1 Nyakati 12 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 12:1-40

Mashujaa Waungana Na Daudi

112:1 Yos 15:31; 1Sam 27:2-6Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani, 212:2 Amu 3:15; 20:16; 2Sam 3:19walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):

312:3 Yos 21:18; 1Nya 11:28Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi, 412:4 Yos 15:36; 10:2; 18:21, 25; 1Fal 9:2; Isa 28:21na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi, 5Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi; 6Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora; 712:7 Yos 15:58Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.

812:8 Mwa 30:11; 2Sam 2:18; 17:10; 23:14, 29; 23:20; 1Nya 2:17; Mit 28:1Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.

9Ezeri alikuwa mkuu wao,

Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,

10Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,

11Atai wa sita, Elieli wa saba,

12Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,

13Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.

1412:14 Law 26:8; Kum 32:30Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000. 1512:15 Yos 3:15; Yer 12:5; 49:19Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.

1612:16 2Sam 3:19Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake. 1712:17 Zek 3:2; Yud 9Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”

1812:18 Amu 6:34; 2Nya 15:1; 2Sam 17:25; 1Sam 25:5-6; 1Nya 2:17Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema:

“Sisi tu watu wako, ee Daudi!

Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese!

Ushindi, naam, ushindi uwe kwako,

pia ushindi kwa wale walio upande wako,

kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.”

Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.

1912:19 1Sam 29:2-4Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”) 2012:20 1Sam 27:6Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase. 21Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake. 22Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.

Wengine Waungana Na Daudi Huko Hebroni

2312:23 2Sam 2:3-4; 1Nya 10:14; 1Sam 16:1; 1Nya 11:10Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:

24watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.

25Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.

26Watu wa Lawi walikuwa 4,600, 27pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700, 2812:28 2Sam 8:17; 1Nya 27:17; 1Fal 1:8; 2:25; 1Nya 6:8; Eze 44:15na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.

2912:29 2Sam 3:19; 2:8-9Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.

30Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.

31Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.

3212:32 Es 1:13Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.

33Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.

34Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.

35Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.

36Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.

37Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.

3812:38 2Sam 5:1-3Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme. 3912:39 2Sam 3:20; Isa 25:6-8Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao. 4012:40 2Sam 16:1; 17:29; 1Sam 25:18; 1Nya 29:22Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.

New International Reader’s Version

1 Chronicles 12:1-40

Fighting Men Join David

1Some fighting men came to David at Ziklag. They were among those who helped him in battle. David had been forced to hide from Saul, the son of Kish. 2The men were armed with bows. They were able to shoot arrows or throw stones from a sling with either hand. They were relatives of Saul from the tribe of Benjamin. Here is a list of them.

3Their chief Ahiezer and Joash, the sons of Shemaah the Gibeathite

Jeziel and Pelet, the sons of Azmaveth

Berakah

Jehu from Anathoth

4Ishmaiah, the Gibeonite, who was a mighty warrior among the 30 chiefs and a leader of the 30 chiefs

Jeremiah

Jahaziel

Johanan

Jozabad from Gederah

5Eluzai

Jerimoth

Bealiah

Shemariah

Shephatiah, the Haruphite

6the Korahites Elkanah, Ishiah, Azarel, Joezer and Jashobeam

7Joelah and Zebadiah, the sons of Jeroham from Gedor

8Some men of Gad went over to David’s side at his usual place of safety in the desert. They were brave fighting men. They were ready for battle. They were able to use shields and spears. Their faces were like the faces of lions. They could run as fast as antelopes in the mountains.

9Ezer was their chief.

Obadiah was next in command. Eliab was third.

10Mishmannah was fourth. Jeremiah was fifth.

11Attai was sixth. Eliel was seventh.

12Johanan was eighth. Elzabad was ninth.

13Jeremiah was tenth. And Makbannai was eleventh.

14All these men of Gad were army commanders. The least important of them was equal to 100 men. The most important was equal to 1,000. 15They went across the Jordan River when it was flowing over its banks. That happened in the first month of spring. They chased away everyone who lived in the valleys. They chased them away from the east and west sides of the river.

16Some men from the territories of Benjamin and Judah also came to David at his usual place of safety. 17David went out to meet them. He said to them, “Have you come to me in peace? Have you come to help me? If you have, I’m ready for you to join me. But suppose you have come to hand me over to my enemies when I haven’t even harmed anyone. Then may the God of our people see it and judge you.”

18The Spirit of God came on Amasai. He was leader of the 30 chiefs. He said,

“David, we belong to you!

Son of Jesse, we’re on your side!

May you have great success.

May those who help you also have success.

Your God will help you.”

So David welcomed them. He made them leaders in his army.

19Some people from the tribe of Manasseh went over to David’s side. They did this when he marched out with the Philistines to fight against Saul. But David and his men didn’t help the Philistines. That’s because after all the Philistine rulers had discussed the matter, they sent him away. They said, “Suppose he deserts to his master Saul. Then our heads will be cut off!” 20So David went to Ziklag. Here are the men of Manasseh who went over to his side. They were Adnah, Jozabad, Jediael, Michael, Jozabad, Elihu and Zillethai. They were leaders of groups of 1,000 men in Manasseh. 21They helped David fight against enemy armies. All the men of Manasseh were brave fighting men. They were commanders in David’s army. 22Day after day men came to help David. Soon he had a large army. It was like the army of God.

Other Fighting Men Join David at Hebron

23Large numbers of men came to David at Hebron. They were prepared for battle. They came to hand Saul’s kingdom over to him, just as the Lord had said. Here are the numbers of the men who came.

24The men from Judah carried shields and spears. They were prepared for battle. The total number of them was 6,800.

25The fighting men from Simeon were ready for battle. The total number of them was 7,100.

26The total number of men from Levi was 4,600. 27They included Jehoiada. He was the leader of the family of Aaron. He came with 3,700 men. 28The men from Levi also included Zadok. He was a brave young fighter. He came with 22 officers from his family.

29The men from Benjamin were from Saul’s tribe. Most of them had remained faithful to Saul’s family until that time. The total number of them was 3,000.

30The men from Ephraim were brave fighting men. They were famous in their own family groups. The total number of them was 20,800.

31The men from half of the tribe of Manasseh had been chosen by name to come and make David king. The total number of them was 18,000.

32The men from Issachar understood what was going on at that time. They knew what Israel should do. The total number of their chiefs was 200. They came with all their relatives who were under their command.

33The men from Zebulun knew how to fight well. That’s because they had done it many times before. They were prepared for battle. They had every kind of weapon. They came to help David with their whole heart. The total number of them was 50,000.

34The total number of officers from Naphtali was 1,000. They came with 37,000 men who carried shields and spears.

35The men from Dan were ready for battle. The total number of them was 28,600.

36The men from Asher knew how to fight well. That’s because they had done it many times before. They were prepared for battle. The total number of them was 40,000.

37The men from the tribes of Reuben, Gad and half the tribe of Manasseh were armed with every kind of weapon. The men came from the east side of the Jordan River. The total number of them was 120,000.

38All these fighting men offered to serve in the army.

Before they came to Hebron, they had agreed completely to make David king over all the Israelites. All the rest of the people also agreed to make David king. 39The men spent three days there with David. They ate and drank what their families had given them. 40Their neighbors also brought food. They brought it on donkeys, camels, mules and oxen. They came from as far away as the territories of Issachar, Zebulun and Naphtali. There was plenty of flour, fig cakes, raisin cakes, wine, olive oil, cattle and sheep. The Israelites brought all these things because they were so happy.