Utangulizi: Kusudi Na Kiini
11:1 1Fal 4:29-34Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2Kwa kupata hekima na nidhamu;
kwa kufahamu maneno ya busara;
31:3 Mit 2:1; 2:1, 9kwa kujipatia nidhamu na busara,
kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
41:4 Mit 8:5, 12; 2:10-11huwapa busara wajinga,
maarifa na akili kwa vijana;
51:5 Mit 9:9wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,
wenye kupambanua na wapate mwongozo;
61:6 Za 78:2; Mt 13:10-17; Hes 12:8; Amu 14:12kwa kufahamu mithali na mifano,
misemo na vitendawili vya wenye hekima.
71:7 Kut 20:20; Ay 28:28Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa,
lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Onyo Dhidi Ya Ushawishi Wa Marafiki Waovu
81:8 Mit 6:20; 22:17; Kum 21:18Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,
wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
91:9 Mit 3:21-22; 4:1-9Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako,
na mkufu wa kuipamba shingo yako.
101:10 Mwa 39:7; Ay 24:15; Kum 13:8; Rum 16:18Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi,
usikubaliane nao.
111:11 Mit 12:6; Yer 5:26; Mik 7:2Kama wakisema, “Twende tufuatane;
tukamvizie mtu na kumwaga damu,
njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
121:12 Ay 33:18; Mwa 38:25; Za 40:3tuwameze wakiwa hai kama kaburi,1:12 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.
13Tutapata aina zote za vitu vya thamani
na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
141:14 Mit 1:19Njoo ushirikiane nasi,
vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
151:15 Za 119:101; Mwa 49:6; Mit 4:14Mwanangu, usiandamane nao.
Usiweke mguu wako katika njia zao,
161:16 Mit 6:18; Isa 59:7kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,
ni wepesi kumwaga damu.
17Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu
wakati ndege wote wanakuona!
181:18 Za 71:10Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe;
hujivizia tu wenyewe!
191:19 Mit 11:19; 15:27; 2Fal 5:20-27Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila;
huuondoa uhai wa wale wenye mali.
Onyo Dhidi Ya Kukataa Hekima
201:20 Ay 28:12; Mt 7:10-13; 9:1-3, 13-15Hekima huita kwa sauti kuu barabarani,
hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
21kwenye makutano ya barabara za mji
zenye makelele mengi hupaza sauti,
kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
221:22 Mit 6:32; 7:7; 8:5; 9:4, 16; Za 50:17“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini?
Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha,
na wapumbavu kuchukia maarifa?
231:23 Yoe 2:28; Yn 7:37Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu,
ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu
na kuwafahamisha maneno yangu.
241:24 Isa 65:12; Zek 7:11Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita
na hakuna yeyote aliyekubali
niliponyoosha mkono wangu,
251:25 Lk 7:30kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote
na hamkukubali karipio langu,
261:26 Za 2:4; Kum 28:63; Mit 10:24mimi nami nitawacheka katika maafa yenu,
nitawadhihaki wakati janga litawapata:
271:27 Za 18:18; Mit 5:12-14wakati janga litawapata kama tufani,
wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,
wakati dhiki na taabu zitawalemea.
281:28 Isa 1:15; Mik 3:4; Eze 8:18; Hos 5:6“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;
watanitafuta lakini hawatanipata.
291:29 Ay 21:14; Isa 27:11; Mdo 7:51Kwa kuwa walichukia maarifa,
wala hawakuchagua kumcha Bwana,
301:30 Ay 21:14; Za 81:11kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,
na kukataa maonyo yangu,
311:31 2Nya 36:16; Yer 14:16watakula matunda ya njia zao,
na watashibishwa matunda ya hila zao.
321:32 Isa 66:4; Yer 2:19Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua,
nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
331:33 Hes 24:21; Za 25:12; 112:8Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama,
atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”
箴言的价值
1这是大卫的儿子以色列王所罗门的箴言。
2为使人认识智慧和教诲,
领悟真知灼见;
3为使人接受劝诫,
为人处事仁义、公平、正直;
4使愚昧人明智,
使青年有知识和明辨力;
5使智者听了长学问,
明哲听了得指引;
6使人领悟箴言和比喻,
明白智者的话和谜语。
7知识始于敬畏耶和华,
愚人轻视智慧和教诲。
8孩子啊,
你要听从父亲的教诲,
不可背弃母亲的训言。
9因为这要作你头上的华冠,
颈上的项链。
10孩子啊,恶人若引诱你,
千万不要听从。
11他们若说:“跟我们来吧,
我们去埋伏杀人,
暗害无辜者取乐;
12我们要像阴间一样生吞他们,
整个吞没他们,
使他们如坠入坟墓的人;
13我们必得到各样宝物,
把战利品装满我们的房屋。
14跟我们一起干吧,
大家有福同享!”
15孩子啊,
不要走他们的道,
切莫行他们的路。
16因为他们奔向罪恶,
急速地去杀人流血。
17在飞鸟眼前设网罗,徒劳无功。
18他们埋伏,却自流己血;
他们伏击,却自害己命。
19这就是贪爱不义之财者的结局,
不义之财终要夺去他们的性命。
智慧的劝诫
20智慧在大街上高喊,
在广场上扬声,
21在热闹的市集宣告,
在城门口演说:
22“你们愚昧人喜爱愚昧,
嘲讽者以嘲弄为乐,
无知者厌恶知识,
要到什么时候呢?
23你们若因我的责备而回转,
我就向你们显明我的旨意1:23 “我就向你们显明我的旨意”希伯来文是“我就将我的灵浇灌你们”。,
叫你们明白我的话语。
24我呼唤你们,
你们却充耳不闻;
我向你们招手,
你们却视若无睹。
25你们漠视我的劝诫,
不接受我的责备。
26因此,
你们遭遇灾难时,
我必发笑;
惊恐临到你们时,
我必嗤笑——
27那时,恐惧如风暴袭击你们,
灾难如旋风临到你们,
忧愁和苦难吞没你们。
28你们呼求我,
我也不回答;
你们恳切地寻找我,
却找不到。
29因为你们厌恶知识,
不愿意敬畏耶和华,
30不接受我的劝诫,
又藐视我的责备。
31所以,你们必自食其果,
因自己的恶谋而吃尽苦头。
32愚昧人背离正道,
自招灭亡;
愚顽人逍遥自在,
毁掉自己。
33然而,那听从我的必安然居住,
得享安宁,
不怕灾祸。”