Zaburi 35 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 35:1-28

Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

Zaburi ya Daudi.

135:1 1Sam 24:15; Kut 14:14Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

235:2 Za 3:3, 7; Ay 17:3; Mwa 50:24; 35:3; Hes 25:7; Za 27:1; Yos 8:18Chukua ngao na kigao.

Inuka unisaidie.

3Inua mkuki wako na fumo35:3 Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi. lako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Iambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

435:4 Za 38:12; 40:14; 69:6, 19; 70:2; 83:17; 25:3; 129:5; Yer 4:30; Mal 2:9; Isa 45:16Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu.

Wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

535:5 Ay 13:25; Za 1:4; 34:7Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika wa Bwana akiwafukuza.

6Njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika wa Bwana akiwafuatilia.

735:7 Ay 18:8; 9:31; Za 7:4; 7:15; 55:23Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

835:8 Isa 47:11; 1The 5:3; Za 7:15; Mit 5:22maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

935:9 Za 2:11; 9:14; 13:5; 27:1; Lk 1:47; 1Sam 2:1; Isa 61:10; Ebr 3:18Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana

na kuufurahia wokovu wake.

1035:10 Kut 9:14; Za 12:5; 71:19; 18:17, 31; 113:5; 37:14; 86:1; 74:21; 109:16; 140:12; Isa 41:17Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana?

Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”

1135:11 Kut 23:1; Mt 26:60Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza mambo nisiyoyajua.

1235:12 Yer 18:20; Za 38:20; 109:5; Mit 17:13Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

1335:13 2Sam 3:31; 1Fal 20:31; Za 30:11; 69:10, 11; 109:24; Ay 30:25Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

1435:14 Za 38:6; 42:9; 43:2niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama ninayemwombolezea mama yangu.

1535:15 Ay 31:29; 16:10Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

1635:16 Za 22:7; Mk 10:34; 9:18; Ay 16:9; Mdo 7:54Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki,

wamenisagia meno.

1735:17 Za 6:3; 22:20, 21; 57:4; 58:6Ee Bwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

1835:18 Za 22:20, 25; 42:4; 109:30Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

1935:19 Za 9:13; 38:19; 69:4; Yn 15:25; Mit 6:13; 10:10Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

2035:20 Za 38:12; 55:21; Yer 9:8; Mik 6:12Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi

kwa utulivu katika nchi.

2135:21 Ay 16:10; Eze 25:3; Za 40:15; 70:3Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha!

Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

2235:22 Kut 3:7; Za 10:1, 14Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, Ee Bwana.

2335:23 Za 7:6; 80:2; 17:13; 1Sam 24:15Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

2435:24 Za 22:17; 7:8; 26:11; 2The 1:6Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

2535:25 Mit 1:12; Za 35:21; 124:3; Mao 2:16Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

2635:26 Za 22:17; 4:1; 109:29; 38:16; Ay 8:22; 19:5; Mik 7:10Wote wanaofurahia dhiki yangu

waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

wavikwe aibu na dharau.

2735:27 Za 9:4; 20:5; 33:3; 147:11; 149:4; Ay 17:3Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe,

ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”

2835:28 Za 5:8; 51:14; 71:15, 24; 72:15Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 35:1-28

第 35 篇

求上帝申冤

大卫的诗。

1耶和华啊,

求你与我的敌人为敌,

攻击那些攻击我的人。

2求你拿起大小盾牌来帮助我,

3举起矛枪攻击追赶我的人。

求你对我说:

“我是你的拯救。”

4愿谋杀我的人蒙羞受辱,

谋害我的人落荒而逃!

5愿耶和华的天使驱散他们,

如风吹散糠秕!

6愿他们的道路漆黑泥泞,

有耶和华的天使在后追赶!

7因为他们无故设网罗,

挖陷阱要害我。

8愿他们突遭祸患,

作茧自缚,自食恶果!

9我要因耶和华而欢欣,

因祂的拯救而快乐。

10我从心底发出赞叹:

耶和华啊,谁能像你?

你拯救弱者免受欺压,

拯救穷人免遭掠夺。

11恶人诬告我,

盘问我毫无所知的事情。

12他们对我以恶报善,

令我伤心欲绝。

13他们生病时,

我披上麻衣,

谦卑地为他们禁食祷告,

但上帝没有垂听。

14我为他们哀伤,

视他们为朋友、弟兄;

我低头为他们哭泣,

如同哀悼自己的母亲。

15我遭遇患难时,

他们却聚在一起幸灾乐祸,

合伙诽谤我。

素不相识的人也群起攻击我,

不住地毁谤我。

16他们肆无忌惮地嘲弄我,

咬牙切齿地憎恶我。

17耶和华啊,

你袖手旁观要到何时?

求你救我的性命免遭残害,

救我脱离这些狮子。

18我要在大会中称谢你,

在众人面前赞美你。

19求你不要让无故攻击我的人幸灾乐祸,

不要让无故恨我的人沾沾自喜。

20他们言语暴戾,

谋害安分守己的人。

21他们高喊:“哈哈!哈哈!

我们亲眼看见了。”

22耶和华啊,这一切你都看见了,

求你不要再缄默,不要远离我。

23我的上帝,我的主啊,

求你起来为我辩护,为我申冤。

24我的上帝耶和华啊,

求你按你的公义宣告我无罪,

别让他们幸灾乐祸。

25别让他们说:

“哈哈,我们如愿以偿了!”

别让他们说:

“我们除掉他了!”

26愿幸灾乐祸的人蒙羞受辱,

自高自大的人无地自容!

27愿盼望我冤屈得雪的人扬声欢呼!

愿他们常说:“耶和华当受尊崇!

祂乐意赐福给自己的仆人。”

28我要诉说你的公义,

终日赞美你。