Yeremia 51 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 51:1-64

151:1 Isa 41:16; Mt 3:12; Yer 50:14; Isa 13:5-951:1 Yer 46:4; Isa 41:25; Yer 50:28, 45; Isa 13:3; Yer 50:9; Isa 21:5; 41:2Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.51:1 Leb-Kamai ni Ukaldayo, yaani Babeli, kwa fumbo.

2Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

351:3 Yer 50:29; 46:4Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

451:4 Isa 13:15-18; Yer 50:30Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.

551:5 Law 26:44; Isa 54:6-8; Za 91:14; Hos 4:1Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

651:6 Ufu 18:4; Isa 48:20; Yer 50:8, 15; Ay 21:19; Isa 1:24; Mao 3:64; Hes 16:26“Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi cha Bwana,

atamlipa kile anachostahili.

751:7 Isa 51:22; Ufu 17:4; Yer 25:15-16; 49:12; Ufu 14:8-10Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

851:8 Isa 14:15; Ufu 14:8; Yer 8:22; Ufu 18:9; Yer 46:11; Isa 21:9Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

951:9 Isa 13:14; 31:9; Ufu 18:4-5; Yer 50:16“ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu hadi mawinguni.’

1051:10 Mik 7:8-9; Za 64:9; Yer 50:28“ ‘Bwana amethibitisha haki yetu;

njooni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’

11“Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwana atalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

1251:12 Za 20:5; 2Sam 18:24; Eze 33:2Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwana atatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

1351:13 Yer 50:38; Ufu 17:15; Eze 22:27; Hab 2:9; Isa 45:3Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

1451:14 Mwa 22:16; Amo 6:8; Nah 3:15; Yer 50:15Bwana Mwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

1551:15 Ay 9:8; Isa 40:26; Mdo 14:15; Za 104:24; 136:5“Aliiumba dunia kwa uweza wake;

akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

1651:16 Za 18:11-13; Kum 28:12; Yn 1:12; Ay 28:26; Za 135:7Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua,

naye huuleta upepo kutoka ghala zake.

1751:17 Isa 44:20; Hab 2:18-19; Yer 50:2“Kila mtu ni mjinga na hana maarifa;

kila sonara ameaibishwa na sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yavyo.

1851:18 Yer 18; 15; Yn 2:8Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.

1951:19 Za 119:57; Kut 34:9Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwani ndiye Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

2051:20 Isa 10:5; Zek 9:13; Mik 4:13; Ay 34:24; Isa 45:1“Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita:

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

2151:21 Kut 15:1; Isa 43:17; Yer 50:37kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

2251:22 2Nya 36:17; Isa 13:17-18kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

2451:24 Kum 32:41; Mao 3:64; Yer 50:15; Isa 45:1“Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.

2551:25 Yer 21:13; 50:23; Kut 3:20; Zek 4:7“Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asema Bwana.

“Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

2651:26 Isa 13:19-22; Yer 50:12Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asema Bwana.

2751:27 Isa 13:2; Za 20:5; Mwa 8:4; 10:3; Yer 25:14“Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

2951:29 Isa 13:20; Yer 50:13; Amu 5:4; Yer 49:21; Za 33:11; Yer 48:9Nchi inatetemeka na kugaagaa,

kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.

3051:30 Yer 50:24; 2Sam 19:16; Mao 2:9; Nah 3:13; Isa 47:14; 45:2Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

3151:31 Yer 50:24; 2Sam 18:19-31; Dan 5:30Tarishi mmoja humfuata mwingine,

na mjumbe humfuata mjumbe,

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

3251:32 Isa 47:14; Yer 50:36Vivuko vya mito vimekamatwa,

mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

3351:33 Isa 21:10; 17:5; Hos 6:11; Mt 13:30; Isa 13:22Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

3451:34 Yer 50:17; Nah 2:12; Hos 8:8“Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35Jeuri iliyofanyiwa miili yetu51:35 Au: Jeuri tuliyofanyiwa sisi na watoto wetu. na iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

3651:36 Za 140:12; Mao 3:58; Yer 20:12; Rum 12:19; Hos 13:15; Yer 50:34; Isa 11:15Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

3751:37 Isa 13:22; Ufu 12:8; Yer 50:39; 18:16; Ufu 18:2; Nah 3:6; Mal 2:9Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

3951:39 Isa 21:5; Yer 50:24; Za 13:3Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asema Bwana.

