1 Nyakati 11 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 11:1-47

Daudi Atiwa Mafuta Kuwa Mfalme Wa Israeli

(2 Samweli 5:1-10)

111:1 1Nya 9:1; Mwa 13:18; 23:19; 2Sam 5:1; 1Nya 12:23Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako. 211:2 1Sam 18:5, 16; Za 78:71; Mt 2:6; 1Nya 5:2Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’ ”

311:3 1Sam 16:1-13; 2Sam 5:3; Rum 8:31Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.

Daudi Ateka Yerusalemu

411:4 Yos 3:10; Amu 1:21; 2Sam 5:6; Mwa 10:16; 15:21; Kut 3:17; Amu 19:10Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo 5wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.

611:6 2Sam 2:13; 8:16Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.

711:7 2Sam 5:7Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi. 811:8 2Sam 5:9; 2Nya 32:5Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu. 911:9 2Sam 3:1; Es 9:4Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.

Mashujaa Wa Daudi

(2 Samweli 23:8-39)

1011:10 1Nya 11:1; 12:23; 2Sam 23:8; 1Sam 16:1, 12Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi. 1111:11 2Sam 17:10Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi:

Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.

12Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu. 1311:13 1Sam 17:1Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti. 1411:14 Kut 14:30; 1Sam 17:10; Mit 21:31Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.

1511:15 1Nya 14:9Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai. 1611:16 2Sam 5:17Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu. 17Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!” 1811:18 Kum 12:16Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana. 19Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa.

Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.

2011:20 1Sam 26:6Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu. 2111:21 2Sam 23:24; 1Nya 27:7Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.

2211:22 Yos 15:21; 1Sam 17:36; 2Sam 1:23; 23:20; 1Nya 12:8Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba. 2311:23 1Sam 26:6Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano.11:23 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao. 24Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu. 25Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.

2611:26 1Nya 2:18; 2Sam 23:24; 1Nya 27:7Wale watu mashujaa walikuwa:

Asaheli nduguye Yoabu,

Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,

2711:27 1Nya 27:8Shamothi Mharori,

Helesi Mpeloni,

2811:28 1Nya 27:12Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa,

Abiezeri kutoka Anathothi,

2911:29 2Sam 21:18Sibekai Mhushathi,

Ilai Mwahohi,

30Maharai Mnetofathi,

Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,

3111:31 1Nya 27:14; Amu 12:13Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini,

Benaya Mpirathoni,

32Hurai kutoka mabonde ya Gaashi,

Abieli Mwaribathi,

33Azmawethi Mbaharumi,

Eliaba Mshaalboni,

34wana wa Hashemu Mgiloni,

Yonathani mwana wa Shagee Mharari,

35Ahiamu mwana wa Sakari Mharari,

Elifale mwana wa Uru,

36Heferi Mmekerathi,

Ahiya Mpeloni,

37Hezro Mkarmeli,

Naarai mwana wa Ezbai,

38Yoeli nduguye Nathani,

Mibhari mwana wa Hagri,

39Seleki Mwamoni,

Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,

4011:40 Yos 15:48; 1Nya 2:50-53Ira Mwithiri,

Garebu Mwithiri,

4111:41 2Sam 11:6; 1Nya 2:36Uria Mhiti,

Zabadi mwana wa Alai,

42Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,

43Hanani mwana wa Maaka,

Yoshafati Mmithni,

4411:44 Kum 1:4Uzia Mwashterathi,

Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,

45Yediaeli mwana wa Shimri,

nduguye Yoha Mtizi,

46Elieli Mmahawi,

Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu,

Ithma Mmoabu,

47Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.

New International Reader’s Version

1 Chronicles 11:1-47

David Becomes King Over Israel

1The whole community of Israel came together to see David at Hebron. They said, “We are your own flesh and blood. 2In the past, Saul was our king. But you led the men of Israel in battle. The Lord your God said to you, ‘You will be the shepherd over my people Israel. You will become their ruler.’ ”

3All the elders of Israel came to see King David at Hebron. There he made a covenant with them in front of the Lord. They anointed David as king over Israel. It happened just as the Lord had promised through Samuel.

David Captures Jerusalem

4David and all the men of Israel marched to Jerusalem. Jerusalem was also called Jebus. The Jebusites who lived there 5said to David, “You won’t get in here.” But David captured the fort of Zion. It became known as the City of David.

6David had said, “Anyone who leads the attack against the Jebusites will become the commander of Israel’s army.” Joab went up first. So he became the commander of the army. He was the son of Zeruiah.

