Yeremia 5 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 5:1-31

Hakuna Hata Mmoja Aliye Mkamilifu

15:1 Eze 22:30; Mwa 18:24; Mik 7:2; Yer 2:29; 2Nya 16:9; Za 45:10“Pandeni na kushuka katika mitaa ya Yerusalemu,

tazameni pande zote na mtafakari,

tafuteni katika viwanja vyake.

Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja tu

atendaye kwa uaminifu na kutafuta kweli,

nitausamehe mji huu.

25:2 Tit 1:16; Yer 4:2; Law 19:12Ingawa wanasema, ‘Kwa hakika kama Bwana aishivyo,’

bado wanaapa kwa uongo.”

35:3 2Nya 16:9; Yer 7:28; Isa 9:13; Sef 3:2; Zek 7:2; Eze 36:26; 3:8-9; Amo 4:6Ee Bwana, je, macho yako hayaitafuti kweli?

Uliwapiga, lakini hawakusikia maumivu,

uliwapondaponda, lakini walikataa maonyo.

Walifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko jiwe

nao walikataa kutubu.

45:4 Yer 8:7; Mit 10:21; Yer 4:22Ndipo nikasema, “Hawa ni maskini tu;

wao ni wapumbavu,

kwa maana hawaijui njia ya Bwana,

sheria ya Mungu wao.

55:5 Mik 3:1, 9; Za 2:3; Yer 2:20Kwa hiyo nitakwenda kwa viongozi

na kuzungumza nao,

hakika wao wanaijua njia ya Bwana,

sheria ya Mungu wao.”

Lakini kwa nia moja nao pia walikuwa wameivunja nira

na kuvivunja vifungo.

65:6 Hos 13:7; Yer 4:7; 30:14; Za 7:12; Law 26:22Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawashambulia,

mbwa mwitu kutoka jangwani atawaangamiza,

chui atawavizia karibu na miji yao,

ili kumrarua vipande vipande yeyote atakayethubutu kutoka nje,

kwa maana maasi yao ni makubwa,

na kukengeuka kwao kumekuwa ni kwingi.

75:7 Yos 23:7; Yer 12:16; Gal 4:8; Amo 8:14; Kum 32:21; Hes 25:1; Yer 2:11; 13:27“Kwa nini niwasamehe?

Watoto wenu wameniacha na kuapa kwa miungu ambayo si miungu.

Niliwapatia mahitaji yao yote,

lakini bado wamefanya uzinzi na kusongana katika nyumba za makahaba.

85:8 Eze 22:11; 2Sam 11:2-4; Eze 33:26; Yer 29:23Wamelishwa vizuri, kama farasi waume wenye tamaa nyingi,

kila mmoja akimlilia mke wa mwanaume mwingine.

95:9 Yer 44:22; Eze 7:9; Isa 1:24; 57:6Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya hili?”

asema Bwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

juu ya taifa kama hili?

105:10 Yer 39:8; 4:27; Amo 9:8“Piteni katika mashamba yake ya mizabibu na kuyaharibu,

lakini msiangamize kabisa.

Pogoeni matawi yake,

kwa kuwa watu hawa sio wa Bwana.

115:11 1Fal 19:10; Yer 3:20; Za 73:27; Isa 24:16Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda

wamekuwa si waaminifu kwangu kamwe,”

asema Bwana.

125:12 Yer 23:17; 2Nya 36:16; Yer 28:7; Isa 28:15; Yer 14:13Wamedanganya kuhusu Bwana.

Wamesema, “Yeye hatafanya jambo lolote!

Hakuna dhara litakalotupata;

kamwe hatutaona upanga wala njaa.

135:13 Yer 14:15; 2Nya 36:16; Ay 6:26Manabii ni upepo tu, wala neno halimo ndani yao,

kwa hiyo hayo wayasemayo na yatendeke kwao.”

145:14 Hos 6:5; Yer 1:9; 23:9; Za 39:3Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote:

“Kwa sababu watu hawa wamesema maneno haya,

nitayafanya maneno yangu vinywani mwenu kuwa moto,

na watu hawa wawe kuni

zinazoliwa na huo moto.

155:15 Kum 28:49; Isa 5:26; 2Fal 24:2; Isa 28:11; Mwa 11:7Ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana,

“Ninaleta taifa toka mbali dhidi yako,

taifa la kale na linaloendelea kudumu,

taifa ambalo lugha yao huijui,

wala msemo wao huwezi kuuelewa.

165:16 Ay 39:23Podo zao ni kama kaburi lililo wazi,

wote ni mashujaa hodari wa vita.

