Zaburi 105 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 105:1-45

Zaburi 105

Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli

(1 Nyakati 16:8-22)

1105:1 1Nya 16:34; Za 80:18; 99:6; 116:13; Yoe 2:32; Mdo 2:21; Isa 12:4Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake,

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

2105:2 Za 30:4; 146:2; 33:3; 96:1; 7:17; 18:49; 27:6; 59:17; 71:22; 75:1Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

3105:3 Za 89:16Lishangilieni jina lake takatifu,

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

4105:4 Za 24:6; 27:8Mtafuteni Bwana na nguvu zake,

utafuteni uso wake siku zote.

5105:5 Za 40:5; Kum 7:18; 8:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

6105:6 Za 105:42; Kum 10:15; Za 106:5enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

7105:7 Isa 26:8Yeye ndiye Bwana Mungu wetu,

hukumu zake zimo duniani pote.

8105:8 Mwa 9:15; Za 106:45; 111:5; Eze 16:60; Lk 1:72Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

9105:9 Mwa 22:16-18; 15:18; Ebr 6:17; Lk 1:73; 17:2; 12:7; Gal 3:15-18; Dan 9:4agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

10105:10 Mwa 28:13-15; Isa 55:3Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

11105:11 Mwa 12:7; Hes 34:2“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

12105:12 Kum 7:7; Ebr 11:9; Mwa 17:8; 23:4; 34:30Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

13105:13 Mwa 15:13-16; Hes 32:13; 33:3-49walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

14105:14 Mwa 35:5; 12:17-20; 20:3; Za 9:5Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

15105:15 Mwa 26:11; 20:7; 1Sam 12:3“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

16105:16 Isa 3:1; Law 26:26; Mwa 12:10; 41:54; 2Fal 8:1; Eze 4:16Akaiita njaa juu ya nchi

na kuharibu chakula chao chote,

17105:17 Mwa 45:5; 37:28; Mdo 7:9naye akatuma mtu mbele yao,

Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.

18105:18 Mwa 40:15Walichubua miguu yake kwa minyororo,

shingo yake ilifungwa kwa chuma,

19105:19 Mwa 12:10; 41:40; 40:20-21hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia,

hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.

20105:20 Mwa 41:14Mfalme alituma watu wakamfungua,

mtawala wa watu alimwachia huru.

21Alimfanya mkuu wa nyumba yake,

mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,

22105:22 Mwa 41:43-44; 41:40kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo

na kuwafundisha wazee wake hekima.

23105:23 Mdo 7:15; 13:17; Mwa 46:6; 47:28; Za 78:51Kisha Israeli akaingia Misri,

Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.

24105:24 Kut 1:7; Kum 26:7; Mdo 7:17Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana,

akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,

25105:25 Kut 4:21; 1:6-10; Mdo 7:19ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,

wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.

26105:26 Kut 3:10; 4:16; Hes 33:1; 16:5; 17:5-8Akamtuma Mose mtumishi wake,

pamoja na Aroni, aliyemchagua.

27105:27 Za 105:28-37; Kut 7:8; 12:51; 4:17; 10:1; 3:20; Dan 4:3Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,

miujiza yake katika nchi ya Hamu.

28105:28 Mwa 1:4; Za 99:7; Kut 10:22; 7:22Alituma giza na nchi ikajaa giza,

kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?

29105:29 Za 78:44; Kut 7:21Aligeuza maji yao kuwa damu,

ikasababisha samaki wao kufa.

30105:30 Kut 8:2, 6Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia

hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.

31105:31 Za 78:45; 107:25; 148:8; Kut 8:16-18; 8:21-24Alisema, yakaja makundi ya mainzi,

na viroboto katika nchi yao yote.

32105:32 Kut 9:22-25; Ay 38:22; Za 78:47Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,

yenye umeme wa radi nchini yao yote,

33105:33 Za 78:47; Kut 10:5, 12akaharibu mizabibu yao na miti ya tini,

na akaangamiza miti ya nchi yao.

34105:34 Za 107:25; Kut 10:4, 12-15; 1Fal 8:27; Yoe 1:6Alisema, nzige wakaja,

tunutu wasio na idadi,

35wakala kila jani katika nchi yao,

wakala mazao ya ardhi yao.

36105:36 Kut 4:23; 12:12Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao,

matunda ya kwanza ya ujana wao wote.

37105:37 Kut 3:21, 22Akawatoa Israeli katika nchi

wakiwa na fedha na dhahabu nyingi,

wala hakuna hata mmoja

kutoka kabila zao aliyejikwaa.

38105:38 Kut 15:16Misri ilifurahi walipoondoka,

kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.

39105:39 Kut 13:21; 1Kor 10:1; Za 78:14; Neh 9:12Alitandaza wingu kama kifuniko,

na moto kuwamulikia usiku.

40105:40 Za 78:18; Kut 16:4; Yn 6:31; Kut 16:12Waliomba, naye akawaletea kware,

akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.