40“Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

4151:41 Yer 25:26; Isa 13:19; Dan 4:30; Yer 50:13“Tazama jinsi Sheshaki51:41 Sheshaki ni Babeli kwa fumbo. atakamatwa,

majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

4251:42 Za 18:4; Isa 8:7-8Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

4351:43 Isa 13:20; Yer 2:6; Isa 21:1Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

4451:44 Isa 21:9; 2Fal 25:4; Isa 25:12; 46:1; Yer 50:15Nitamwadhibu Beli katika Babeli,

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

4551:45 Ufu 18:4; Yer 50:8; Isa 48:20; Za 76:10; 79:6“Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali ya Bwana.

4651:46 Yer 46:27; 2Fal 19:7; Za 18:45Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi,

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

4751:47 Isa 46:1-2; Yer 50:12; 27:7; 50:12Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu,

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

4851:48 Isa 44:23; Ufu 18:20; Yer 25:26; Isa 41:25; Za 149:2; Ay 3:7Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asema Bwana.

4951:49 Za 137:8; Yer 50:29“Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

5151:51 Za 44:13-16; 79:4; Mao 1:10“Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”

5251:52 Ay 24:12“Lakini siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

5351:53 Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Ay 15:21; Yer 49:16Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asema Bwana.

54“Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

5551:55 Za 18:4; Isa 25:5Bwana ataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

5651:56 Ay 15:21; Mwa 4:24; Za 46:9; Hab 2:8; Za 94:1-2Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

5751:57 Za 76:5; Yer 25:27; Isa 6:5; Yer 46:18; Ay 5:13; Isa 21:7Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.

5851:58 2Fal 25:4; Isa 15:4; 47:14; Hab 2:13; Isa 13:2Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”

5951:59 Yer 36:4; 52:1; 28:1Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 6051:60 Kut 17:14; Yer 30:2; 36:2Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli. 61Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa. 6251:62 Isa 13:20; Yer 9:11; 50:13Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’ 6351:63 Mwa 2:14Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati. 6451:64 Ay 31:40; Za 18:21; Eze 26:21; 28:19Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

