Yohana 15 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 15:1-27

Yesu Mzabibu Wa Kweli

115:1 Za 80:8-11“Mimi ndimi mzabibu wa kweli na Baba yangu ndiye mkulima. 215:2 Mt 3:10; Za 92:14; Mt 3:8; 7:20; Gal 5:22; Efe 5:9; Flp 1:11; Yn 16:6Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, Baba yangu hulikata, nalo kila tawi lizaalo, hulisafisha ili lipate kuzaa matunda zaidi. 315:3 Yn 17:17; Efe 5:26Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililonena nanyi. 415:4 Yn 6:56; 2:6Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda lisipokaa ndani ya mzabibu, vivyo hivyo ninyi msipokaa ndani yangu hamwezi kuzaa matunda.

515:5 1Kor 12:12, 27; 2Kor 3:5“Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana, maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya jambo lolote. 615:6 Mt 3:10; 13:40; Eze 15:4; Yn 15:2Mtu yeyote asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka. Matawi kama hayo hukusanywa na kutupwa motoni, yakateketea. 715:7 Mk 11:24; Yn 6:56; Mt 7:7Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lolote mtakalo, nanyi mtatendewa. 815:8 Mt 5:16; Yn 8:31Kwa hiyo Baba yangu hutukuzwa, kwa vile mzaavyo matunda mengi, nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.

915:9 Yn 17:23, 24, 26“Kama vile Baba alivyonipenda mimi, hivyo ndivyo mimi nilivyowapenda ninyi. Basi kaeni katika pendo langu. 1015:10 Yn 14:15Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. 1115:11 Yn 3:29Nimewaambia mambo haya ili furaha yangu iwe ndani yenu na furaha yenu iwe kamili. 1215:12 Yn 13:34; 1Yn 3:11; Mk 12:30Amri yangu ndiyo hii: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi. 1315:13 Mwa 44:33; Rum 5:7, 8Hakuna mtu mwenye upendo mkuu kuliko huu, mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. 1415:14 Mit 18:24; Mt 12:50Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru. 1515:15 Yn 8:26Siwaiti ninyi watumishi tena, kwa sababu watumishi hawajui bwana wao analofanya, bali nimewaita ninyi rafiki, kwa maana nimewajulisha mambo yote niliyoyasikia kutoka kwa Baba yangu. 1615:16 Yn 6:70; 13:18Si ninyi mlionichagua, bali mimi ndiye niliyewachagua ninyi na kuwaweka mwende mkazae matunda, na matunda yenu yapate kudumu. Ili nalo lolote mtakalomwomba Baba katika Jina langu, awape ninyi. 1715:17 Yn 15:12Amri yangu ndiyo hii: Mpendane.

Ulimwengu Wawachukia Wanafunzi

1815:18 Isa 66:5“Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba ulinichukia mimi kabla yenu. 1915:19 Yn 15:16; 17:14Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungeliwapenda kama vile unavyowapenda walio wake. Kwa sababu ninyi si wa ulimwengu, lakini mimi nimewachagua kutoka ulimwengu, hii ndiyo sababu ulimwengu unawachukia. 2015:20 Yn 13:16; 2Tim 3:12Kumbukeni lile neno nililowaambia, ‘Hakuna mtumishi aliye mkuu kuliko bwana wake.’ Kama wamenitesa mimi, nanyi pia watawatesa. Kama wamelishika neno langu, watalishika na neno lenu pia. 2115:21 Isa 66:5; Yn 16:3Watawatendea ninyi haya yote kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma. 2215:22 Rum 1:20; 2:1Kama sikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa hawana udhuru kwa ajili ya dhambi zao. 2315:23 1Yn 2:23Yeyote anayenichukia mimi, anamchukia pia na Baba yangu. 2415:24 Yn 5:36Kama sikuwa nimefanya miujiza ambayo haijapata kufanywa na mtu mwingine yeyote, wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa wameiona miujiza hii na bado wakatuchukia mimi na Baba yangu. 2515:25 Za 69:4; 109:3Lakini hii ni kutimiza lile neno lililoandikwa kwenye Sheria kwamba, ‘Walinichukia pasipo sababu.’

2615:26 Yn 14:15; 16:7; 14:17; 1Yn 4:4“Lakini atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, yaani, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi. 2715:27 Lk 24:48; 1:21; 1Yn 4:14Ninyi nanyi itawapasa kushuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.

King James Version

John 15:1-27

1I am the true vine, and my Father is the husbandman. 2Every branch in me that beareth not fruit he taketh away: and every branch that beareth fruit, he purgeth it, that it may bring forth more fruit. 3Now ye are clean through the word which I have spoken unto you. 4Abide in me, and I in you. As the branch cannot bear fruit of itself, except it abide in the vine; no more can ye, except ye abide in me. 5I am the vine, ye are the branches: He that abideth in me, and I in him, the same bringeth forth much fruit: for without me ye can do nothing. 6If a man abide not in me, he is cast forth as a branch, and is withered; and men gather them, and cast them into the fire, and they are burned. 7If ye abide in me, and my words abide in you, ye shall ask what ye will, and it shall be done unto you. 8Herein is my Father glorified, that ye bear much fruit; so shall ye be my disciples. 9As the Father hath loved me, so have I loved you: continue ye in my love. 10If ye keep my commandments, ye shall abide in my love; even as I have kept my Father’s commandments, and abide in his love. 11These things have I spoken unto you, that my joy might remain in you, and that your joy might be full. 12This is my commandment, That ye love one another, as I have loved you. 13Greater love hath no man than this, that a man lay down his life for his friends. 14Ye are my friends, if ye do whatsoever I command you. 15Henceforth I call you not servants; for the servant knoweth not what his lord doeth: but I have called you friends; for all things that I have heard of my Father I have made known unto you. 16Ye have not chosen me, but I have chosen you, and ordained you, that ye should go and bring forth fruit, and that your fruit should remain: that whatsoever ye shall ask of the Father in my name, he may give it you. 17These things I command you, that ye love one another. 18If the world hate you, ye know that it hated me before it hated you. 19If ye were of the world, the world would love his own: but because ye are not of the world, but I have chosen you out of the world, therefore the world hateth you. 20Remember the word that I said unto you, The servant is not greater than his lord. If they have persecuted me, they will also persecute you; if they have kept my saying, they will keep yours also. 21But all these things will they do unto you for my name’s sake, because they know not him that sent me. 22If I had not come and spoken unto them, they had not had sin: but now they have no cloke for their sin. 23He that hateth me hateth my Father also. 24If I had not done among them the works which none other man did, they had not had sin: but now have they both seen and hated both me and my Father. 25But this cometh to pass, that the word might be fulfilled that is written in their law, They hated me without a cause. 26But when the Comforter is come, whom I will send unto you from the Father, even the Spirit of truth, which proceedeth from the Father, he shall testify of me: 27And ye also shall bear witness, because ye have been with me from the beginning.