175:17 Yer 30:16; Law 26:16; Yer 50:7-17; Kum 28:31-33; Yer 8:16; Hes 16:14; Hos 2:12Watayaangamiza mazao yenu na chakula chenu,

wataangamiza wana wenu na mabinti zenu;

wataangamiza makundi yenu ya kondoo na ya ngʼombe,

wataangamiza mizabibu yenu na mitini yenu.

Kwa upanga wataangamiza

miji yenye maboma mliyoitumainia.

18“Hata hivyo katika siku hizo, sitakuangamiza kabisa,” asema Bwana. 195:19 Kum 29:24-26; 4:28; Yer 15:4; 13:22; 1Fal 9; 9; Yer 16:13“Nao watu watakapouliza, ‘Kwa nini Bwana, Mungu wetu ametufanyia mambo haya yote?’ utawaambia, ‘Kama vile mlivyoniacha mimi na kutumikia miungu migeni katika nchi yenu wenyewe, ndivyo sasa mtakavyowatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.’

20“Itangazie nyumba ya Yakobo hili

na ulipigie mbiu katika Yuda:

215:21 Isa 6:10; Eze 12:2; Mdo 28:26; Isa 42:20; Mk 8:18; Kum 32:6; Yer 4:22; Hes 2:18Sikieni hili, enyi watu wapumbavu, msio na akili,

mlio na macho lakini hamwoni,

mlio na masikio lakini hamsikii:

225:22 Kum 28:58; Ay 4:14; Isa 64:2; Za 46:3Je, haiwapasi kuniogopa mimi?” asema Bwana.

“Je, haiwapasi kutetemeka mbele zangu?

Niliufanya mchanga kuwa mpaka wa bahari,

kizuizi cha milele ambacho haiwezi kupita.

Mawimbi yanaweza kuumuka, lakini hayawezi kuupita;

yanaweza kunguruma, lakini hayawezi kuuvuka.

235:23 Kum 21:18; Za 14:3Lakini watu hawa wana mioyo ya ukaidi na ya uasi,

wamegeukia mbali na kwenda zao.

245:24 Mt 5:45; Yoe 2:23; Mwa 8:22; Mdo 14:17; Kum 6:24; Yak 5:7Wao hawaambiani wenyewe,

‘Sisi na tumwogope Bwana Mungu wetu,

anayetupatia mvua za masika na za vuli kwa majira yake,

anayetuhakikishia majuma ya mavuno kwa utaratibu.’

25Matendo yenu mabaya yamezuia haya yote,

dhambi zenu zimewazuia msipate mema.

265:26 Za 10:8; Mit 1:11; Mt 7; 15; Mhu 9:12; Yer 9:8; Mik 7:2“Miongoni mwa watu wangu wamo walio waovu

wanaovizia kama watu wanaotega ndege,

na kama wale wanaoweka mitego

kuwakamata watu.

27Kama vitundu vilivyojaa ndege,

nyumba zao zimejaa udanganyifu;

wamekuwa matajiri na wenye nguvu,

285:28 Kum 32:15; Zek 7:10; Kut 22:21-24; Amo 5:12; Za 73:12; 82:3wamenenepa na kunawiri.

Matendo yao maovu hayana kikomo;

hawatetei mashauri ya yatima wapate kushinda,

hawatetei haki za maskini.

29Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya hili?”

asema Bwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

juu ya taifa kama hili?

305:30 Yer 18:13; Hos 6:10; Yer 23:14“Jambo la kutisha na kushtusha

limetokea katika nchi hii:

315:31 Eze 13:6; Isa 30:10; Mik 2:11; Mao 4:13; Hos 9:5Manabii wanatabiri uongo,

makuhani wanatawala kwa mamlaka yao wenyewe,

nao watu wangu wanapenda hivyo.

Lakini mtafanya nini mwisho wake?

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Jeremías 5:1-31

La corrupción de Jerusalén y de Judá

1«Recorred las calles de Jerusalén,

observad con cuidado,

buscad por las plazas.

Si encontráis una sola persona

que practique la justicia y busque la verdad,

yo perdonaré a esta ciudad.

2Aunque juran: “Por la vida del Señor”,

de hecho juran en falso».

3Señor, ¿acaso no buscan tus ojos la verdad?

Golpeaste a esa gente, y no les dolió,

acabaste con ellos, y no quisieron ser corregidos.

Endurecieron su rostro más que una roca,

y no quisieron arrepentirse.

4Entonces pensé: «Así es la plebe;

siempre actúan como necios,

porque no conocen el camino del Señor

ni las demandas de su Dios.

