Zaburi 69
Kilio Cha Kuomba Msaada Wakati Wa Dhiki
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi.
169:1 Za 42:7; 32:6; Yon 2:5Ee Mungu, niokoe,
kwa maana maji yamenifika shingoni.
269:2 Ay 30:19Ninazama kwenye vilindi vya matope,
pasipo mahali pa kukanyaga,
Nimefika kwenye maji makuu,
mafuriko yamenigharikisha.
369:3 Za 6:6; 119:82Nimechoka kwa kuomba msaada,
koo langu limekauka.
Macho yangu yanafifia,
nikimtafuta Mungu wangu.
469:4 Yn 15:25; Za 25:19; 35:19; 38:19; 40:14; 119:95; Isa 32:7Wale wanaonichukia bila sababu
ni wengi kuliko nywele za kichwa changu;
wengi ni adui kwangu bila sababu,
wale wanaotafuta kuniangamiza.
Ninalazimishwa kurudisha
kitu ambacho sikuiba.
569:5 Za 38:5; 44:21Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu,
wala hatia yangu haikufichika kwako.
6Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
wakutumainio wasiaibishwe
kwa ajili yangu;
wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
769:7 Yer 15:15; Za 39:8; 44:15Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako,
aibu imefunika uso wangu.
869:8 Ay 19:13-15; Za 31:11; 38:11; Isa 53:3; Yn 7:5Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
969:9 Yn 2:17; Rum 15:3; Za 89:50-51Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila,
matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
1069:10 Za 35:13Ninapolia na kufunga,
lazima nivumilie matusi.
1169:11 2Sam 3:31; Za 35:13Ninapovaa nguo ya gunia,
watu hunidharau.
1269:12 Mwa 18:1; 23:10; Ay 30:9Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga,
nimekuwa wimbo wa walevi.
1369:13 Isa 49:8; 2Kor 6:2; Za 17:7; 51:1Lakini Ee Bwana, ninakuomba,
kwa wakati ukupendezao;
katika upendo wako mkuu, Ee Mungu,
unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
1469:14 Za 69:2; 144:7Uniokoe katika matope,
usiniache nizame;
niokoe na hao wanichukiao,
kutoka kwenye vilindi vya maji.
1569:15 Za 36:6; 68:22; Hes 21:33; Yer 22:2069:15 Za 28:1; 124:4, 5; Hes 16:33Usiache mafuriko yanigharikishe
au vilindi vinimeze,
au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
1669:16 Za 63:3Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako;
kwa huruma zako nyingi unigeukie.
1769:17 Za 22:24; 143:7; 50:15; 66:14Usimfiche mtumishi wako uso wako,
uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
1869:18 Za 49:15Njoo karibu uniokoe,
nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
1969:19 Za 22:6Unajua jinsi ninavyodharauliwa,
kufedheheshwa na kuaibishwa,
adui zangu wote unawajua.
2069:20 Ay 16:2; Isa 63:5; Za 142:4Dharau zimenivunja moyo
na nimekata tamaa,
nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata,
wa kunituliza, lakini sikumpata.
2169:21 Hes 6:3; Lk 23:36; Mt 27:34, 48; Mk 15:23, 36; Yn 19:28-30Waliweka nyongo katika chakula changu
na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
2269:22 1Sam 28:9; Ay 18:10Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego,
nayo iwe upatilizo na tanzi.
2369:23 Rum 11:9-10Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona,
nayo migongo yao iinamishwe daima.
2469:24 Za 79:6; Yer 10:25Uwamwagie ghadhabu yako,
hasira yako kali na iwapate.
2569:25 Law 26:43; Mt 23:38; Mdo 1:20Mahali pao na pawe ukiwa,
wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
2669:26 Ay 19:22; Zek 1:15Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi,
na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
2769:27 Neh 4:5; Za 109:14Walipize uovu juu ya uovu,
usiwaache washiriki katika wokovu wako.
