Zaburi 88
Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.
188:1 Za 51:14; 3:4; 22:2; Lk 18:7Ee Bwana, Mungu uniokoaye,
nimelia mbele zako usiku na mchana.
2Maombi yangu yafike mbele zako,
utegee kilio changu sikio lako.
388:3 Ay 33:22; Isa 38:10; Za 6:3; 25:17; 107:18Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,
na maisha yangu yanakaribia kaburi.88:3 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
488:4 Za 31:12; 18:1Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,
niko kama mtu asiye na nguvu.
588:5 Za 31:22Nimetengwa pamoja na wafu,
kama waliochinjwa walalao kaburini,
ambao huwakumbuki tena,
ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
688:6 Za 30:1; 69:15; Mao 3:55; Yon 2:3Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,
katika vina vya giza nene.
788:7 Za 7:11; 42:7Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,
umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
888:8 Ay 3:23; 19:13; Za 31:11; Yer 32:2; 33:1Umenitenga na rafiki zangu wa karibu
na kunifanya chukizo kwao.
Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
988:9 Za 38:10; 5:2; 143:6; Ay 11:13nuru ya macho yangu
imefifia kwa ajili ya huzuni.
Ee Bwana, ninakuita kila siku,
ninakunyooshea wewe mikono yangu.
1088:10 Za 6:5Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?
Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
1188:11 Za 30:9Je, upendo wako hutangazwa kaburini,
uaminifu wako katika Uharibifu?88:11 Yaani Abadon.
1288:12 Ay 10:21; 31:12; Mhu 8:10Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,
au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
1388:13 Za 30:2; 5:3; 55:17; 119:147Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie;
asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
1488:14 Za 43:2; 13:1Ee Bwana, kwa nini unanikataa
na kunificha uso wako?
1588:15 Dan 9:26; Za 9:12; 129:1; Yer 22:21; Eze 16:22; Hos 2:15; Isa 53:8; Ay 6:4; 18:11; 2Kor 4:8Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;
nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
1688:16 Za 7:11; Ay 6:4Ghadhabu yako imepita juu yangu;
hofu zako zimeniangamiza.
1788:17 Za 124:4Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;
zimenimeza kabisa.
1888:18 Za 88:8; 38:11; Ay 19:13Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;
giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.