5Me dirigiré a los líderes

y les hablaré;

porque ellos sí conocen el camino del Señor

y las demandas de su Dios».

Pero ellos también quebrantaron el yugo

y rompieron las ataduras.

6Por eso los herirá el león de la selva

y los despedazará el lobo del desierto;

frente a sus ciudades está el leopardo al acecho,

y todo el que salga de ellas será despedazado,

pues son muchas sus rebeliones

y numerosas sus infidelidades.

7«¿Por qué habré de perdonarte?

Tus hijos me han abandonado,

han jurado por los que no son dioses.

Cuando suplí sus necesidades,

ellos cometieron adulterio

y en tropel se volcaron a los prostíbulos.

8Son como caballos bien cebados y fogosos;

todos relinchan por la mujer ajena.

9¿Y no los he de castigar por esto?

—afirma el Señor—.

¿Acaso no he de vengarme de semejante nación?

10»Subid por los surcos de esta viña

y arrasadla, pero no acabéis con ella.

Arrancadle sus sarmientos,

porque no son del Señor.

11Pues las casas de Israel y de Judá

me han sido más que infieles»,

afirma el Señor.

12Ellas han negado al Señor,

y hasta dicen: «¡Dios no existe!

Ningún mal vendrá sobre nosotros,

no sufriremos guerras ni hambre».

13Los profetas son como el viento:

la palabra del Señor5:13 del Señor (LXX); TM no incluye esta frase. no está en ellos.

¡Que así les suceda!

14Por eso, así dice el Señor,

el Dios Todopoderoso:

«Por cuanto el pueblo ha hablado así,

mis palabras serán como fuego en tu boca,

y este pueblo, como un montón de leña.

Ese fuego los consumirá.

15»Pueblo de Israel,

voy a traer contra vosotros una nación lejana,

una nación fuerte y antigua,

una nación cuyo idioma no conocéis,

cuyo lenguaje no entendéis

—afirma el Señor—.

16Todos ellos son guerreros valientes;

sus flechas presagian la muerte.

17Acabarán con tu cosecha y tu alimento,

devorarán a tus hijos e hijas,

matarán a tus rebaños y ganados,

y destruirán tus viñas y tus higueras.

Tus ciudades fortificadas,

en las que pusiste tu confianza,

serán pasadas a filo de espada.

18»Sin embargo, aun en aquellos días no os destruiré por completo —afirma el Señor—. 19Y, cuando te pregunten: “¿Por qué el Señor, nuestro Dios, nos ha hecho todo esto?”, tú les responderás: “Así como vosotros me habéis abandonado y en vuestra propia tierra habéis servido a dioses extranjeros, así también en tierra extraña serviréis a gente extranjera”.

20»Anunciad esto entre los descendientes de Jacob

y proclamadlo en Judá:

21Escucha esto, pueblo necio e insensato,

que tiene ojos, pero no ve,

que tiene oídos, pero no oye.

22¿Acaso has dejado de temerme?

—afirma el Señor—.

¿No debieras temblar ante mí?

Yo puse la arena como límite del mar,

como frontera perpetua e infranqueable.

Aunque se agiten sus olas,

no podrán prevalecer;

aunque bramen,

no franquearán esa frontera.

23Pero este pueblo tiene un corazón terco y rebelde;

se ha descarriado, ha sido infiel.

24No reflexionan ni dicen:

“Temamos al Señor, nuestro Dios,

quien a su debido tiempo nos da lluvia,

las lluvias de otoño y primavera,

y nos asegura las semanas señaladas

para la cosecha”.

25Vuestras iniquidades

os han quitado estos beneficios;

vuestros pecados os han privado

de estas bendiciones.

26Sin duda, en mi pueblo hay malvados,

que están al acecho como cazadores de aves,

que ponen trampas para atrapar a la gente.

27Como jaulas llenas de pájaros,

llenas de engaño están sus casas;

por eso se han vuelto poderosos y ricos,

28gordos y pedantes.

Sus obras de maldad no tienen límite:

no hacen justicia al huérfano,

para que su causa prospere;

ni defienden tampoco

el derecho de los menesterosos.

29¿Y no los he de castigar por esto?

¿No he de vengarme de semejante nación?

—afirma el Señor—.

30»Algo espantoso y terrible

ha ocurrido en este país.

31Los profetas profieren mentiras,

los sacerdotes gobiernan a su antojo,

¡y mi pueblo tan campante!

Pero ¿qué vais a hacer vosotros

cuando todo haya terminado?