Zaburi 88 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 88:1-18

Zaburi 88

Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada

Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.

188:1 Za 51:14; 3:4; 22:2; Lk 18:7Ee Bwana, Mungu uniokoaye,

nimelia mbele zako usiku na mchana.

2Maombi yangu yafike mbele zako,

utegee kilio changu sikio lako.

388:3 Ay 33:22; Isa 38:10; Za 6:3; 25:17; 107:18Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,

na maisha yangu yanakaribia kaburi.88:3 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

488:4 Za 31:12; 18:1Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,

niko kama mtu asiye na nguvu.

588:5 Za 31:22Nimetengwa pamoja na wafu,

kama waliochinjwa walalao kaburini,

ambao huwakumbuki tena,

ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.

688:6 Za 30:1; 69:15; Mao 3:55; Yon 2:3Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,

katika vina vya giza nene.

788:7 Za 7:11; 42:7Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,

umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.

888:8 Ay 3:23; 19:13; Za 31:11; Yer 32:2; 33:1Umenitenga na rafiki zangu wa karibu

na kunifanya chukizo kwao.

Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;

988:9 Za 38:10; 5:2; 143:6; Ay 11:13nuru ya macho yangu

imefifia kwa ajili ya huzuni.

Ee Bwana, ninakuita kila siku,

ninakunyooshea wewe mikono yangu.

1088:10 Za 6:5Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?

Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?

1188:11 Za 30:9Je, upendo wako hutangazwa kaburini,

uaminifu wako katika Uharibifu?88:11 Yaani Abadon.

1288:12 Ay 10:21; 31:12; Mhu 8:10Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,

au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

1388:13 Za 30:2; 5:3; 55:17; 119:147Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie;

asubuhi maombi yangu huja mbele zako.

1488:14 Za 43:2; 13:1Ee Bwana, kwa nini unanikataa

na kunificha uso wako?

1588:15 Dan 9:26; Za 9:12; 129:1; Yer 22:21; Eze 16:22; Hos 2:15; Isa 53:8; Ay 6:4; 18:11; 2Kor 4:8Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;

nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.

1688:16 Za 7:11; Ay 6:4Ghadhabu yako imepita juu yangu;

hofu zako zimeniangamiza.

1788:17 Za 124:4Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;

zimenimeza kabisa.

1888:18 Za 88:8; 38:11; Ay 19:13Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;

giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

Hoffnung für Alle

Psalm 88:1-19

Am Rande des Todes – völlig allein!

1Ein Lied von den Nachkommen Korachs. Der Esrachiter Heman verfasste es zum Nachdenken. Auf eine traurige Weise zu singen.

2Herr, mein Gott, du allein kannst mir noch helfen!

Tag und Nacht schreie ich zu dir!

3Lass mein Gebet zu dir dringen,

verschließ deine Ohren nicht vor meinem Flehen!

4Schweres Leid drückt mich nieder,

ich bin dem Tod schon näher als dem Leben.

5Jeder rechnet damit, dass ich bald sterbe,

denn alle Kraft hat mich verlassen.

6Es geht mir wie den Toten, die du vergessen hast,

fern von deiner Hilfe liegen sie in ihrem Grab.

7Du hast mich in den tiefsten Abgrund gestoßen,

in nichts als unergründliche Finsternis.

8Dein Zorn lastet schwer auf mir,

wie hohe Brandungswellen wirft er mich um.

9Alle meine Freunde hast du mir genommen,

voller Abscheu wandten sie sich von mir ab.

Ich bin gefangen und weiß keinen Ausweg mehr.

10Meine Augen sind vom Weinen ganz verquollen.

Jeden Tag rufe ich, Herr, zu dir

und strecke meine Hände nach dir aus.

11Wirst du an den Toten noch ein Wunder tun?

Kommen sie etwa aus ihren Gräbern, um dich zu loben?

12Erzählt man im Totenreich von deiner Gnade

oder in der Gruft von deiner Treue?

13Sind deine Wunder wohl am Ort der Finsternis bekannt?

Wissen die längst vergessenen Toten von deiner Gerechtigkeit?

14Herr, ich schreie zu dir um Hilfe.

Schon früh am Morgen klage ich dir mein Leid.

15Warum hast du mich verstoßen, Herr?

Warum verbirgst du dich vor mir?

16Seit meiner Jugend bin ich elend und vom Tod gezeichnet.

Du hast mir dieses furchtbare Leid auferlegt –

und jetzt bin ich am Ende!

17Dein glühender Zorn hat mich zu Boden geschmettert,

deine schreckliche Strafe hat mich vernichtet!

18Die Angst bedrängt mich von allen Seiten,

vor dieser tödlichen Flut gibt es kein Entrinnen.

19Du hast erreicht, dass mir alle den Rücken kehren,

Freunde und Nachbarn gehen mir aus dem Weg.

Mein einziger Begleiter ist die Finsternis.