Danieli 3 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 3:1-30

Sanamu Ya Dhahabu Na Moto Mkali

13:1 Isa 41:24; 46:6; Hab 2:19; Yer 16:20Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini,3:1 Dhiraa sitini ni sawa na mita 27. na upana wa dhiraa sita,3:1 Dhiraa sita ni sawa na mita 2.7. akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli. 23:2 Es 1:1; Dan 6:7Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha. 33:3 Rum 1:20-23; Mdo 19:34-35; Mt 7:13Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.

43:4 Dan 6:25; Ufu 10:11; Dan 4:1Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya: 53:5 Dan 4:1Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha. 63:6 Yer 29:22; Ufu 13:15; Mt 13:42, 50; Dan 5:19; 6:7Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”

7Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.

83:8 Isa 19:3; Dan 2:10; Ezr 4:12-16Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi. 93:9 Neh 2:3; Dan 6:6; Hos 7:3Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele! 103:10 Dan 6:12Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu, 11na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. 123:12 Dan 2:49; 6:13; Es 3:3Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”

133:13 Dan 2:12; Mdo 5:25-27; Mk 13:9Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme, 143:14 Isa 46:1; Yer 50:2naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha? 153:15 Isa 36:18-20; Kut 5:22; 2Nya 32:15; 32:15; Kut 5:22Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”

163:16 Mt 10:18-19; Dan 1:7Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili. 173:17 Mwa 48:16; Za 18:48; Ay 5:19; 2Kor 1:10; Dan 6:20; Yer 1:8Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme. 183:18 Kut 1:17; Yos 24:15Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”

193:19 Law 26:18-28Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake 20na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto. 21Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine. 22Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego. 23Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.

24Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?”

Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”

25Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”

26Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!”

Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto. 273:27 Dan 6:7; Ebr 11:32-34; Za 91:3-11; Dan 6:23; Isa 43:2Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.

283:28 Za 34:7; Mdo 5:19; Kum 31:20; Ay 13:15; Dan 6:22; Za 97:10; Mdo 12:11Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao. 293:29 Dan 6:26-27; Ezr 6:11Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”

303:30 Dan 2:49Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.

Persian Contemporary Bible

دانيال 3:1-30

مجسمهٔ طلا و كورهٔ آتش

1نبوكدنصر مجسمه‌ای از طلا به بلندی سی متر و پهنای سه متر ساخت و آن را در دشت «دورا» در سرزمين بابل بر پا نمود. 2‏-3سپس به تمام اميران، حاكمان، واليان، قاضيان، خزانه‌داران، مشاوران، وكيلان و ساير مقامات مملكت پيغام فرستاد كه برای تبرک نمودن مجسمه‌اش بيايند. وقتی همه آمدند و در برابر آن مجسمه ايستادند، 4جارچی دربار با صدای بلند اعلام كرد: «ای مردمی كه از نژادها، قومها و زبانهای گوناگون جمع شده‌ايد، فرمان پادشاه را بشنويد: 5وقتی صدای آلات موسيقی را شنيديد همه بايد به خاک بيفتيد و مجسمهٔ طلا را كه نبوكدنصر پادشاه بر پا كرده، سجده كنيد. 6هر كه از اين فرمان سرپيچی نمايد، بی‌درنگ به داخل كورهٔ آتش انداخته خواهد شد.»

7پس وقتی آلات موسيقی نواخته شدند، همهٔ مردم، از هر قوم و نژاد و زبان كه بودند به خاک افتادند و مجسمه را سجده كردند.

8‏-9ولی عده‌ای از بابليان نزد پادشاه رفتند و عليه يهوديان، زبان به اعتراض گشوده، گفتند: «پادشاه تا به ابد زنده بماند! 10فرمانی از پادشاه صادر شد كه وقتی صدای آلات موسيقی شنيده شود، همه بايد به خاک بيفتند و مجسمهٔ طلا را بپرستند، 11و اگر كسی اين كار را نكند، به داخل كورهٔ آتش انداخته شود. 12چند يهودی به نامهای شدرک، ميشک و عبدنغو، يعنی همان كسانی كه بر ادارهٔ مملكتی بابل گماشته‌ايد، از دستور پادشاه سرپيچی می‌كنند و حاضر نيستند خدايان شما را بپرستند و مجسمهٔ طلا را كه بر پا نموده‌ايد، سجده كنند.»

