Danieli 2 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 2:1-49

Ndoto Ya Nebukadneza

12:1 Mwa 20:3; 41:8; Ay 33:15-18; Es 6:1; Dan 6:18; 4:5Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala. 22:2 Mwa 41:8; Kut 7:11; Yer 27:9; Isa 9:13; 44:25; Dan 4:6Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme, 32:3 Dan 4:5akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”

42:4 Ezr 4:7; Neh 2:3; Dan 5:10Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu,2:4 Kutoka hapa hadi Dan 7:28, mwandishi aliandika na Kiaramu. “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”

52:5 Ezr 6:11; Dan 3:29; Mwa 41:32Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi. 62:6 Dan 5:7, 16Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”

7Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”

8Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti: 92:9 Es 4:11; Isa 41:22-24; 2:10Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”

102:10 Dan 3:8; 4:7; 5:8Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote. 112:11 Kut 8:10; Mwa 41:38; Dan 5:11Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”

122:12 Dan 3:13-19; Mit 16:14; 28:15Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli. 132:13 Dan 1:20; 5:19Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.

14Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara. 15Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo. 16Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.

17Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo. 182:18 Isa 37:4; Yer 33:3; Ufu 11:13; Ezr 1:2; Neh 1:4Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli. 192:19 Ay 33:15; Dan 1:17; Hes 12:6; Yos 22:23Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni, 202:20 Za 113:2; 145:1-2; Ay 9:4; Yer 32:19; Ay 12:13na akasema:

“Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele;

hekima na uweza ni vyake.

212:21 Dan 7:25; Ay 12:19; Rum 13:1; Yak 1:5; Yer 27:5; Za 75:6-7; 2Sam 14:17; Dan 4:17Yeye hubadili nyakati na majira;

huwaweka wafalme na kuwaondoa.

Huwapa hekima wenye hekima,

na maarifa wenye ufahamu.

222:22 Mwa 40:8; 1Kor 2:10; Ay 12:22; Ebr 4:13; Isa 45:7; Yak 1:17; Za 139:11-12; Dan 4:17Hufunua siri na mambo yaliyofichika;

anajua yale yaliyo gizani,

nayo nuru hukaa kwake.

232:23 Mwa 31:5; Kut 3:15; Dan 1:17; Eze 28:3Ninakushukuru na kukuhimidi,

Ee Mungu wa baba zangu:

Umenipa hekima na uwezo,

umenijulisha kile tulichokuomba,

umetujulisha ndoto ya mfalme.”

Danieli Aifasiri Ndoto

242:24 Eze 28:3Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”

252:25 Dan 5:13; 6:13; Kum 21:10; Dan 1:6Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”

262:26 Dan 1:7Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”

272:27 Mwa 41:8Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza, 282:28 Yer 10:7; Amo 4:13; Dan 4:5; Mwa 40:8; Dan 10:14; Mt 24:6; Eze 28:3; Dan 1:20lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:

29“Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea. 302:30 Mwa 41:16; Mdo 3:12; Isa 45:3; Amo 4:13; Dan 1:7Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.

312:31 Isa 25:3-5; Hab 1:7“Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake. 32Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba, 33miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa. 342:34 Ay 12:19; Zek 4:6; Isa 60:12; Dan 8:25; Ay 34:24; Za 2:9Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja. 352:35 Isa 41:15-16; 2:3; Ufu 11:15; Za 37:10; Isa 17:13; Zek 12:3; Za 1:4Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.

362:36 Mwa 40:12“Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme. 372:37 Ezr 7:12; Eze 26:7; Yer 27:7; Dan 4:26Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu. 382:38 Dan 4:21; Yer 27:6; Dan 5:18Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.

392:39 Dan 7:5“Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote. 402:40 Dan 7:7; Yn 11:48; Dan 7:232:40 Ufu 12:3; Eze 40:2; Dan 8:7-10Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote. 41Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi. 42Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu. 43Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.

442:44 Mwa 27:29; Mt 21:43-44; 1Sam 9:20; Isa 60:12; Ufu 11:15; 1Kor 15:24-25; Za 145:13; Isa 9:7; Dan 4:34; 6:26; 7:14, 27; Oba 1:12; Mik 4:7, 13; Lk 1:33“Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele. 452:45 Isa 28:16; Dan 8:25; Mwa 41:25; Ufu 22:6Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande.

“Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”

462:46 Mdo 10:25; Dan 8:17; Mdo 14:13; Ezr 6:10Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba. 472:47 Kum 10:17; Dan 11:36; 4:25; 1Tim 6:15; Dan 4:25; 4:9Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”

482:48 Es 8:2; Dan 8:27; Mwa 41:40; 2Fal 25:28; Dan 1:20; 4:9; 5:11Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote. 492:49 Dan 3:30; Mit 28:12; 1:7; Es 2:19; Amo 5:15; Dan 6:2; 3:30Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.

