Zaburi 132 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 132:1-18

Zaburi 132

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

Wimbo wa kwenda juu.

1Ee Bwana, mkumbuke Daudi

na taabu zote alizozistahimili.

2132:2 Mwa 49:24; Isa 49:26; 60:16Aliapa kiapo kwa Bwana

na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:

3132:3 2Sam 7:2, 27“Sitaingia nyumbani mwangu

au kwenda kitandani mwangu:

4132:4 Rut 3:18sitaruhusu usingizi katika macho yangu,

wala kope zangu kusinzia,

5132:5 1Fal 8:17; Mdo 7:46mpaka nitakapompatia Bwana mahali,

makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

6132:6 1Sam 7:2; 17:12; Yos 9:17; 18:1; 1Nya 13:5Tulisikia habari hii huko Efrathi,

tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:132:6 Yaani Kiriath-Yearimu.

7132:7 2Sam 15:25; Za 5:7; 122:1; 1Nya 28:2“Twendeni kwenye makao yake,

na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;

8132:8 Hes 10:35inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia,

wewe na Sanduku la nguvu zako.

9132:9 Ay 27:6; Zek 3:4; Isa 61:3, 10; Mal 3:3; Ay 29:14Makuhani wako na wavikwe haki,

watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”

10Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,

usimkatae mpakwa mafuta wako.

11132:11 Za 89:3-4, 35; 1Nya 17:11-14; Mt 1:1; Lk 3:31Bwana alimwapia Daudi kiapo,

kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua:

“Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe

katika kiti chako cha enzi,

12132:12 2Nya 6:16; Za 25:10; Lk 1:32; Mdo 2:30kama wanao watashika Agano langu

na sheria ninazowafundisha,

ndipo wana wao watarithi

kiti chako cha enzi milele na milele.”

13132:13 Kut 15:17; Za 48:1, 2; 68:16; 1Fal 18:13Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni,

amepaonea shauku pawe maskani yake:

14132:14 Za 80:1; 68:16; 2Sam 6:2“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele;

hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:

15132:15 Za 107:9; 147:14Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele:

nitashibisha maskini wake kwa chakula.

16132:16 2Nya 6:41; Ay 8:21; Za 149:5Nitawavika makuhani wake wokovu,

nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.

17132:17 1Sam 2:10; Za 18:28; 84:9; 92:10; Eze 29:21; Lk 1:69; 1Fal 11:36; 2Fal 8:19; 2Nya 21:7“Hapa nitamchipushia Daudi pembe,132:17 Pembe inawakilisha nguvu.

na kuweka taa kwa ajili ya masiya132:17 Masiya yaani mpakwa mafuta. wangu.

18132:18 Ay 8:22; 2Sam 12:30Adui zake nitawavika aibu,

bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 132:1-18

第 132 篇

求上帝赐福圣殿

上圣殿朝圣之诗。

1耶和华啊,

求你顾念大卫和他所受的一切苦难。

2他曾向你起誓,

雅各的大能者许愿说:

3-5“我不为耶和华找到居所,

不为雅各的大能者找到安居之处,

必不进家门,

不沾床,不睡觉,不打盹。”

6我们在以法他听到约柜的消息,

基列·耶琳找到了它。

7让我们进入耶和华的居所,

在祂脚前俯伏敬拜。

8耶和华啊,

求你起来和你大能的约柜一同进入圣所。

9愿你的祭司身披公义,

愿你忠心的子民高声欢唱。

10为了你仆人大卫的缘故,

求你不要弃绝你所膏立的人。

11耶和华曾向大卫起了永不废弃的誓说:

“我必使你的后代继承你的王位。

12你的后代若守我的约,

遵行我教导他们的法度,

他们的子孙必永远坐在你的宝座上。”

13因为耶和华已经拣选了锡安

愿意将锡安作为祂的居所。

14祂说:“这是我永远的居所;

我要住在这里,

因为我喜爱这地方。

15我要使她粮食充足,

使她里面的穷人饮食无忧。

16我要用救恩作她祭司的衣裳,

城里忠心的子民必高声欢唱。

17我必使大卫的后裔在那里做王,

我必为我所膏立的预备明灯。

18我必使他的仇敌满面羞愧,

但他头上的王冠必光芒四射。”