:17-19; Mhu 3:10; Ay 28:3Nilitumia muda wangu wote kujifunza na kuvumbua kwa hekima yote yanayofanyika chini ya mbingu. Jinsi gani Mungu ameweka mzigo mzito juu ya wanadamu! 141:14 Mhu 2:11; 4:4; 6:9Nimeshaona mambo yote yanayotendeka chini ya jua, hayo yote ni ubatili, hii ni kukimbiza upepo.

151:15 Mhu 7:13Kilichopindika hakiwezi kunyooshwa,

kile ambacho hakipo haiwezekani kukihesabu.

161:16 1Fal 3:12; 4:30; Mhu 2:9Niliwaza mwenyewe, “Tazama, nimekua na kuongezeka katika hekima kuliko yeyote aliyewahi kutawala Yerusalemu kabla yangu. Nimekuwa na uzoefu mkubwa wa hekima na maarifa.” 171:17 1The 5:21; Mhu 7:23, 25; 2:3, 12; 8:16Ndipo nilipojitahidi kufahamu kutofautisha hekima, wazimu na upumbavu, lakini nikatambua hata hili nalo ni kukimbiza upepo.

181:18 Mhu 2:23; 12:12; 7:16; Ay 28:28; Yer 45:3Kwa kuwa hekima nyingi huleta huzuni kubwa;

maarifa yanapoongezeka, masikitiko yanaongezeka.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

传道书 1:1-18

万事虚空

1以下是在耶路撒冷做王的大卫之子——传道者的话。

2传道者说:虚空的虚空,

虚空的虚空,一切都是虚空。

3人在日光之下的一切劳碌有什么益处呢?

4一代过去,一代又来,

大地却永远长存。

5太阳升起,太阳落下,

匆忙回到升起之地。

6风吹向南,又转向北,

循环不息,周而复始。

7江河涌流入海,海却不会满溢;

江河从何处流出,又返回何处。

8万事令人厌烦,人述说不尽。

眼看,看不饱;

耳听,听不够。

9以往发生的事,将来还会发生;

先前做过的事,将来也必再做。

日光之下,根本没有新事。

10人可以指着哪件事说:

“看啊,这是新事”?

所谓的新事在我们以前早就有了。

11过去的事无人记得,

将来的事后人也不记得。

智慧之虚空

12我传道者曾在耶路撒冷以色列的王。 13我专心用智慧去研究、探索天下各样的事,发现上帝给世人的是极重的苦工。 14我观察一切日光之下所做的事,看啊,都是虚空,好像捕风。 15弯曲的不能变直,缺少的无法补足1:15 补足”希伯来文是“数算”。16我心里想:“我获得极大的智慧,远超过以前统治耶路撒冷的人。我拥有丰富的智慧和知识。” 17我又专心察明智慧和知识、狂妄和愚昧,却发现这也是捕风。 18因为智慧越高,愁烦越多;知识越多,痛苦越深。