Persian Contemporary Bible

دانيال 2:1-49

خواب نبوكدنصر

1نبوكدنصر در سال دوم سلطنتش خوابی ديد. اين خواب چنان او را مضطرب كرد كه سراسيمه بيدار شد و نتوانست دوباره به خواب رود. 2پس همهٔ منجمان، جادوگران، طالع‌بينان و رمالان خود را احضار كرد تا خوابش را تعبير كنند.

وقتی همه در حضورش ايستادند 3گفت: «خوابی ديده‌ام كه مرا مضطرب كرده، از شما می‌خواهم آن را برای من تعبير كنيد.»

4آنها به زبان ارامی به پادشاه گفتند: «پادشاه تا به ابد زنده بماند! خوابتان را بگوييد تا تعبيرش كنيم.»

5ولی پادشاه جواب داد: «حكم من اين است: اگر شما به من نگوييد چه خوابی ديده‌ام و تعبيرش چيست، دستور می‌دهم شما را تكه‌تكه كنند و خانه‌هايتان را خراب نمايند! 6ولی اگر بگوييد چه خوابی ديده‌ام و تعبيرش چيست، به شما پاداش و انعام می‌دهم و عزت و افتخار می‌بخشم. حال، بگوييد چه خوابی ديده‌ام و تعبيرش چيست؟»

7ايشان باز گفتند: «اگر شما خوابتان را برای ما تعريف نكنيد چطور می‌توانيم تعبيرش كنيم؟»

8پادشاه جواب داد: «مطمئنم دنبال فرصت می‌گرديد كه از حكم من جان به در ببريد؛ 9ولی بدانيد اگر خواب را نگوييد حكم من در مورد شما اجرا خواهد شد. شما با هم تبانی كرده‌ايد كه به من دروغ بگوييد به اميد اينكه باگذشت زمان اين موضوع فراموش شود. خواب مرا بگوييد تا من هم مطمئن شوم تعبيری كه می‌كنيد درست است.»

10حكيمان در جواب پادشاه گفتند: «در تمام دنيا كسی پيدا نمی‌شود كه بتواند اين خواستهٔ پادشاه را انجام دهد. تا به حال هيچ پادشاه يا حاكمی، از منجمان و جادوگران و طالع‌بينان خود چنين چيزی نخواسته است. 11آنچه كه پادشاه می‌خواهند ناممكن است. هيچكس جز خدايان نمی‌تواند به شما بگويد چه خوابی ديده‌ايد. خدايان هم با انسانها زندگی نمی‌كنند تا از ايشان كمک بگيريم.»

12پادشاه وقتی اين را شنيد چنان خشمگين شد كه فرمان قتل تمام حكيمان بابل را صادر كرد. 13دانيال و يارانش هم جزو كسانی بودند كه می‌بايست كشته شوند.

14‏-15اما دانيال نزد اريوک رئيس جلادان كه مأمور اجرای فرمان بود، رفت و با حكمت و بصيرت در اين باره با او سخن گفت. دانيال پرسيد: «چرا پادشاه چنين فرمانی صادر كرده است؟» آنگاه اريوک تمام ماجرا را برای دانيال تعريف كرد.

16پس دانيال به حضور پادشاه رفت و از او مهلت خواست تا خواب او را تعبير كند. 17سپس به خانه رفت و موضوع را با ياران خود حننيا، ميشائيل و عزريا در ميان نهاد. 18او از ايشان خواست كه از خدای آسمانها درخواست نمايند تا بر ايشان رحم كند و نشان دهد كه پادشاه چه خوابی ديده و تعبيرش چيست، مبادا با ساير حكيمان كشته شوند. 19همان شب در رؤيا آن راز بر دانيال آشكار شد و او خدای آسمانها را ستايش نموده، 20گفت: «بر نام خدا تا ابد سپاس باد! زيرا حكمت و توانايی از آن اوست، 21وقتها و زمانها در دست اوست و اوست كه پادشاهان را عزل و نصب می‌كند. اوست كه به حكيمان، حكمت و به دانايان، دانايی می‌بخشد. 22اوست كه اسرار عميق و نهان را آشكار می‌سازد. او نور است و آنچه را كه در تاريكی مخفی است، می‌داند. 23ای خدای اجدادم، از تو سپاسگزارم، زيرا به من حكمت و توانايی بخشيده‌ای و دعای ما را اجابت كرده، مرا از خواب پادشاه و معنی آن آگاه ساخته‌ای.»

24آنگاه دانيال نزد اريوک كه از طرف پادشاه دستور داشت حكيمان بابل را بكشد، رفت و گفت: «حكيمان بابل را نكش. مرا نزد پادشاه ببر تا آنچه را می‌خواهد بداند به او بگويم.»

25پس اريوک با عجله دانيال را به حضور پادشاه برد و گفت: «من يكی از اسيران يهودی را پيدا كرده‌ام كه می‌تواند خواب پادشاه را بگويد.»