2869:28 Kut 32:32-33; Lk 10:20; Eze 13:9Wafutwe kutoka kitabu cha uzima
na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
2969:29 Za 20:1Mimi niko katika maumivu na dhiki;
Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
3069:30 Za 28:7; 34:3Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,
nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
3169:31 Za 50:9-13; 51:16Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume,
zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
3269:32 Za 34:2; 22:26Maskini wataona na kufurahi:
ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
3369:33 Za 12:5Bwana huwasikia wahitaji
wala hadharau watu wake waliotekwa.
3469:34 Za 96:11; 98:7; Isa 44:23Mbingu na dunia zimsifu,
bahari na vyote viendavyo ndani yake,
3569:35 Oba 1:17; Ezr 9:9; Za 51:18kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni
na kuijenga tena miji ya Yuda.
Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
3669:36 Za 25:13; 37:29watoto wa watumishi wake watairithi
na wale wote walipendao jina lake
wataishi humo.
第 69 篇
祈求上帝拯救的禱告
大衛作的詩,交給樂長,調用「百合花」。
1上帝啊,求你拯救我,
因為洪水快把我淹沒;
2我深陷泥沼,無法站穩腳;
我落入深淵,被洪流淹沒。
3我連連呼救,已聲嘶力竭;
我期盼上帝的幫助,望眼欲穿。
4無故恨我的人不計其數,
無故害我的仇敵勢力強大,
逼我償還我沒有偷過的東西。
5上帝啊,你知道我的愚昧,
我的罪惡也瞞不過你。
6主——萬軍之耶和華啊,
求你不要使等候你的人因我而受辱;
以色列的上帝啊,
求你不要讓信靠你的人因我而蒙羞。
7我為了你的緣故遭受辱罵,
羞辱滿面。
8我的弟兄視我為陌生人,
我的手足看我為外人。
9我對你的殿充滿炙熱的愛,
辱罵你之人的辱罵都落在我身上。
10我悲傷禁食,
他們就羞辱我。
11我披上麻衣,
他們就譏笑我。
12我成了街談巷議的話題,
醉漢作歌取笑我。
13可是,耶和華啊,
在你悅納人的時候,
我向你禱告。
上帝啊,
求你以你的大愛和信實拯救我。
14求你救我脫離泥沼,
不要讓我沉下去;
求你救我脫離恨我的人,
使我離開深淵。
15求你不要讓洪水淹沒我,
深淵吞滅我,
墳墓吞噬我。
16耶和華啊,求你答應我的禱告,
因為你充滿慈愛和良善;
求你以無限的憐憫眷顧我。
17求你不要掩面不理你的僕人。
我正身陷困境,
求你快快答應我。
18求你前來拯救我,
把我從仇敵手中救贖出來。
19你知道我受的辱罵、欺凌和羞辱,
你看到了我仇敵的所作所為。
20他們的辱罵使我心碎,
令我絕望無助。
我渴望有人同情,卻沒有一個;
期望有人安慰,卻無一人。
21他們給我苦膽當食物,
又拿醋給我解渴。
22願他們面前的宴席變為網羅,
成為他們的陷阱。
23願他們眼目昏暗,無法看見;
願他們哆哆嗦嗦,直不起腰來。
24求你把烈怒傾倒在他們身上,
將怒氣撒向他們。
25願他們的家園一片荒涼,
願他們的帳篷無人居住。
26因為他們迫害你擊打過的人,
嘲笑你所打傷之人的痛苦。
27求你清算他們的種種罪行,
不要讓他們有份於你的拯救之恩。
28願他們的名字從生命冊上被抹去,
不得和義人的名字列在一起。
29上帝啊,
我陷入痛苦和憂傷,
求你拯救我,保護我。
30我要用歌聲讚美上帝的名,
以感恩的心尊崇祂。
31這要比獻上有蹄有角的公牛等祭牲更討耶和華喜悅。
32卑微的人看見這一切就歡喜快樂,
願你們尋求上帝的人精神振奮。
33耶和華垂聽窮苦人的祈求,
不輕看祂被囚的子民。
34願天地都讚美祂,
願海和其中的一切都讚美祂!
35因為上帝必拯救錫安,
重建猶大的城邑。
祂的子民要住在那裡,
擁有那片土地。
36祂僕人的後裔要承受那地方為業,
凡愛祂的人都要住在那裡。