7David moved into the fort. So it was called the City of David. 8He built up the city around the fort. He filled in the low places. He built a wall around it. During that time, Joab built up the rest of the city. 9David became more and more powerful. That’s because the Lord who rules over all was with him.

David’s Mighty Warriors

10The chiefs of David’s mighty warriors and the whole community of Israel helped David greatly. They helped him become king over the entire land. That’s exactly what the Lord had promised him. 11Here is a list of David’s mighty warriors.

Jashobeam was chief of the officers. He was a Hakmonite. He used his spear against 300 men. He killed all of them at one time.

12Next to him was Eleazar. He was one of the three mighty warriors. He was the son of Dodai, the Ahohite. 13Jashobeam was with David at Pas Dammim. The Philistines had gathered there for battle. Israel’s troops ran away from the Philistines. At the place where that happened, there was a field full of barley. 14The three mighty warriors took their stand in the middle of the field. They didn’t let the Philistines capture it. They struck them down. The Lord helped them win a great battle.

15David was near the rock at the cave of Adullam. Three of the 30 chiefs came down to him there. A group of Philistines was camped in the Valley of Rephaim. 16At that time David was in his usual place of safety. Some Philistine troops were stationed at Bethlehem. 17David really wanted some water. He said, “I wish someone would get me a drink of water from the well near the gate of Bethlehem!” 18So the three mighty warriors fought their way past the Philistine guards. They got some water from the well near the gate of Bethlehem. They took the water back to David. But David refused to drink it. Instead, he poured it out as a drink offering to the Lord. 19“I would never drink that water!” David said. “It would be like drinking the blood of these men. They put their lives in danger by going to Bethlehem.” The men had put their lives in danger by bringing the water back. So David wouldn’t drink it.

Those were some of the brave things the three mighty warriors did.

20Abishai was chief over the three mighty warriors. He was the brother of Joab. Abishai used his spear against 300 men. He killed all of them. So he became as famous as the three mighty warriors. 21He was honored twice as much as the three mighty warriors. He became their commander. But he wasn’t included among them.

22Benaiah was a great hero from Kabzeel. He was the son of Jehoiada. Benaiah did many brave things. He struck down two of Moab’s best fighting men. He also went down into a pit on a snowy day. He killed a lion there. 23And Benaiah struck down an Egyptian who was seven and a half feet tall. The Egyptian was holding a spear as big as a weaver’s rod. Benaiah went out to fight against him with a club. He grabbed the spear out of the Egyptian’s hand. Then he killed him with it. 24Those were some of the brave things Benaiah, the son of Jehoiada, did. He too was as famous as the three mighty warriors. 25He was honored more than any of the 30 chiefs. But he wasn’t included among the three mighty warriors. And David put him in charge of his own personal guards.

26Here is a list of David’s mighty warriors.

Asahel, the brother of Joab

Elhanan, the son of Dodo, from Bethlehem

27Shammoth, the Harorite

Helez, the Pelonite

28Ira, the son of Ikkesh, from Tekoa

Abiezer from Anathoth

29Sibbekai, the Hushathite

Ilai, the Ahohite

30Maharai from Netophah

Heled, the son of Baanah, from Netophah

31Ithai, the son of Ribai, from Gibeah in Benjamin

Benaiah from Pirathon

32Hurai from the valleys of Gaash

Abiel, the Arbathite

33Azmaveth, the Baharumite

Eliahba, the Shaalbonite

34the sons of Hashem, the Gizonite

Jonathan, the son of Shagee, the Hararite

35Ahiam, the son of Sakar, the Hararite

Eliphal, the son of Ur

36Hepher, the Mekerathite

Ahijah, the Pelonite

37Hezro from Carmel

Naarai, the son of Ezbai

38Joel, the brother of Nathan

Mibhar, the son of Hagri

39Zelek from Ammon

Naharai, from Beeroth, who carried the armor of Joab, the son of Zeruiah

40Ira, the Ithrite

Gareb, the Ithrite

41Uriah, the Hittite

Zabad, the son of Ahlai

42Adina, the son of Shiza, the Reubenite, who was chief of the Reubenites and the 30 men with him

43Hanan, the son of Maakah

Joshaphat, the Mithnite

44Uzzia, the Ashterathite

Shama and Jeiel, the sons of Hotham from Aroer

45Jediael, the son of Shimri

his brother Joha, the Tizite

46Eliel, the Mahavite

Jeribai and Joshaviah, the sons of Elnaam

Ithmah from Moab

47Eliel

Obed

Jaasiel, the Mezobaite