Mithali 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 1:1-33

Utangulizi: Kusudi Na Kiini

11:1 1Fal 4:29-34Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:

2Kwa kupata hekima na nidhamu;

kwa kufahamu maneno ya busara;

31:3 Mit 2:1; 2:1, 9kwa kujipatia nidhamu na busara,

kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;

41:4 Mit 8:5, 12; 2:10-11huwapa busara wajinga,

maarifa na akili kwa vijana;

51:5 Mit 9:9wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,

wenye kupambanua na wapate mwongozo;

61:6 Za 78:2; Mt 13:10-17; Hes 12:8; Amu 14:12kwa kufahamu mithali na mifano,

misemo na vitendawili vya wenye hekima.

71:7 Kut 20:20; Ay 28:28Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa,

lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.

Onyo Dhidi Ya Ushawishi Wa Marafiki Waovu

81:8 Mit 6:20; 22:17; Kum 21:18Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

91:9 Mit 3:21-22; 4:1-9Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako,

na mkufu wa kuipamba shingo yako.

101:10 Mwa 39:7; Ay 24:15; Kum 13:8; Rum 16:18Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi,

usikubaliane nao.

111:11 Mit 12:6; Yer 5:26; Mik 7:2Kama wakisema, “Twende tufuatane;

tukamvizie mtu na kumwaga damu,

njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;

121:12 Ay 33:18; Mwa 38:25; Za 40:3tuwameze wakiwa hai kama kaburi,1:12 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.

13Tutapata aina zote za vitu vya thamani

na kujaza nyumba zetu kwa nyara.

141:14 Mit 1:19Njoo ushirikiane nasi,

vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”

151:15 Za 119:101; Mwa 49:6; Mit 4:14Mwanangu, usiandamane nao.

Usiweke mguu wako katika njia zao,

161:16 Mit 6:18; Isa 59:7kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,

ni wepesi kumwaga damu.

17Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu

wakati ndege wote wanakuona!

181:18 Za 71:10Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe;

hujivizia tu wenyewe!

191:19 Mit 11:19; 15:27; 2Fal 5:20-27Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila;

huuondoa uhai wa wale wenye mali.

Onyo Dhidi Ya Kukataa Hekima

201:20 Ay 28:12; Mt 7:10-13; 9:1-3, 13-15Hekima huita kwa sauti kuu barabarani,

hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;

21kwenye makutano ya barabara za mji

zenye makelele mengi hupaza sauti,

kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:

221:22 Mit 6:32; 7:7; 8:5; 9:4, 16; Za 50:17“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini?

Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha,

na wapumbavu kuchukia maarifa?

231:23 Yoe 2:28; Yn 7:37Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu,

ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu

na kuwafahamisha maneno yangu.

241:24 Isa 65:12; Zek 7:11Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita

na hakuna yeyote aliyekubali

niliponyoosha mkono wangu,

251:25 Lk 7:30kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote

na hamkukubali karipio langu,

261:26 Za 2:4; Kum 28:63; Mit 10:24mimi nami nitawacheka katika maafa yenu,

nitawadhihaki wakati janga litawapata:

271:27 Za 18:18; Mit 5:12-14wakati janga litawapata kama tufani,

wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,

wakati dhiki na taabu zitawalemea.

281:28 Isa 1:15; Mik 3:4; Eze 8:18; Hos 5:6“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu;

watanitafuta lakini hawatanipata.

291:29 Ay 21:14; Isa 27:11; Mdo 7:51Kwa kuwa walichukia maarifa,

wala hawakuchagua kumcha Bwana,

301:30 Ay 21:14; Za 81:11kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu,

na kukataa maonyo yangu,

311:31 2Nya 36:16; Yer 14:16watakula matunda ya njia zao,

na watashibishwa matunda ya hila zao.

321:32 Isa 66:4; Yer 2:19Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua,

nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.

331:33 Hes 24:21; Za 25:12; 112:8Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama,

atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 1:1-33

箴言的價值

1這是大衛的兒子以色列所羅門的箴言。

2為使人認識智慧和教誨,

領悟真知灼見;

3為使人接受勸誡,

為人處事仁義、公平、正直;

4使愚昧人明智,

使青年有知識和明辨力;

5使智者聽了長學問,

明哲聽了得指引;

6使人領悟箴言和比喻,

明白智者的話和謎語。

7知識始於敬畏耶和華,

愚人輕視智慧和教誨。

8孩子啊,

你要聽從父親的教誨,

不可背棄母親的訓言。

9因為這要作你頭上的華冠,

頸上的項鏈。

10孩子啊,惡人若引誘你,

千萬不要聽從。

11他們若說:「跟我們來吧,

我們去埋伏殺人,

暗害無辜者取樂;

12我們要像陰間一樣生吞他們,

整個吞沒他們,

使他們如墜入墳墓的人;

13我們必得到各樣寶物,

把戰利品裝滿我們的房屋。

14跟我們一起幹吧,

大家有福同享!」

15孩子啊,

不要走他們的道,

切莫行他們的路。

16因為他們奔向罪惡,

急速地去殺人流血。

17在飛鳥眼前設網羅,徒勞無功。

18他們埋伏,卻自流己血;

他們伏擊,卻自害己命。

19這就是貪愛不義之財者的結局,

不義之財終要奪去他們的性命。

智慧的勸誡

20智慧在大街上高喊,

在廣場上揚聲,

21在熱鬧的市集宣告,

在城門口演說:

22「你們愚昧人喜愛愚昧,

嘲諷者以嘲弄為樂,

無知者厭惡知識,

要到什麼時候呢?

23你們若因我的責備而回轉,

我就向你們顯明我的旨意1·23 我就向你們顯明我的旨意」希伯來文是「我就將我的靈澆灌你們」。

叫你們明白我的話語。

24我呼喚你們,

你們卻充耳不聞;

我向你們招手,

你們卻視若無睹。

25你們漠視我的勸誡,

不接受我的責備。

26因此,

你們遭遇災難時,

我必發笑;

驚恐臨到你們時,

我必嗤笑——

27那時,恐懼如風暴襲擊你們,

災難如旋風臨到你們,

憂愁和苦難吞沒你們。

28你們呼求我,

我也不回答;

你們懇切地尋找我,

卻找不到。

29因為你們厭惡知識,

不願意敬畏耶和華,

30不接受我的勸誡,

又藐視我的責備。

31所以,你們必自食其果,

因自己的惡謀而吃盡苦頭。

32愚昧人背離正道,

自招滅亡;

愚頑人逍遙自在,

毀掉自己。

33然而,那聽從我的必安然居住,

得享安寧,

不怕災禍。」