26پادشاه به دانيال گفت: «آيا تو می‌توانی بگويی چه خوابی ديده‌ام و تعبيرش چيست؟»

27دانيال جواب داد: «هيچ حكيم، منجم، جادوگر و طالع‌بينی نمی‌تواند اين خواستهٔ پادشاه را به جا آورد. 28ولی خدايی در آسمان هست كه رازها را آشكار می‌سازد. او آنچه را كه در آينده می‌بايد اتفاق بيفتد، از پيش به پادشاه خبر داده است. خوابی كه پادشاه ديده، اين است:

29«ای پادشاه، وقتی در خواب بوديد، خدايی كه رازها را آشكار می‌سازد شما را از آنچه كه در آينده اتفاق خواهد افتاد آگاه ساخت. 30اما اين خواب از آن جهت كه از ديگران داناترم بر من آشكار نشد، بلكه از اين نظر بر من آشكار شد تا پادشاه از تعبير آن آگاه شوند.

31«ای پادشاه، در خواب مجسمهٔ بزرگی را ديديد كه بسيار درخشان و ترسناک بود. 32سر اين مجسمه از طلای خالص، سينه و بازوهايش از نقره، شكم و رانهايش از مفرغ، 33ساقهايش از آهن، پاهايش قسمتی از آهن و قسمتی از گل بود. 34در همان حالی كه به آن خيره شده بوديد، سنگی بدون دخالت دست انسان از كوه جدا شد و به پاهای آهنی و گلی آن مجسمه اصابت كرد و آنها را خرد نمود. 35سپس مجسمه، كه از طلا و نقره و مفرغ و گل و آهن بود، فرو ريخت و به شكل ذرات ريز درآمد و باد آنها را مانند كاه پراكنده كرد، به طوری كه اثری از آن باقی نماند. اما سنگی كه آن مجسمه را خرد كرده بود كوه بزرگی شد و تمام دنيا را در برگرفت.

36«خواب اين بود، اما حال تعبير آن:

37«ای پادشاه، شما شاه شاهان هستيد، زيرا خدای آسمانها به شما سلطنت و قدرت و توانايی و شكوه بخشيده است. 38او شما را بر تمام مردم جهان و حيوانات و پرندگان مسلط گردانيده است. سر طلايی آن مجسمه شما هستيد. 39اما وقتی سلطنت شما به پايان رسد، سلطنت ديگری2‏:39 منظور از «سلطنت ديگر» حکومت ماد و پارس است و منظور از «سلطنت سوم» حکومت يونان می‌شد.‏ روی كار خواهد آمد كه ضعيفتر از سلطنت شما خواهد بود. پس از آن، سلطنت سومی كه همان شكم مفرغی آن مجسمه باشد روی كار خواهد آمد و بر تمام دنيا سلطنت خواهد كرد. 40پس از آن، سلطنت چهارم2‏:40 «سلطنت چهارم» احتمالاً حکومت روم می‌شد.‏ به ظهور خواهد رسيد و همچون آهن قوی خواهد بود و همه چيز را در هم كوبيده خرد خواهد كرد. 41‏-42همانطور كه ديديد پاها و انگشتهای مجسمه قسمتی از آهن و قسمتی از گل بود. اين نشان می‌دهد كه اين سلطنت تقسيم خواهد شد و بعضی از قسمتهای آن مثل آهن قوی و بعضی مثل گل ضعيف خواهد بود. 43مخلوط آهن و گل نشان می‌دهد كه خانواده‌های سلطنتی سعی خواهند كرد از راه وصلت، با يكديگر متحد شوند، ولی همانطور كه آهن با گل مخلوط نمی‌شود، آنها نيز متحد نخواهند شد.

44«در دوران سلطنت آن پادشاهان، خدای آسمانها سلطنتی برقرار خواهد ساخت كه هرگز از بين نخواهد رفت و كسی بر آن پيروز نخواهد شد، بلكه همهٔ آن سلطنتها را در هم كوبيده مغلوب خواهد ساخت و خودش تا ابد پايدار خواهد ماند. 45اين است معنی آن سنگی كه بدون دخالت دست انسان از كوه جدا شد و تمام آهن، مفرغ، گل، نقره و طلا را خرد كرد. به اين وسيله خدای بزرگ آنچه را كه در آينده اتفاق خواهد افتاد، به پادشاه نشان داده است. تعبير خواب عين همين است كه گفتم.»

46آنگاه نبوكدنصر در برابر دانيال خم شده او را تعظيم كرد و دستور داد برای او قربانی كنند و بخور بسوزانند. 47پادشاه به دانيال گفت: «براستی خدای شما خدای خدايان و خداوند پادشاهان و آشكار كنندهٔ اسرار است، چون او اين راز را بر تو آشكار كرده است.»

48سپس، پادشاه به دانيال مقام والايی داد و هدايای ارزندهٔ فراوانی به او بخشيد و او را حاكم تمام بابل و رئيس همهٔ حكيمان خود ساخت. 49آنگاه پادشاه در پی درخواست دانيال، شدرک و ميشک و عبدنغو را بر ادارهٔ امور مملكتی گماشت، اما خود دانيال در دربار نبوكدنصر ماند.