Japanese Contemporary Bible

エレミヤ書 51:1-64

51

1神はこう言います。

「わたしは、カルデヤ人の住むバビロンを

隅々まで滅ぼす者たちを、勇気づける。

2ふるい分ける者たちが来て、

バビロンをふるいにかけ、風を起こして吹き飛ばす。

彼らは、災いの日に四方八方から来て、攻め立てる。

3敵の矢はバビロンの射手を倒し、勇士のよろいを貫く。

生き延びる者は一人もいない。

若者も老人もみな、いのちを落とす。

4カルデヤ人の地に倒れ、

めった切りにされて路上で息絶える。

5わたしは、イスラエルとユダを見捨てたわけではなく、

依然として彼らの神である。

だがカルデヤ人の地は、

イスラエルのきよい神に対する罪で満ちている。」

6バビロンから逃げ出し、自分のいのちを救いなさい。

罠にかかってはいけません。

そのまま残ったら、神がバビロンのすべての罪に

報復する時、巻き添えを食います。

7バビロンは、主の御手にある金の杯のようでした。

すべての国々はこれから飲んで、酔いつぶれました。

8ところが今度は、突然、そのバビロンが倒れたのです。

この国のために泣きなさい。薬を与えなさい。

もしかしたら、元どおりになるかもしれません。

9できることなら助けたいのです。

しかし今となっては、どんな手を打っても救えません。

この国を見捨てて、故国へ帰りなさい。

主がこの国に天罰を下したからです。

10主は私たちの顔を立ててくださいました。

さあ、エルサレムで、

神のなさったすべてのことを言い広めましょう。

11矢じりを研ぎ、盾を高く掲げなさい。

主はメディヤ人の王たちを勇気づけて

バビロンに乗り込ませ、

これを滅ぼすことに決めたからです。

これが、神の民を虐待し、

神殿を汚した者たちへの報復です。

12バビロンよ、守備を固め、城壁に見張りを大ぜい立て、

伏兵を隠しておきなさい。

神は宣言したことをみな実行するからです。

13商業の中心地である繁栄した港よ。

いのちの糸が切られる最期の時がきました。

14天の軍勢の主はご自分の名にかけて、こう誓いました。

おまえの町々は、無数のばったが群がる畑のように、

敵兵であふれ返る。

彼らは、天にも届けとばかり、勝ちどきを上げる。

15神は力と知恵をもって地をお造りになりました。

すぐれた知性をもって天を張り広げました。

16神が口を開くと大空に雷がとどろき渡ります。

神は大地から水蒸気を上らせ、ご自分の倉から、

雨と風を伴ういなずまを取り出します。

17神に比べたら、人間は愚かな獣で、

一かけらの知恵もありません。

金細工人は偶像を作るたびに、

ますます良心が鈍くなります。

偶像には、いのちのしるしである息がないのに、

それを作るたびに神ができたと言って、

うそをつくからです。

18偶像は、むなしいものです。

神が来てそれをみな滅ぼす時が近づいています。

19イスラエルの神は偶像ではありません。

この神があらゆるものを造り、

イスラエルをご自分の民としました。

その名は天の軍勢の主です。

20バビロンは神のための戦いの斧であり、また剣です。

主は言います。

「わたしは国々を木端微塵に砕き、

多くの王国を滅ぼすためにおまえを用いる。

21おまえを使って軍勢を蹴散らし、馬と乗り手を倒し、

戦車とそれに乗っている者を打ち砕く。

22おまえを使って、年老いた者も若者も、

若い男も若い女も、

23羊飼いも羊の群れも、農夫も牛も、

指揮官も総督も倒す。

24わたしはイスラエルの目の前で、

バビロンとカルデヤ人に報いる。

彼らがわたしの民に加えたすべての悪に

仕返しするのだ。

25全世界を破壊する大きな山、バビロンよ。

わたしはおまえを攻める。

おまえにこぶしを振り上げ、高い所から突き落とし、

おまえを焼けただれた山にする。

26おまえは永久に荒れ地となり、

おまえの石さえも、建築用として再生されることはない。

おまえは地上から完全に一掃されるのだ。」

27多くの国々に合図して、

バビロンを攻める兵士を集めなさい。

雄たけびをあたりに響かせなさい。

アララテ、ミニ、アシュケナズの軍隊を呼びなさい。

指揮官を決め、長蛇の列をなして馬を進めなさい。

28バビロンめざして、メディヤ人の王たちと将軍たち、

その支配下の国々の軍隊を攻め上らせなさい。

29バビロンは震え、苦痛で身もだえします。

主がこの国について計画したことはみな、

少しも変更されないからです。

バビロンは、だれも住まない荒れ地となります。

30大勇士でも、戦う気力を失い、

仮小屋に引きこもります。

力が尽きて、女のようになるのです。

侵略者たちは家々を焼き、町の門を壊しました。