41105:41 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17:6; Neh 9:15; Isa 48:21Alipasua mwamba, maji yakabubujika,

yakatiririka jangwani kama mto.

42105:42 Mwa 15:1-4, 13-16; 13:14-17Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,

aliyompa Abrahamu mtumishi wake.

43105:43 Kut 15:1-19; Za 106:12Aliwatoa watu wake kwa furaha,

wateule wake kwa kelele za shangwe,

44105:44 Kum 6:10-11; Za 106:12akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi

wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:

45105:45 Kum 6:14-21; 4:1, 40; Za 105:35; 78:5-7alifanya haya ili wayashike mausia yake

na kuzitii sheria zake.

Msifuni Bwana.105:45 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Japanese Contemporary Bible

詩篇 105:1-45

105

1主のなさるすばらしいことの一つ一つに感謝し、

諸国の民に伝えなさい。

2賛美の歌を歌い、

会う人ごとにその奇跡を告げ知らせなさい。

3主を拝む人々は、その名を誇り、喜びなさい。

4常に主を求め、御力を慕い続けなさい。

5-6主がどれほど大きいことをしてくださったか、

考えてみなさい。

それは、私たちが主のしもべアブラハムと

ヤコブの子孫であり、選ばれた民だからです。

さあ、どのようにして敵を滅ぼしていただいたか、

思い起こしなさい。

7私たちの神の恵みは、国中の至る所で明らかです。

8-9たとえ、何千年を経たのちでも、

主は約束を忘れず、

アブラハムやイサクと結んだ契約を

守られます。

10-11そして、この契約をヤコブに再確認されました。

「カナンの地を相続させよう」という、

イスラエルへの約束です。

12このころはまだ、

イスラエルはほんの一にぎりの民族で、

カナンの寄留民にすぎませんでした。

13彼らは国々に散らされ、

国から国へと放浪したこともありました。

14しかし、そんな時でも、主の許しなしには、

だれも彼らを攻撃することはできなかったのです。

彼らを攻撃しようとする多くの王が滅ぼされました。

15神の警告が響き渡りました。

「わたしの選んだ者にさわるな。

わたしの預言者に害を加えるな。」

16主がカナンの地にききんを呼び寄せられると、

食糧が底をつきました。

17一方、ご自分の民を飢えから救うため、

ヨセフを奴隷としてエジプトに送られました。

18ところがヨセフは牢獄につながれ、

足かせや鉄の首輪をかけられたのです。

19神の時がくるまで、

ヨセフは忍耐を試されました。

20彼はついに、王によって自由の身とされ、

21王室の全財産の管理を任されました。

22ヨセフは、思いどおりに王の補佐官を投獄したり、

側近を教育したりできる身分となったのです。

23そののち、ヤコブもエジプトを訪れて、

息子たちとともに住みつくことになりました。

24それ以後、イスラエルの民は増え、

支配者たちを脅かす大民族とまでなったのです。

25このころ神は、

エジプト人をイスラエルの敵と変え、

イスラエルは奴隷にされました。

26しかし、主はご自分の代理として、

モーセをアロンとともに派遣なさいました。

27エジプトに、恐ろしいみわざを行うためです。

28主からの指図を受けて、

この二人は国中を暗闇で覆い、

29あの大河を血に変え、

魚を死滅させました。

30また、おびただしいかえるが現れ、

王の部屋に侵入しました。

31モーセのひと言で、

あぶやぶよが、雲が立ちこめるように、

エジプト全土を覆いました。

32主は、雨の代わりに、

人の頭を打ち砕く雹をお降らせになりました。

また、いなずまの先に、

エジプトの民は震え上がりました。

33ぶどうといちじくの木は全滅し、

木という木の幹は、ことごとく裂けたのです。

34また、主のひと声で、いなごの大群が襲来し、

35青いものを跡形なく食い尽くし、

穀物をすべて食い荒らしました。

36続いて、主は

エジプト人の全家庭の長男を、

その家の誇りである長男を打たれました。

37一方、ご自分の民には、

銀と金をふんだんに持たせて、

エジプトを脱出させてくださいました。

その時、一行の中からは、

体の弱い者や病人は一人も出ませんでした。

38エジプトは彼らを

非常に恐れるようになっていたので、

彼らが出て行くことを喜びました。

39主は雲の幕を広げて、

彼らを焼けつく日ざしから守り、

夜には火の柱を立てて、明かりとされました。

40人々が肉を欲しがると、空からうずらを降らせ、

天からパンであるマナを

お与えになりました。

41主が岩を裂かれると、水がほとばしり出て、

乾いた地を潤す川となりました。

42主は、しもべアブラハムへの約束を

覚えておられたのです。

43こうして、選ばれた民イスラエルは、

意気揚々と約束の地に入りました。

44主が、麦の穂の波打つ他民族の地を

与えてくださったので、

彼らは他人が育てた穀物を食べました。

45これは、かれらが主のおきてを

忠実に守るようになるためでした。

ハレルヤ。