Zaburi 109 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 109:1-31

Zaburi 109

Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1109:1 Kut 15:2; Yer 17:14; Ay 34:29; Za 83:1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2109:2 Za 43:1; 52:4kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3109:3 Za 69:4; 35:7; 35:7, 10; Yn 15:25; 1Sam 19:4, 5Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4109:4 Za 69:13; 141:5Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5109:5 Mwa 44:4; Za 38:20Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.

6109:6 1Nya 21:1; Ay 1:6; Zek 3:1Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtaki109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume.

7109:7 Za 1:5; Mit 28:9; Zek 3:1Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8109:8 Ay 15:32; Mdo 1:20Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9109:9 Kut 22:24; Yer 18:21Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10109:10 Mwa 4:12Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11109:11 Hes 14:3; Isa 1:7; 6:11; 36:1; Mao 5:2; Neh 5:3; Ay 20:18; 18:9Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12109:12 Ay 5:4Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13109:13 Za 21:10; 9:5; 37:28; Hes 14:12; Mit 10:7; Ay 18:19Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14109:14 Kut 20:5Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele za Bwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15109:15 Za 90:8; Kut 17:14; Kum 32:26; Ay 18:17Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.

16109:16 Ay 20:19; Za 35:10; 34:18Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17109:17 Mit 28:27; Mt 7:2Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18109:18 Za 10:7; Hes 5:22Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19109:19 Za 109:29; 73:6; Eze 7:27Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20109:20 Kut 32:34; Za 54:5; 94:23; 7:10; Isa 3:11; 2Tim 4:14Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.

21109:21 Kut 9:16; Za 3:7; 23:3; 69:16Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23109:23 Ay 14:2Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24109:24 Ebr 12:12; Ay 16:8; Za 35:13Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25109:25 Za 22:6; Ay 16:4; Mt 27:39; Mk 15:29; Isa 37:22Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.

26109:26 Za 12:1; 119:86Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27109:27 Ay 37:7Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.

28109:28 2Sam 16:12; Za 66:4; Isa 35:10; 51:11; 54:1; 65:14; Hes 22:12Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29109:29 Za 35:26Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.

30109:30 Za 35:18Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31109:31 Za 16:8; 108:6Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

詩篇 109:1-31

第 109 篇

患難中的苦訴

大衛的詩歌,交給樂長。

1我所讚美的上帝啊,

求你不要沉默不語。

2因為邪惡和詭詐的人開口攻擊我,

用謊言譭謗我。

3他們惡言惡語地圍著我,

無緣無故地攻擊我。

4我愛他們,他們卻控告我,

但我為他們禱告。

5他們對我以惡報善,

以恨報愛。

6求你差惡人攻擊我的仇敵,

派人站在他右邊控告他。

7當他受審時,

願他被判為有罪,

他的禱告也算為罪過。

8願他的年日短少,

願別人取代他的職位。

9願他的孩子失去父親,

妻子成為寡婦。

10願他的孩子流浪行乞,

被趕出自己破敗的家。

11願債主奪取他所有的財產,

陌生人搶走他的勞動成果。

12願無人向他施恩,

無人同情他的孤兒。

13願他斷子絕孫,

他的姓氏傳不到下一代。

14願耶和華記住他祖輩的罪惡,

不除去他母親的罪過。

15願耶和華永不忘記他的罪惡,

把他從世上剷除。

16因為他毫無仁慈,

迫害困苦、貧窮和傷心的人,

置他們於死地。

17他喜歡咒詛人,

願咒詛臨到他;

他不喜歡祝福人,

願祝福遠離他。

18他咒詛成性,

願咒詛如水侵入他的身體,

如油浸透他的骨頭。

19願咒詛不離其身,

如同身上的衣服和腰間的帶子。

20願耶和華這樣報應那些誣告我,

以惡言攻擊我的人。

21主耶和華啊,

求你因自己的名恩待我,

因你的美善和慈愛拯救我。

22因為我貧窮困苦,

內心飽受創傷。

23我像黃昏的日影一樣消逝,

如蝗蟲一般被抖落。

24禁食使我雙腿發軟,

瘦骨嶙峋。

25仇敵都嘲笑我,

他們看見我就連連搖頭。

26我的上帝耶和華啊,

求你幫助我,施慈愛拯救我,

27讓他們都看見這是你耶和華的作為。

28任憑他們咒詛吧,

你必賜福給我。

攻擊我的人必蒙羞,

你的僕人必歡喜。

29願誣告我的人滿面羞辱,

無地自容。

30我要竭力頌揚耶和華,

在眾人面前讚美祂。

31因為祂保護貧窮的人,

拯救他們脫離置他們於死地的人。