31伝令が四方八方から王のもとへ駆けつけ、

何もかも失われたと報告します。

32退路はすべて断たれ、とりでは焼き払われ、

兵士たちは大混乱に陥っています。

33イスラエルの神である天の軍勢の主が、

こう言ったからです。

「バビロンは打ち場に積まれた麦のようだ。

もうすぐ、からざおで打たれる。」

34-35バビロンのユダヤ人たちは訴えます。

「バビロンのネブカデネザル王は、私たちを食い物にし、

踏みつけ、骨なしにしました。

怪物のように私たちをのみ込み、

私たちの財宝で腹を満たし、

私たちをイスラエルから追放しました。

バビロンに、このすべての悪事の報いを刈り取らせ、

その手で流した私たちの血を完全に償わせてください。」

36それに対して、主はこうお答えになります。

「わたしはおまえたちを弁護する者となり、

おまえたちのために報復する。

バビロンの川を干上がらせ、水の補給を断つ。

37こうしてバビロンは、石くれの山となり、

山犬が住みつき、だれもいない見るも恐ろしい地となる。

38バビロニヤ人は宴会を開いて、

ライオンのようにほえる。

39彼らがありったけのぶどう酒を飲んで

気持ちが大きくなっている時、

わたしは彼らのために別の宴会を設け、

彼らが意識を失って倒れ、

永遠の眠りにつくまで飲ませる。

40彼らを子羊のように、また雄羊や雄やぎのように、

ほふり場に引いて行く。

41全世界の人のあこがれの的だった、

あの偉大なバビロンは、なぜ倒れたのか。

世界は、バビロンが倒れるのを見て、目を疑う。

42海がせり上がってバビロンを包むと、

それは波に覆われた。

43町々は廃墟となった。

バビロンは、誰ひとり住まず、旅人さえ寄りつかない、

乾ききった荒れ地となる。

44わたしはバビロンの神であるベルを罰し、

その口から、彼がのみ込んだ物を取り出す。

諸国の民は二度と彼を拝まない。

バビロンの城壁は倒れてしまった。

45わたしの民よ、バビロンを脱出し、

わたしの激しい怒りから自分を救いなさい。

46外国の軍隊が近づいて来るといううわさを聞いても、うろたえてはならない。うわさは、いつになっても絶えないものだ。だが、この国に内戦が起こり、各州の総督が互いに戦う時がくる。 47わたしがこの大都市とこの国のすべての偶像を罰する時が、きっとくる。そうなれば、町中に死人が転がるようになる。 48バビロンを攻める強力な軍勢が北から来るので、天も地も喜ぶ。」そう主は言います。 49かつてイスラエルの民を殺したように、今度はバビロンが殺される番です。 50剣から逃れた者は、立ち止まって、あたりの様子を見ていてはいけません。力の限り逃げなさい。主を思い出して、はるかかなたのエルサレムへ帰って行きなさい。 51「バビロンから来た外国人たちの手で神殿が汚されたので、私たちはとても恥ずかしい思いをしました。」

52「そのとおりだ」と、主は言います。しかし、バビロンの偶像が壊される時が近づいています。国中に、傷ついた人のうめき声が聞こえます。 53「たとえ、バビロンが天のように高くなり、その力が信じられないほど増し加わったとしても、必ず死ぬ」と、主は言います。 54カルデヤ人の支配する地、バビロンに上がる大きな破壊の叫びを聞きなさい。 55主はバビロンの息の根を止めます。その大きな声も、やがては大波にのまれて消えます。 56すべてのものを破壊する軍勢が攻めて来て、勇士たちを滅ぼします。武器という武器はどれも、まるで役に立ちません。神がバビロンに与えるものは、当然の刑罰だけです。 57「わたしは、この国の重立った者、知恵のある者、支配者、指揮官、それに勇士たちを酔いつぶす。彼らは深い眠りに落ち、二度と目を覚まさない。」こう天の軍勢の主である王が言います。

58バビロンの厚い城壁はくずれて平らになり、

高い城門も無残に焼け落ちます。

多くの国から呼び集められた建築士は、

造った物が火で焼かれるため、

むだ骨を折ったことに気づきます。

59ゼデキヤ王の治世の第四年に、エレミヤを通して、次のことばがマフセヤの子のネリヤの子セラヤにありました。それは、宿営長セラヤがユダのゼデキヤ王と共に捕まり、バビロンへ流される、というものでした。 60エレミヤは、先に書いたような、神がバビロンに下そうとしているすべての災害を巻物に書き留め、 61-62その巻物をセラヤに渡して言いました。「バビロンに着いたら、私の書いたことを読み、次のように言いなさい。『主よ。あなたはバビロンを滅ぼし、そこを猫の子一匹いない、永遠に見捨てられた所にする、と語りました。』 63-64読み終えたら、石を結びつけてユーフラテス川に投げ込み、こう言いなさい。『このように、バビロンは沈み、二度と浮かび上がらない。わたしがこの国に災いを招くからだ。』」

これで、エレミヤのことばは終わります。