13نبوكدنصر بسيار غضبناک شد و دستور داد شدرک، ميشک و عبدنغو را به حضورش بياورند. وقتی آنها را آوردند 14پادشاه از ايشان پرسيد: «ای شدرک، ميشک و عبدنغو آيا حقيقت دارد كه نه خدايان مرا می‌پرستيد و نه مجسمهٔ طلا را كه بر پا نموده‌ام؟ 15حال خود را آماده كنيد تا وقتی صدای آلات موسيقی را می‌شنويد به خاک بيفتيد و مجسمه را سجده كنيد. اگر اين كار را نكنيد بی‌درنگ به داخل كورهٔ آتش انداخته خواهيد شد؛ آنگاه ببينم كدام خدايی می‌تواند شما را از دست من برهاند.»

16شدرک، ميشک و عبدنغو جواب دادند: «ای نبوكدنصر، ما را باكی نيست كه چه بر سرمان خواهد آمد. 17اگر به داخل كورهٔ آتش انداخته شويم، خدای ما كه او را می‌پرستيم قادر است ما را نجات دهد. پس ای پادشاه، او ما را از دست تو خواهد رهانيد. 18ولی حتی اگر نرهاند، بدان كه خدايان و مجسمهٔ طلای تو را سجده نخواهيم كرد.»

19نبوكدنصر به شدت بر شدرک، ميشک و عبدنغو غضبناک شد و دستور داد آتش كوره را هفت برابر بيشتر كنند 20و چند نفر از قويترين سربازان خود را احضار كرد تا شدرک، ميشک و عبدنغو را ببندند و در آتش بيندازند. 21پس آنها را محكم بستند و به داخل كوره انداختند. 22آتش كوره كه به دستور پادشاه زياد شده بود آنچنان شديد بود كه سربازان مأمور اجرای حكم پادشاه را كشت! 23به اين ترتيب، شدرک و ميشک و عبدنغو دست و پا بسته در ميان شعله‌های سوزان افتادند.

24ناگهان نبوكدنصر حيرت‌زده از جا برخاست و از مشاوران خود پرسيد: «مگر ما سه نفر را در آتش نينداختيم؟»

گفتند: «بلی، ای پادشاه، چنين است.»

25نبوكدنصر گفت: «ولی من چهار نفر را در آتش می‌بينم! دست و پای آنها باز است و در ميان شعله‌های آتش قدم می‌زنند و هيچ آسيبی به آنها نمی‌رسد! چهارمی شبيه خدايان است!»

26آنگاه نبوكدنصر به دهانهٔ كورهٔ آتش نزديک شد و فرياد زد: «ای شدرک، ميشک، عبدنغو! ای خدمتگزاران خدای متعال، بيرون بياييد!» پس ايشان از ميان آتش بيرون آمدند.

27سپس اميران، حاكمان، واليان و مشاوران پادشاه دور ايشان جمع شدند و ديدند آتش به بدن آنها آسيبی نرسانيده، مويی از سرشان سوخته نشده، اثری از سوختگی روی لباسشان نيست و حتی بوی دود نيز نمی‌دهند!

28آنگاه نبوكدنصر گفت: «ستايش بر خدای شدرک، ميشک و عبدنغو كه فرشتهٔ خود را فرستاد تا خدمتگزاران خود را كه به او توكل كرده بودند نجات دهد. آنها فرمان پادشاه را اطاعت نكردند و حاضر شدند بميرند، ولی خدايی را جز خدای خود پرستش و بندگی نكنند.

29«پس فرمان من اين است: از هر نژاد و قوم و زبان، هر کس بر ضد خدای شدرک و ميشک و عبدنغو سخنی بگويد، تكه‌تكه خواهد شد و خانه‌اش خراب خواهد گرديد؛ زيرا هيچ خدايی مانند خدای ايشان نمی‌تواند اينچنين بندگانش را نجات بخشد.»

30پادشاه به شدرک و ميشک و عبدنغو مقام والاتری در سرزمين بابل داد.